• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Profesa Kamuzora Afanya Ziara Visiwani Awaelimisha Wavuvi Kuzingatia Ubora Katika Uchakataji wa Mazao ya Samaki

Imewekwa : April 3rd, 2019

Katibu Tawala Mkoa wa Kagera Profesa Faustin Kamuzora katika kusimamia maendeleo ya mkoa kupitia sera ya kila mwananchi kujikwamua kiuchumi kwa kuzalisha na kujiingizia kipato halali kupitia kazi anayoifanya atembelea na kukagua miradi ya maendeleo Visiwani Wilayani Muleba na kuongea na wavuvi kwa kuwaelimisha juu ya uvuvi wa kisasa wenye tija na kukuza uchumi.

Akifanya ziara ya siku mbili Machi 28 hadi 29, 2019 katika visiwa vinne vya Kimoyomoyo, Mulumo, Kassenyi, na Chakazimbwe katika Kata za Mazinga na Ikuza Prof. Kamuzora alikagua miradi ya maendeleo hasa ujenzi wa ghati katika visiwa hivyo na kushauri miradi hiyo isimamiwe vizuri na ujenzi uzingatie viwango vya ujenzi ili mara baada ya kukamilika ziweze kudumu zaidi ya miaka 100.

Pamoja na kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo pia Prof. Kamuzora alimtembelea Bw. Issa Jiwa Mjasiliamali  anayechakata dagaa kwa kuowaongezea thamani na kuuza katika masoko ya ndani na nje ya nchi. Pia Prof. Kamuzora alijionea wavuvi wengine wanavyochakata mazao ya samaki hasa uanikaji wa dagaa.

Katika mikutano yake na wananchi waishio visiwani Prof. Kamuzora mara baada ya kutembelea na kukaua miradi ya maendeleo aliwaelimisha wananchi hao kuzingatia ubora wa mazoa wanayoyazalisha hasa ubora wa samaki au dagaa wanapochakatwa kabla ya kufikishwa sokoni.

Prof. Kamuzola alikaripia vikali wavuvi wanaoanika dagaa chini kuwa hairusiwi kufanya hivyo kwani dagaa wakianikwa chini kwenye mchanga ubora wake unapungua katika masoko ya ndani api masoko ya nje ya nchi. Dagaa hao huwa na mchanga jambo ambalo huleta usumbufu mkubwa kwa watumiaji.

“Hapa nchini Tanzania tuna tatizo kubwa la uharibifu baada ya mavuno (Post Harvest Loss) yaani unakuta mwananchi anahangaika kuzalisha bidhaa zake ili akauze sokoni lakini anashindwa kuziandaa bidhaa hizo katika hatua za mwisho wakati wakuzipeleka sokoni jambo ambalo linapelekea hasara kubwa kwa mhusika na wakati mwingine kusababisha madhara kwa watumiaji.” Alitahadharisha Prof. Kamzora

Prof. Kamzora aliwaagiza Maafisa Uvuvi na Maafisa Afya visiwani humo kuhakikisha wanatekeleza sheria ya uvuvi Namba 22 ya mwaka 2003 na kanuni zake za mwaka 2009 katika kusimamia masuala ya uvuvi na uchakataji wa mazao yake na kuchukua hatua kali kwa wale wote ambao wanaoendelea kukiuka sheria, taratibu na kanuni za uvuvi.

Pia Prof. Kamuzora akiongea na wananchi katika mikutano ya hadhara aliwaelimisha juu ya lishe hasa wazazi kuhakikisha wanapata elimu juu ya lishe ili kuondoa utapiamlo kwa watoto ambapo madhara ya utapiamlo ni makubwa katika makuzi ya watoto na madhara yake huonekana hata kama mtu akiwa mtu mzima.

Vilevile wananchi waishio visiwani walielimishwa kuhakikisha wanajiunga na bima ya afya iliyoboreshwa ili iweze kuwasaidia pale wanapokuwa wagonjwa au pale wanapokuwa wamepoteza uwezo wakufanya kazi kuvua samaki badala ya kurudishwa nyumbani nchi kavu badala yake wapatiwe matibabu au huduma ya afya hukohuko visiwani.

Katika hatua nyingine Prof. Kamuzora aliwapongeza wananchi katika visiwa alivyotembelea kwa kuchangia shilingi milioni 17 kwaajili ya ununuzi wa boti ya doria za ulinzi na kuwaomba kuendelea kuchangia ili boti hiyo yenye thamani ya jumla ya shilingi milioni 29 iweze kununuliwa na kuanza kazi mara moja kuondoa maharamia wanaowasumbua wavuvi katika shughuli zao.

Mwisho Prof. Kamzora aliwaasa wavuvi kuachana na uvuvi haramu au kutumia zana haramu katika kuvua ambapo alichoma nyavu haramu katika kisia cha Chakazimbwe. Pia aliwasisitiza wananchi kuendelea kushirikiana na Halmashaur ya Wilaya ya Muleba kutekeleza miradi ya maendeleo kama kujenga shule na zahanati ili wapate huduma nzuri za kijamii.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa