• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Operesheni Ondoa Mifugo Kagera Yasonga Mbele Sasa Ng’ombe Wasakwa Kwa Ndege Zisizokuwa na Rubani Kila Pembe ya Hifadhi

Imewekwa : April 8th, 2017

Operesheni Ondoa Mifugo Kagera Yasonga Mbele Sasa Ng’ombe Wasakwa Kwa Ndege Zisizokuwa na Rubani Kila Pembe ya Hifadhi

Operesheni ondoa mifugo katika Hifadhi za Misitu na Mapori ya Akiba Mkoani Kagera yaendelea kwa kasi ambapo tangu kuanza kwa operesheni hiyo Machi 31, 2017 hadi kufikia Aprili 7, 2107 tayari  mifugo 4489 imekamatwa na watuhumiwa wa makosa mbalimbali 115 wametiwa mbaloni.

Mifugo iliyokamatwa ni pamoja na Ng’ombe 4328, Mbuzi 125 na Kondoo 36. Pia watuhumiwa 115 waliokamatwa kwa makosa mbalimbali  Watanzania ni 109, Warundi 4 na Wanyarwanda 2. Aidha Ng’ombe 144, kondoo 17 na mbuzi 113 wametaifishwa na Serikali baada ya watuhumiwa kushindwa kesi zao na Mahakamani kuiamurisha Serikali kutaifisha mifugo hiyo.

Serikali ya Mkoa wa Kagera katika kuhakikisha zoezi la operesheni linafanikiwa kwa asilimia 100%  imeanza  kutumika ndege zisizotumia Rubani (Drones) pia na ndege zinazotumia Rubani ili kukagua maeneo yote ambayo siyo rahisi kuonwa au kufikika na vikosi vya nchi kavu ambako mifugo hufichwa na wavamizi na kuendesha shuguli za kinadamu.

Akirusha ndege isiyotumia Rubani katika kituo Kiteule cha Nyakanazi  Bw. Parmena Pallangyo Afisa Wanyamapori kutoka Pori la Akiba la Lwikwika Lumesule lililopo Wilayani Masasi Mkoani Mtwara alisema ndege hizo zina uwezo wa kusafiri zaidi ya Kilometa 10 kwa muda mfupi zikiwa zinapiga picha mnato na picha za video kwa kuonesha viwianishi (coordinates) za kila eneo kila kitu kilichopo ardhini.

“Badala ya kuangaingaka na kutumia rasilimali magari, mafuta au rasilimali watu kwenda kutafuta mifugo katika maeneo ambayo hatuna uhakika, tunazituma kwanza ndege hizi zinatuletea taarifa za picha na eneo walipo mifugo pia picha hizo zinakuwa na viwianishi (coordinates) ambazo zinatusaidia kujua eneo husika ndipo sasa vikosi vinaelekezwa eneo husika na kwa kutumia kifaa kiitwacho GPS huwawezesha  kukamata mifugo hiyo.” Alifafanua Bw. Parmena

Wafugaji na Wafanyabiashara wa Ng’ombe wasemaje?

Katika Mnada wa Ng’ombe wa Rusahunga ambao hufanyika kila siku ya Alhamisi kila wiki wanunuzi wa Ng’ombe wanasema kuwa kwasasa Ng’ombe wanapatikana kwa wingi katika Mnada. Bw. Sena Elias Magoma mnunuzi  aliseam kuwa kwa Ng’ombe aliyekuwa anauzwa bei ya shilingi 1,200,000/=  wiki mbili zilizopita kwasasa anauzwa bei ya shilingi 800,000/= hadi 700,000/= na aliyekuwa anauzwa shilingi 500,000/= kwasasa anauzwa shilingi 300,000/= hadi 250,000/=.

Naye Bw. Fikiri Matenya Mashine  ambaye ni mfugaji alisema kuwa katika mnada huo kwa sasa Ng’ombe ni wengi kiasi kwamba bei imeshuka sana na wafugaji wanawarudisha ng’ombe wao nyumbani kwakukosa soko. Akiulizwa sababu ya ngo’ombe kuwa wengi katika mnada huo wa Rusahunga kwasasa na bei kushuka alisema;

“Mimi nadhani kutokana na ‘parancha’  (akimaanisha operesheni) linaloendelea huko maporini ndiyo maana ng’ ombe wamekuwa wengi katika mnada na pengine matajiri wanasubiri mnada wa ng’ombe ambao Serikali imewakamata ili wawanunue kwenye mnada kwa bei ya chini sana. Lakini mimi naona Serikali imefanya jambo jema hawa Wafugaji kutoka nje ya nchi wanatunyanyasa sana kama watondoka mimi naamini kuwa malisho yatatutosha sisi wenyeji.” Alifafanua Bw. Mashine

Aidha, Afisa Mifugo anayesimamia Mnada wa Rusahunga Bw. Raphael Barakekenwa alisema kwa kipindi hiki cha operesheni mifugo hasa ng’ombe wamekuwa wengi mno kiasi kwamba wanakosa soko lakini Serikali kuu na Halmashauri zinapata mapato ya kutosha kutokana na wingi wa ng’ombe mnadani. Pia alitoa angalizo kuwa kwa wiki mbili au tatu zijazo huenda kukawa na uhaba mkubwa wa nyama sokoni kwasababu ng’ombe wengi kuondolewa maporini na kusafishwa kwenda mikoani na nje ya nchi.

Vilevile katika mnada huo Mwandishi wa habari hii alishuhudia malori mengi yakiwa yanapakia ng’ombe kwa wingi na kuondoka kuelekea mikoani pia ng’ombe wengi wakiwa katika eneo hilo la mnada wa Rusahunga wakisubiri kununuliwa aidha wafugaji wengine wakiamua kurudi nyumbani na ng’ombe wao waliokosa soko katika mnada huo.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa