• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Serikali Kupafanya Nyakanazi Biharamulo Kuwa Eneo la Kimkakati Katika Biashara ya Tanzania na Nchi Jirani – Waziri Mkuu Kassim Majaliwa

Imewekwa : September 18th, 2021

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Kassim Majaliwa Majaliwa  aanza rasmi ziara ya kikazi ya siku tano Mkoani Kagera akitarajia kutembele, kukagua, kuzindua au kuweka mawe ya msingi katika miradi kumi yenye thamani ya shilingi bilioni 927.3.

Mara baada ya kuwasili Mkoani Kagera Septemba 18, 2021 Wilayani Biharamulo katika eneo la Nyakanazi Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alikagua ujenzi wa mradi wa maegesho ya magari makubwa ya mizigo ynayosafirisha mizigo kutoka nchi jirani za Rwanda, Burundi na Congo DR ambapo mradi huo ukikamilika utagharimu takribani shilingi bilioni 2.6

Akiwa katika mradi huo na kukagua hatua ya utekelezaji wa mradi iliyofikiwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa hakuridhishwa na kasi ya Mkandarasi katika ujenzi kwani mradi ulitakiwa kuwa umekamilika mwezi Machi 2021 lakini hadi sasa mradi bado upo asilimia 47 tu ambapo Waziri Mkuu alitoa alimwagiza Mkuu wa Mkoa Kagera Meja Jenerali Charles Mbuge kusimamia kwa karibu mradi huo ukamilike ifikapo Novemba 23, 2021.

Aidha, akiongea na wananchi wa Nyakanazi Wilayani Biharamulo Waziri Mkuu Kassim majaliwa alisema kuwa Serikali inao mpango wa kulifanya eneo la Nyakanazi kuwa eneo la kimkakati kwa kuwa linapokea malori mengi ya mizigo kutoka Bandari ya Dar es Salaam kwenda nchi jirani  na kutoka nchi hizo kwenda Bandari ya Dar es Salaam na kukifanya eneo hilo kuwa kituo kikubwa cha biashara.

Pia Waziri Mkuu  aliuwagiza uongozi wa  Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo kulipangilia vizuri eneo la Nyakanazi na kulipima kwa kuwa ni eneo linalokaliwa na watu wengi na wananchi wanatakiwa kujenga kwa utaratibu na kuruhusu miundombinu mingine kupangiliwa vizuri ili kupanya Nyakanazi kuwa kitovu cha baiashara.

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliwahakikishia wananchi wa Nyakanazi kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan itajenga upya barabara ya Rusahunga Nyakahura Rusumo kwani barabara hiyo imeisha muda wake, ikiwa ni pamoja na barabara ya Nyakanazi Kibondo kilometa hamsini kukamilishwa ili Nyakanazi ifikikie kwa urahisi.

Katika namna ya kipekee wananchi wa Nyakahura Mzani Wilayani Biharamulo wamehaidiwa kujengewa shule mpya baada ya kuwasilisha kilio chao kwa Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa aliposimama kuwasalimia katika eneo la Nyakahura mzani akielekea Wilayani Ngara  ambapo shule iliyopo sasa imezidiwa uwezo na kupelekea watoto kusoma kwa shida. Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa ataendelea na ziara yake Mkoani kagera Wilayani Ngara Septemba 19, 2021.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa