• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Rais Magufuli na Rais Museveni wa Uganda Wakikata Utepe Kuzindua Rasmi OSBP Mtukula.

Imewekwa : November 9th, 2017

Rais Magufuli na Museveni Wazindua Rasmi Kituo Cha Forodha Cha Huduma Kwa Pamoja Katika Mpaka wa Mtukula Kagera 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Uganda Yoweri Kaguta Museveni wazindua rasmi Kituo cha Forodha cha Huduma kwa Pamoja (OSBP) pande zote mbili Mtukula  mpakani mwa Tanzania na Uganda leo Novemba 9,  2017.

Mara baada ya kupokelewa na mwenyeji wake Rais Yoweri Kaguta Museveni na kupigiwa mizinga 21 na kuzindua  Kituo  cha Forodha cha Huduma kwa  Pamoja upande wa Tanzania Rais Magufuli akiongea na wananchi  katika mpaka wa Mtukula alisema kuwa lengo la kituo hicho ni kupunguza muda mwingi uliokuwa unapotezwa wakati wasafiri wakivuka mpaka kutoka nchi moja kwenda nchi nyingine.

Rais Magufuli alisema kuwa baada ya vituo hivyo kujengwa faida nyingi zimepatikana ambapo malori 400 hadi 700 yanayobeba  chakula cha msaada kuelekea katika nchi ya Sudani Kusini  hupita mpaka wa  Mtukula kwa mwezi kwasababu taratibu za kuvuka mpaka zimerahisishwa zaidi.

“Kabla ya vituo hivi kujengwa abiria alikuwa anachukua dakika 10 hadi 30 kuvuka lakini sasa abiria mmoja anatumia dakika 2 hadi 3 kuvuka,  kabla ya vituo hivi lori moja lilikuwa linatumia siku nzima kuvuka lakini kwasasa lori moja linatumia dakika 30 hadi saa moja,”  alisistiza Rais magufuli.

Pia Rais Magufuli alifafanua kuwa Kituo cha Forodha cha Huduma kwa  Pamoja(OSBP)  kimepunguza rushwa iliyokuwa kubwa mpakani na kuikosesha Serikali ya Tanzania Mapato lakini kwasasa baada ya kituo hicho kuanza kufanya kazi tangu Agosti 2015 mapato  yameongezeka  mfano  nchi ya Uganda mapato yameongezeka kwa asilimia 110%

Vilevile Rais Magufuli alisema kituo hicho kimeongeza Taasisi za Serikali zinazofanya kazi kwa pamoja kutoka Taasisi 6 hadi 16, pia fedha zinazokusanywa na TRA pamoja na Uhamiaji zinaingia mojakwamoja katika mfuko mkuu wa Serikali  ikiwa ni pamoja na taasisi zilizokuwa hazikusanyi  mapato mfano TBS  kwasasa wanankusanya mapato na tayari wamekusanya milioni 380.5 toka Novemba 2015 hadi sasa.

Mwisho Rais Magufuli alitoa shukrani  kwa Serikali ya Uingereza waliotoa fedha za kutekeleza mradi wa ujenzi wa vituo hivyo viwili kupitia Kampuni ya Trade Mark East Afrika, na ujenzi huo uligharimu shilingi bilioni 7.16 Pia alimshukuru Rais Mseveni kwa kukubali bomba la mafuta lenye urefu wa kilometa 1,415 kupita Tanzania na kuwataka Watanzania kuchangamkia fursa ya ajira katika ujenzi wa bomba hilo.

Katika Hatua nyingine Rais wa Jamhuri ya Uganda Yoweli Kaguta Museveni alimkaribisha Rais Magufuli na kumpongeza kwa kukubali mwaliko wake wa kwenda kuzindua bomba la Mafuta nchini Uganda pia na kukubali kushirikiana katika masuala mbalimbali ya kukuza uchumi wan chi mbili.

Rais Museveni alisema kuwa yeye kuja Tanzania kufanya uzinduzi wa Kituo cha Forodha cha Huduma kwa  Pamoja(OSBP) ni hija ya ukombozi kwake. Kwani  alisema kuwa hapo mwanzo alikuwa anakuja kwa siri ili kupanga mipango ya ukombozi wa nchi yake lakini sasa anakuja kuzindua miradi ya maendeleo wakati nchi yake ikiwa imekombolewa.

“Uwepo wa mpaka wa Mtukula na  Vituo vya Forodha vya kutolea Huduma kwa  Pamoja (OSBP) ni Ustawi wa Sekta (‘akabodo’ kwa kiganda) za Uchumi  ambapo ili wananchi watajirike na kupata ajira lazima Sekta nne zizingatiwe moja ikiwa ni Kilimo na kufuga kisasa, Pili ni Uchumi wa Viwanda, Tatu ni Huduma za jamii, na Nne ni Tehama. Hapo wananchi watapata ajira na kutajirika,” Alifafanua Rais Museveni.

Mwisho Rais Museveni alimshukuru Rais Magufuli kwa kukubali kuwapatia nishati ya umeme wananchi wa eneo la Nyangoma lililopo Wilayani Missenyi na kukwamua mradi wa umeme wa Mulongo Wilayani Kyerwa  ambapo mradi huo sasa unajengwa ili kuanza kuzalisha umeme.

Rais Magufuli na Rais Museveni wameelekea nchini Uganda kwenye sherehe za uzinduzi wa Bomba la mafuta kutoka Hoima Nchini Uganda hadi Tanga Tanzania. Aidha Rais Magufuli amehitimisha Ziara yake ya kikazi ya siku nne Mkoani Kagera leo Novemba 9, 2017  

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa