• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Prof. Joyce Ndalichako Akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Kijuu Funguo za Majengo ya Shule ya Msingi Mgezo Mseto Yaliyojengwa na UNICEF

Imewekwa : February 15th, 2018

Waziri Ndalichako Akabidhiwa na Majengo na Shule na Unicef Awaagiza TBA Kulipa Madeni na Kumaliza Mradi wa Ihungo Sekondari

Katika Siku yake ya pili Mkoani Kagera Waziri Ndalichako  alipokea majengo yaliyojengwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la UNICEF katika Shule ya Msingi Mgeza Mseto ambapo  pia alikabidhi majengo hayo kwa Mkuu wa mkoa wa Kagera Mhe. Kijuu naye pia aliyakabidhi majengo hayo kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Bukoba.

Katika hafla hiyo fupi Prof. Ndalichako aliwashukuru UNICEF kwa kuitikia wito wake baada ya Tetemeko lililotokea Septemba 10, 2016 ambapo aliwaomba kutoa msaada katika Sekta ya Elimu kwani miundombinu mingi ilikuwa imeadhirika, na UNICEF walikubali kutoa milioni 700 kwaajili ya Shule ya Msingi Mugeza Mseto.

UNICEF imejenga Madarasa 3, Jengo 1 la kuwapumzisha wanafunzi watakaokuwa wanaumwa, Mabweni 4 yenye uwezo wa kubeba wanafunzi 190, Vyoo 2. Pia wametekeleza mradi wa maji wenye thamani ya milioni 107 na kujenga matundu ya vyoo yenye thamani ya milioni 500 katika shule mbalimbali ndani ya Manispaa ya Bukoba.

Waziri Ndalichako pia aliwashukuru wadau wengine ambao walichangia katika Shule ya Msingi Mgeza Mseto. Wadau hao ni Rotary Club waliotoa milioni 80 kwaajili ya kununulia magodoro, makabati na mashuka kwa ajili ya watoto wenye ulemavu ambao wanalala katika mabweni yaliyojengwa na UNICEF.

Bi Cecilia Baldeh Mwakilishi wa UNICEF anayeshughulikia masuala ya elimu kwa Watoto aliyemwakilisha Mwakilishi Mkazi wa UNICEF Tanzania  akiongea na wanafunzi na wananchi waliohudhuria katika hafla hiyo fupi alisema kuwa UNICEF iliguswa na uhuhitaji wa shule hiyo baada ya Tetemeko kutokea mwaka 2016 na ndiyo maana waliamua kutoa fedha ili kupunguza changamoto katika shule hiyo yenye mahitaji maalum.

Pia Bi Cecilia alisema kuwa anatambua kuwa bado kuna changamoto katika shule ambapo hakuna njia za kutembelea (walka way), usafiri wa wanafunzi, nyumba za watumishi wanaowalea watoto, uzio na vifaa vya michezo ambapo alitoa wito kwa mashirika ya Kimataifa kuguswa kuchangia ili watoto hao wenye uhuhitaji maalum waishi kwenye mazingira bora zaidi.

Shule ya Msingi Mgeza Mseto ilianza mwaka 1950 ikiwa Middle School na baadae ilibadilishwa kuwa shule watoto wenye mahitaji Maalum miaka ya 1960 katika shule hiyo kuna watoto wenye mahitaji maalum 150. Manispaa ya Bukoba inazo Shule zenye mahitaji maalum 3, Shule ya Msingi Tumaini, Shule ya Msingi Mgeza Viziwi na Shule ya Msingi Mgeza Mseto.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera aliwashukuru UNICEF pamoja na Waziri Ndalichako kwa ufadhili wao wa kuhakikisha miundombinu ya shule hiyo inaimarishwa na kuonesha moyo wa kusaidia mara baada ya Tetemeko kutokea mwaka 2016  ambapo alisema kuwa wananchi wa Kagera walifarijika na wataendelea kufarijika kwa kuona miundombinu ya shule zao inarejeshwa na inaimarishwa zaidi kuliko hata mwanzo.

Ihungo Sekondari, Mara baada ya Hafla ya Makabidhiano Shule ya Msingi Mugeza Mseto Waziri Ndalichako alitembelea Shule ya Sekondari Ihungo kuona maendeleo ya ujezi wa shule hiyo ambapo aliridhishwa sana na kiwango cha ujenzi wa shule hiyo na kuwapongeza wajenzi Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kwa kujenga shule hiyo kwa viwango vya hali ya juu sana.

Pamoja na pongezi hizo Waziri Ndalichako aliwataka TBA kuhakikisha wanakamilisha ujenzi huo mara moja ili wanafunzi waweze kurejea katika shule yao na kuendelea na masomo yao. Pia Waziri Ndalichako alisema kuwa Wizara yake tayari imetoa bilioni 9.13 kati ya bilioni 10.48 fedha za kutekeleza mradi mzima wa Ihungo Sekondari.

Waziri Ndalichako alisema hayo baada ya kupokea taarifa ya Meneja wa TBA Mkoa wa Kagera  Mhandisi Salum Chanzi kuhusu mradi huo na kusikia kuwa kuna wazabuni , vibarua na mafundi wanaodai fedha zao baada ya kutoa huduma za vifaa mbalimbali vya ujenzi na huduma katika ujenzi huo wa Ihungo.

Wizara yangu tayari imetoa kiasi kikubwa cha fedha  bilioni 9.13 na tumebaki tunadaiwa milioni 715 tu na fedha iliyobaki ni asilimia 5% itakayolipwa baada ya kujihakikishia kuwa kila kitu kimekamilika. Nawataka TBA kumaliza mradi pia kuhakikisha wanawalipa wanaowadai na siyo mapaka wamalize mradi kwani fedha wanayo wao, Alisistiza Prof. Ndalichako.

Shule Sekondari Nyakato, Waziri Ndalichako pia alipata wasaa wa kutembelea Shule ya Sekondari Nyakato kuona maendeleo ya ujenzi wa shule hiyo  ambapo mjenzi ni SUMA JKT na ujenzi umefikia asilimia 60% kwa sasa baada ya kuanza Septemba 21, 2017 na unatarajia kukamilika Septemba 20, 2018.

Waziri Ndalichako aliwapongeza SUMA JKT kwa kujenga majengo ya shule hiyo kwa viwango lakini pia kwa kwenda na muda ambao ujenzi unatarajia kukamilika. Ujenzi wa Shule ya Sekondari Nyakato utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 2.2 Ikumbukwe kuwa Shule za Sekondari Ihungo na Nykato ziliathiriwa vibaya na Tetemeko la Ardhi mwaka 2016 na zinajengwa upya na Serikali.

Waziri Ndalichako pia alizitembelea Shule za Sekondari Omumwani Rugambwa na kuongea na wanafunzi na uongozi wa shule hizo huku akisistiza wanafunzi kuongeza bidii katika masomo yao.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa