• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Rais wa Burundi Mhe. Nkurunziza (Wakwanza Kushoto) Akiwa na Rais Magufuli Wilayani Ngara Mkoani Kagera Mbele ya Wananchi Kwenye Mkutano wa Hadhara.

Imewekwa : July 20th, 2017

Rais Magufuli Afanya Mazungumzo na Rais wa Burndi Nkurunziza na Kukubaliana Kufufua Fursa za Kiuchumi Kati ya Nchi Mbili

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli afufua rasmi mazungumzo ya Kiuchumi na Nchi ya Burundi baada ya kukuta na Rais wa Jamhuri ya Burundi Pierre Nkurunziza Wilayani Ngara Mkoani Kagera na kufanya naye mazungumzo ya kuanzisha ushirikiano wa kibiashara baina ya Tanzania na nchi ya Burundi.

Rais Dkt. Magufuli akiongea na wananchi baada ya kufanya mazungumzo na mgeni wake  Rais Nkurunziza alisema mwaka 2013 yalifanyika mazungumzo kati ya nchi za Tanzania na Burundi ambapo Mawaziri wa fedha wa nchi hizo  walikutanana na kuanzisha mazungumzo ya kibiashara kati ya nchi mbili ambapo kwasasa wamezungumza kufufua upya mazungumzo hayo ili kuanzisha ushirikiano wa kibiashara .

“Kwa takwimu za mwaka 2016 zinaonyesha kuwa biashara zilizokuwa zinafanyika kati ya Tanzania na Burundi zilikuwa zina thamani ya shilingi bilioni 116.5 ambazo biashara hizo ni kidogo sana ukilinganisha na watu milioni 50 Watanzania  na watu zaidi ya milioni 12 Warundi, kwahiyo kuna haja ya kukuza na kuimarsha biashara kati ya nchi zetu mbili.” Alifafanua Rais Dkt. John Magufuli.

Aidha, Rais Dkt. Magufuli alimpongeza Rais Nkurunziza kwa juhudi zake za kuendelea kuimarisha amani na usalama na kuwataka Wakimbizi kutoka nchi ya Burundi kurudi kwao kuijenga  nchi yao kwani tayari kuna amani na utulivu . Pia aliyakemea Mashirika ya kuwahudumia Wakimbizi kuacha kuwapotosha Wakimbizi hao kuwa kwao hakuna amani aidha, alisema kuwa tayari anajua kuwa Mashirika hayo ya Kimataifa yanatumia mwanya huo kuwatumia Wakimbizi kama Biashara.

Rais Dkt. Magufuli pia alimwagiza Waziri wa Mambo ya Ndani kuacha kutoa uraia kwa wakimbizi kuwa hicho kinaweza kuwa kivutio  kwa Wakimbizi kuendelea kuingia nchini Tanzania hata kama kwao hakuna vita.  Vilevile aliwataka Warundi kuishi kwa mshikamano kama Tanzania ambapo alisema kuwa hapo awali Tanzania ilikuwa na makabila 121 lakini kwa sasa kuna makabila 123 mawili yameongezeka  ambao ni Wahutu na Watutsi wapatao 200,000 waliopewa uraia  kuwa Watanzania.

Naye Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ya Tanzania Mwigulu Nchemba alipewa nafasi na Rais Dkt. Magufuli na  kusema kuwa kwasasa Wakimbizi kutoka nchi ya Burundi waliopo Tanzania ni 247,000 na tayari kuna Wakaimbizi 150,000 waliondoka kwa hiari yao na tayari wengine 5000 wamejiandikisha kurudi kwao kwa hiari.

Rais wa Jamhuri ya Burundi Pierre Nkurunziza akiwasalimia wananchi wa Wilaya ya Ngara na Watanzania kwa ujumla aliishukuru nchi ya Tanzania kwa ushirikiano mkubwa pamoja na nchi yake ya Burundi. Pia alisema kuwa katika mazungumzo yake na Rais Dkt. Magufuli yamefungua mwanzo mpya  wa fursa za kibiashara baina ya nchi mbili.

Vile vile  Rais Nkurunziza alitoa wito kwa Watanzania kuanza kufanya biashara na nchi yake ya Burundi na alisema kuwa anaona kuwa hapo mbele mambo yatakuwa sawasawa  kati ya nchi hizi mbili na watoto wa nchi hizo mbili watakuwa na mambo mazuri hapo mbeleni.

Aidha, Rais Nkurunziza  alitoa wito kwa Wakimbizi Warundi walioko nchini Tanzania kurudi kwao Burundi kwenda kushirikiana kuijenga nchi yao kwani amani imerejea kwa sasa hakuna vita tena. “Nawaomba Warundi wenzangui walipo mrudi nyumbani ili tukaijenge nchi  yetu na kukuza uchumi na tuweze kunufaika kwa pamoja na watoto wetu.  Alisistiza Rais Pierre Nkurunziza.

Katika Hatua nyingine Rais Dkt.  John Pombe Magufuli aliwaeleza wananchi wa Wilaya ya Ngara na taifa  kwa ujumla kuwa Serikali yake inaendelea kuwaletea maendeleo katika Sekta mbalimbali, mfano Katika Afya Serikali tayari imenunua vitanda vyenye thamani ya  Bilioni 33 na itavigawa katika Hospitali zote za Serikali nchini.

Aidha,  Serikali imenunua vifaa vya mahabara na na kuvigawa katika shule 1900, na imetenga shilingi bilioni 483 kwaajili ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya Juu. Vilevile  Serikali inatarajia kujenga upya barabara ya Nyanazi hadi Ngara ambayo ina mashimo mengi kwasasa na kujenga barabra ya Nyakahura Rulenge kilometa 92 kwa kiwango cha rami.

Katika Siku yake ya pili Rais Dkt. Magufuli Mkoani Kagera alimpokea kwa heshima zote za kitaifa Rais wa Jamhuri ya Burundi Pierre Nkurunziza katika uwanja mpira wa Lemela Wilayani Ngara majira ya saa 5:00 asubuhi na Rais Nkurunziza alipigiwa mizinga ya heshima 21 na kukagua Gwaride. Aidha, baada ya kukamilisha ziara yake na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Burundi Pierre Nkurunziza alirudi nchini Burundi.

Katika Mapokezi ya Rais wa Jamhuri ya Burundi Pierre Nkurunziza Rais Dkt. Magufuli aliambata na Mawaziri wa Wizara za Mambo ya Ndani Mwiguru Nchemba, Wizara ya Fedha Dk. Philip Mpango, Wizara ya Ulinzi Dkt. Hussein Mwinyi, Wizara ya Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbalawa, na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Naibu Wazi Dkt. Suzan Kolimba  pamoja na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama Kitaifa.

Rais Dkt. Magufuli amemaliza ziara yake ya siku mbili Mkoani Kagera na anatarajia kuelekea Mkoani Kigoma Juni 21, 2017 kuendelea na ziara yake ya kazi.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa