• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli

Imewekwa : November 4th, 2017

Rais Magufuli Kuwasili Mkoani Kagera Novemba 6, 2017

Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Joseph Pombe Magufuli atarajia kufanya ziara Mkoani Kagera kuanzia tarehe 06 hadi 09 Novemba, 2017.

Dhumuni la ziara ya Mhe. Rais Magufuli ni kuwatembelea wananchi wa Mkoa wa Kagera pia kutembelea na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo Mkoani hapa. Vilevile  Mhe. Rais Magufuli atapata fursa ya kuongea na wananchi  kwenye Mkutano wa Hadhara Uwanja wa Ndege wa Bukoba.

Mhe. Rais Magufuli atawasili Mkoani Kagera tarehe 06.11.2017 siku ya Jumatatu mchana na atapokelewa na viongozi mbalimbali wa Mkoa. Aidha Mhe. Rais Magufuli ataanza ziara yake siku hiyo ya tarehe 06.11.2017 katika Manispaa ya Bukoba kwa kuzindua Uwanja wa Ndege wa Bukoba saa 08:00 mchana. Aidha, mara baada ya uzinduzi Mhe. Rais ataongea na wananchi katika Mkutano wa Hadhara.

Tarehe 07.11.2017 siku ya Jumanne Mhe. Rais Magufuli ataelekea Wilayani Karagwe katika eneo la Nyakahanga na kuzindua Barabara ya Kyaka Bugene majira ya 03:00 Asubuhi na mara baada ya uzinduzi huo Mhe. Rais atasalimia wananchi.  

Vilevile Mhe. Rais Magufuli ataendelea na ziara yake Mkoani hapa tarehe 8.11.2017 siku ya Jumatano kwa kutembelea kiwanda cha Kagera Sukari Wilayani Missenyi ambapo atapata fursa ya kukagua mashamba ya miwa pia na kuongea na Wafanyakazi, Uongozi na Menejimenti ya Kiwanda hicho. 

Mhe. Magufuli atahitimisha ziara yake Mkoani Kagera tarehe 9.11.2017 siku ya Alhamisi katika Wilaya ya Missenyi kwa kuzindua Kituo cha Pamoja cha Forodha katika eneo la Mtukula mpakani mwa Tanzania na Uganda akiwa na Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Mseveni. Baada ya uzinduzi Ma-Rais wote watawasalimia wananchi.

 

Mkuu wa Mkoa wa Kgera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu anatoa wito kwa wananchi wote wa Mkoa wa Kagera kujitokeza kwa wingi kumpokea na kumshangilia Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sehemu zote atakazopita kuanzia Nyakabango Wilayani Muleba  mpakani mwa Mkoa wa Geita na Kagera pia na maeneo yote yaliyotajwa atakapokuwa anatembelea, anazindua miradi ya maendeleo, na atakapokuwa anaongea na wananchi.

Pia Mhe. Kijuu anawasisitiza wananchi wote kudumisha utulivu, amani na mshikamano pamoja na upendo kama ilivyo kawaida na desturi ya wananchi wa Mkoa wa Kagera wakati wanapotembelewa na wageni hasa ugeni mkubwa kama wa Mhe. Rais.

Aidha, Mhe. Kijuu anawahakikishia wananchi wote kuwa Vyombo vya Ulinzi na Usalama vipo imara na vinaendelea na kazi yake ya kudumisha amani na utulivu. Pia anatoa rai kuwaasa wananchi wote kujiepusha na vitendo vyote vya uvunjifu wa amaniambapo anasema kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya yeyote atakayethubutu kufanya vitendo vya uvunjifu wa amani.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa