• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Operesheshi Mkoani Kagera yanasa Mifugo 3053, Watuhumiwa 19, Watano watiwa Hatiani

Imewekwa : April 3rd, 2017

Operesheni ya Kunusuru Hifadhi za Misitu na Mapori ya Akiba Kagera Yanasa Mifugo 3053 na Kuwatia Hatiani Watuhumiwa Watano

Operesheni ya kuondoa wavamizi na waharibifu wa Mapori ya Akiba, Hifadhi za Misitu, Mapori Tengefu na Maeneo ya vyanzo vya maji Mkoani Kagera tayari imekamata jumla ya mifugo 3,053 na kukuwakamata watuhumiwa 19 ambao tayari wamefikishwa katika Mahakama  ya Wilaya ya Biharamulo April 3, 2017

Operationi ya kunusuru Misitu ya Hifadhi na Mapori ya Akiba Mkoani Kagera imeanza rasmi Machi 30, 2017 mara baada ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu  kutoa muda wa siku tatu kuanzia Machi 18-21, 2017 kwa wavamizi wote kuondoka na kuondoa mifugo yao kwa hiari  katika hifadhi hizo.

Mara baada ya muda wa kuondoka na kuondoa kwa hiari mifugo kuisha na operesheni kuanza,  Mifugo iliyokamatwa kwenye Hifadhi za Misitu na Mapori ya Akiba Mkoani Kagera ni Pamoja na Ng’ombe 2905, Mbuzi 113, na Kondoo 35 ambapo kazi inaendelea kufanyika kuhakikisha hakuna mvamizi yeyote atakayebaki katika Hifadhi hizo.

Hatua Zilizochukuliwa

Watuhumiwa 19 tayari wamekamatwa na kufikishwa Makamani kwa makosa mbalimbali ya kuendesha shughuli za kibinadamu katika Misitu ya Hifadhi na Mapori ya Akiba ambapo akitoa ufafanuzi mara baada ya kutoka Mahakamani Wakili wa Serikali Mwandamizi Athumani Matuma Kirati akiambatana na Mawakili wenzake wawili wa Serikali Erastus Anosisye na Haruna Shomari alisema;

“Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kufikia April 2, 2017 ilikuwa imepokea mafaili 12 yanayohusiana na makosa mbalimbali katika Hifadhi za Wanyamapori na Hifadhi za Misitu ambapo watuhumiwa 19 wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya kwa makosa ya kuingia bila kibali katika hifadhi, kuchunga mifugo katika hifadhi za Misitu na Wanyamapori, kukutwa na mazao ya Misitu bila kibali na kukutwa na zana za kuvunia mazao ya misitu kama misumeno na shoka.” Alifafanua Wakili Matuma.

Makosa mengine ni kukutwa na vifaa vya kusafirishia mazao ya misitu kama baiskeli,  na kuvuna mazao ya misitu (Kambapori) bila kibali au idhini ya mamlaka husika. Katika kesi hizo 12 zilizofikishwa mahakamani kesi tatu tofauti zilimalizika kwa watuhumiwa watano kukiri makosa yao na kutozwa faini ya shilingi 100,000/= (laki moja) hadi shilingi 500,000/= (laki tano) au kifungo cha mwaka mmoja kwa kila kosa.

Pia Wakili Mwandamizi Matuma alisema ofisi ya Mwanansheria Mkuu wa Serikali inaendelea kupokea mafaili mengine ya kesi na mara baada ya kuyapitia na kukaridhika na vielelezo  vya ushahidi watawasilisha kesi hizo Mahakamani. Kesi tatu zilizokamilika na kutolewa hukumu na Mahakama ni Kesi namba 83, 85, 79 za mwaka 2017 ambapo jumla ya watuhumiwa watano walikiri makosa yao na kuhukumiwa kamailivyotajwa hapo juu.

Kuhusu mifugo iliyokamatwa Wakili Mwandamizi wa Serikali Bw. Matuma alisema kuwa Mahakama itatoa uamuzi mara baada ya kutembelea maeneo ya mifugo ilikokamatiwa na kuhifadhiwa katika hifadhi ili kujionea na kukubali kiwe kielelezo cha ushahidi. Kesi zote 12 ziliskilizwa na tatu kutolewa uamuzi na  Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Biharamulo Niku Mwakatobe.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa