• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Rais Magufuli Pamoja na Viongozi Wengine Wakikata Utepe Kuashiria Kuwa Uwanja wa Ndege wa Bukoba Umezinduliwa Rasmi Novemba 6, 2017

Imewekwa : November 6th, 2017

Rais Magufuli Azindua Rasmi Uwanja Wandege wa Bukoba na Kuagiza Fedha za Fidia Omukajunguti Zihamishiwe Katika Uwanja Huo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika siku yake ya kwanza ziarani Mkoani Kagera azindua rasmi Uwanja wa Ndege wa Bukoba na kumuagiza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbalawa  kuhamisha shilingi Bilioni 9 za kulipa fidia kwa  wananchi ili kupisha ujenzi wa uwanja mpya wa Omukajunguti Wilayani Missenyi.

Rais Magufuli akiwahutubia wananchi katika Uwanja wa Ndege wa Bukoba aliouzindua leo Novemba 6, 2017 alisema kuwa ili kuutendea haki uwanja huo wenye urefu wa kilometa 1.5  na upana wa meta 30 na jengo zuri la abiria ambalo ni la tatu ukiacha majengo ya abiria ya Dar es Salaam na Kilimanjaro, Rais magufuli alisistiza kuwa lazima uwanja huo upanuliwe ili wananchi wa Kagera wafanye biashara.

“Kujenga uwanja mmoja wa ndege ni gharama kubwa mno ni mabilioni fedha, ili Mkoa huu ukue kiuchumi lazima tuupanue huu ambao umekamilika kwa kiwango kikubwa ili samaki zinazosindikwa hapa Bukoba zipakiwe hapa pamoja na ndizi na mazao mengine  vilevile na watalii wapiti hapa kwenda Burigi kutalii kuona wanyama na utalii uliopo  Kagera.” Alifafanua Rais Magufuli.

Rais Magufuri akifafanua zaidi alisema fedha zilizotengwa  kwenye bajeti ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano mwaka huu wa fedha 2017/2018 shilingi bilioni 9 kwa ajili ya fidia za wananchi Omukajunguti zinatosha kufanya upanuzi wa uwanja huo na kama zikipungua yeye ataongeza  ili uwanja upanuliwe na ndege kubwa za mizigo ziweze kutua na kupakia mizigo uwanjani hapo kuliko kuanza ujenzi  wa uwanja mpya ambao matumaini yake ya kukamilika ni madogo sana.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi  Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini Bw. Richard Muyongera  alisema kuwa Uwanja wa Ndege wa Bukoba  umejengwa na kukamilika kwa jumla ya gharama ya shilingi bilioni 31.95 ambapo Serikali ya Tanzania ilichangia shilingi bilioni 6.35 na fedha zilizobaki zaidi ya Bilioni 25 zilitolewa na Benki ya Dunia kama mkopo nafuu.

Bw. Muyongera alisema ujenzi wa uwanja huo ulihusisha ukarabati na upanuzi wa barabara ya kurukia ndege kwa urefu wa kilometa 1.5 na upana wa meta 30, Ujenzi wa maegesho ya ndege ambapo ndege tatu zinaegeshwa kwa wakati mmoja, Ujenzi wa jengo la abiria lenye uwezo wa kuhudumia abiria 500,000 kwa mwaka.

Ambapo jengo hilo limefungwa mifumo ya kisasa ya kuhudumia mizigo, mfumo kamera za usalama, maegesho ya magari 67 kwa pamoja , kituo cha kufua umeme na kuhamisha Shule ya Msingi Tumaini ambayo imejengwa upya kwa gharama ya shilingi bilioni 2.6 na imejengwa kisasa zaidi ya ile ya awali.

Naye Mwakilishi wa wa Benki ya Dunia Bw. Andre Bald alisema Benki ya Dunia iliamua kufadhili ujenzi wa Uwanja wa Bukoba kwa manufaa ya wananchi wa Bukoba ambapo alisema kuwa Shule ya Msingi Tumaini ilikuwa inahudumia Elimu Maalum na yeye aliguswa na ndiyo maana Benki ya Dunia iliamua  kugharamia ujenzi wa Shule mpya katika eneo la Mafumbo Manispaa ya Bukoba.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbalawa amewahasa wananchi wa Bukoba kuutunza Uwanja wa Ndege wa Bukoba na akayakaribisha Mashirika mengine ya Ndege kuanza safari zake Bukoba , kwasasa mashirika yanyofanya kazi uwanjani hapo ni Air Tanzania, Precision Air, na Auric Air.

Katika hatua nyingine Rais Magufuli amewahakikishia wananchi wa Bukoba kuwa tayari fedha za kununua meli mpya tayari zimepatikana na kutengwa ambapo tenda imeishatangazwa na Mkandarasi wa ujenzi wa meli mpya ni Nchi ya Korea Kusini na Mwezi Desemba 2017 au Januari 2018 Mkataba wa ujenzi wa meli mpya utasainiwa ili ujenzi uanze rasmi.

Pia Rais Magufuli  aliwahakikishia wakulima wa zao la kahawa  kuwa sasa zao hilo litapanda bei kwani tayari Serikali imefuta kodi 17 na sasa zao la kahawa linatakiwa kuwa na bei ya kuridhisha. Vilevile Rais Magufuli amewataka wananchi wa Kagera kuhakikisha wanatumia fursa ya Bomba la mafuta kutoka Uganda kujipatia ajira

Rais Magufuli ataendelea na ziara yake Mkoani Kagera Kesho Novemba 7, 2017 ambapo ataelekea Wilayani Karagwe kuzindua Barabara ya Kyaka Bugene na kuongea na wananchi wa Wilaya Karagwe.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa