• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Picha ya Pamoja ya Wadau wa Chanjo MKoani Kagera Wakati wa Kikao cha Kujadili Chanjo Mpya ya Saratani ya Mlango wa Kizazi Kwa Akinamama

Imewekwa : April 18th, 2018

Wadau Mkoani Kagera Waweka Mikakati ya Kutoa Chanjo Mpya ya Saratani ya Mlango wa Kizazi Kwa Wasichana Waliotimiza Umri wa Miaka 14

Wadau wa wa Chanjo Mkoani Kagera wafanya kikiao cha kujadili namna bora ya kuanzisha na kutekeleza  kwa ufanisi  chanjo mpya ya Saratani ya Mlango wa Kizazi kwa wasichana wenye umri miaka 14 ambapo mkoa unatarajia kuchanja jumala ya wasichana 35,917 katika vituo vya kutolea huduma za Afya  1,182.

Akifungua kikao hicho  Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mhe. Deodatus Kinawilo kwaniaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera  aliwasisitiza wajumbe wa kikao kuhakikisha wanawahamasisha wananchi hasa wazazi kuwaruhusu watoto wao wasichana wenye umri  wa miaka 14 kupata chanjo hiyo ambayo ni muhimu sana kwao na inatolewa bure bila malipo yoyote.

Mkuu wa Mkoa alisema kuwa  Saratani ya Mlango wa Kizazi ni ugonjwa wa kwanza Tanzania unaowaua akinamama wengi ukifuatiwa na Saratani ya Matiti, ambapo aliwasisitiza wajumbe wa kikao kuhakikisha wanawahamasisha wazazi katika maeneo yao  ili watoto wao wapate chanjo hiyo na kupunguza vifo kwa akina mama hapo mbeleni.

“Serikali ya mkoa imejipanga vizuri katika kutoa chanjo ya Saratani ya Mlango wa Kizazi kwa wasichana 35,917 katika mkoa wetu. Aidha, chanjo hiyo itatolewa katika vituo 1,182 vya kutolea huduma za afya vya Serikali na visivyokuwa vya Serikali pamoja na baadhi ya shule zitakazokuwa zimeainishwa,” Alitoa Msisitizo Mhe. Kinawilo.

Naye Dk.Siliacus Mtabuzi mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) akitoa salaam za Shirika hilo aliupongeza Mkoa wa Kagera kwa kufanya vizuri katika chanjo mbalimbali na kusema kuwa ni matarajio yake kuwa katika Chanjo hii mpya  ya Kizazi cha Saratani ya Mlango wa Kizazi kwa wasichana wenye umri wa miaka 24 Mkoa wa Kagera utafanya vizuri zaidi kwa kuwafikia walengwa wote.

Katika hatua nyingine Dk. Mtabuzi alisema kuwa Shirika la Afya Duniani (WHO) kama mdau Mkuu wa Afya litaendelea kushirikiana kwa karibu sana na Mkoa wa Kagera ili kuhakikisha lengo la mkoa linafikiwa na wasichana wenye umri wa miaka 14 ambao ni akinamama wa kesho wasidhurike na Saratani ya Mlango wa Kizazi.

Mganaga Mkuu wa Mkoa Dk. Thomas Rutachunzibwa alifafanua namna chanjo hiyo itakvyotolewa katika Mkoa wa Kagera kwa kusema kuwa chanjo itaanza kutolewa tarehe 23 Aprili, 2018 na lengo likiwa ni kuwafikia wasichana 35,917 waliotimiza miaka 14 ambao walizaliwa kipindi cha Januari hadi Aprili 2004 na baada ya hapo zoezi litakuwa endelevu kwa wasichana watakaokuwa wanatimiza miaka 14 kila mwezi  watakuwa wanapewa chanjo hiyo.

Kwa niaba ya Wakuu wa Wilaya Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mhandisi Richard Luyango alitoa rai kwa wananchi ambao  watajaribu kupotosha utoaji wa chanjo hiyo kuwa Kamati za Ulinzi na Usalaama zitamshughulikia kwa kuwachukulia hatua kali za kisheria mahala popote atakapokuwa.

Dalili za ugonjwa wa Saratani ya Mlango wa Kizazi ni kuishiwa damu, figo kushindwa kufanya kazi, kuvimba miguu, kutokwa na usaha wa rangi ya kahawia katika sehemu za siri za mwanamke. Aidha, visababishi vya ugonjwa huo ni kuanza mapenzi katika umri mdogo, kuwa na wapenzi wengi, na kuvuta sigara.

Ili kujikinga na ugonjwa wa Saratani ya Mlango wa Kizazi ni muhimu sana wasichana wakazingatia kutojihusisha na visababishi vilivyotajwa hapao juu. Pia Katika Mkoa wa Kagera kuna vituo vipatavyo 56 vinavyohusika na uchunguzi wa awali wa ugonjwa wa Saratani ya Mlango wa Kizazi ambapo mkoa unatoa wito  kwaakina mama kuwahi mapema katika vituo hivyo pale wanapohisi dalili hizo ili kufanyiwa uchunguzi mapema.

Kikao cha wadau wa chanjo Mkoani Kagera kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera Aprili 18, 2018 kiliwahusisha Wakuu wa Wilaya, Wenyeviti wa Halmashauri za Wilaya, Waganga Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi  Watendaji wa Halmashauri, Maafisa Elimu wa Wilaya, Wadau wa Maendeleo wa Afya wa Mkoa wa Kagera, Wataalamu mbalimbali kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa na na Wataalamu wa Afya kutoka katika Halmashauri za Wilaya.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa