• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Tayari Tumepata na Kutekeleza Miradi ya Zaidi ya Shilingi Bilioni 151 Tunayo Haki ya Kumpongeza Rais Magufuli Kagera Tusonge Mbele – RC Gaguti

Imewekwa : October 30th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti akimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika siku yake ya kuzaliwa tarehe 29 Septemba, 2019 aliwaomba wananchi Mkoani Kagera kuendelea kumwombea afya njema Mhe. John Pombe Magufuli ili aendelee kuchapa kazi na kuufanya Mkoa wa Kagera uendelee kupiga hatua kubwa kimaendeleo.

Mkuu wa Mkoa Gaguti alitoa rai hiyo Septemba 29, 2019 katika viwanja vya Nyamkazi Manispaa ya Bukoba akiongea na wananchi wa eneo hilo ambao ni wavuvi wakiwakilisha wananchi wa mkoa wa Kagera ambapo alieleza namna Rais Magufuli alivyotekeleza miradi ya maendeleo katika mkoa huo na kustahili pongezi ikiwa ni pamoja nakuendelea kumwombea  sala ili aendelee kutekeleza maendeleo kwa wnanchi wa Kagera

“Sisi Wanakagera tunayo sababu ya kumpongeza Rais Magufuli katika siku yake ya kuzaliwa leo tarehe 29/10/2019 kwani Serikali yake ya Awamu ya Tano  imetekeleza miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Kagera yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 151 tangu aingie madarakani mwaka 2015.” Alieleza Mkuu wa Mkoa Gaguti

Mhe. Gaguti alifafanua kuwa miradi iliyopokea fedha na kutekelezwa ni pamoja na shilingi bilioni 4.5 ujenzi wa Hospitali za Wilaya tatu, bilioni 5.9 ujenzi wa vituo vipya 14 vya afya, bilioni 22 ujenzi wa chuo cha Ufundi stadi VETA Kagera, bilioni 3.2 ukarabati wa shule kongwe, bilioni 92.6 ujenzi wa meli mpya, bilioni 22.8 ukarabati wa meli ya MV Victoria uliofikia asilimia 53. Aidha, huduma ya upatikanaji wa dawa muhimu umeimarika nchini  hadi asilimia 97% kutoka shilingi milioni 800 mwaka 2015 hadi kufikia shilingi bilioni 5.4 mwaka huu 2019.

Pia Mkuu wa Mkoa Gaguti aliwahimiza wananchi wa Nyamkazi ambao shughuli zao ni uvuvi kujitafakari wao weyewe katika kazi zao na kuona namna bora ya kujiunga katika vikundi na kuanza kutafuta masoko ya mazao ya samaki katika nchi jirani na mkoa wa Kagera na kuacha ndoto za kuwasubiri wawekezaji kutoka nje ya mkoa wakati wao wapo na shughuli zao ndizo hizo za kila siku.

“Nataka kuona viwanda vya samaki hapa Kagera kwani fursa ya kupata mazo ya samaki tunayo lakini pia nataka niione Kagera ikishindana na nchi ya Rwanda kwani ukiangalia ukubwa wa nchi ya Rwanda ni kilometa za mraba 26000 wakati Mkoa wa Kagera unazo kilometa za mraba 25000 pia mkoa wetu unazo fursa nyingi  za kutosha kushindana na nchi ya Rwanda, wavuvi tutoke  tukatafute masoko tuache kujifungia ndani  wenyewe mwisho wa siku tukakuze mitaji yetu.” Alisisitiza Mkuu wa Mkoa Gaguti

Vilevile Mkuu wa Mkoa Gaguti aliwataka wananchi hao kuendelea kuwa wazalendo kwa kuzilinda raslimali za nchi kwa kutoshiriki uvuvi haramu pia kutoa taarifa kwa mamlaka husika pale wananchi hao wanapoona au kupata taarifa za mtu yeyyote anayeshiriki  kwenye vitendo viovu  vya uvuvi haramu hasa katika Ziwa Victoria.

Mwisho  Mhe. Gaguti aliupongeza uongozi wa Kituo cha Ulinzi na Usimamizi wa Raslimali za Uvuvi Mkoa wa Kagera kwa kuendelea kutekeleza majukumu yake ipasavyo kwa kuhakikisha uvuvi haramu haufanyiki katika Ziwa Victoria aidha, kufanikiwa kunasa zana haramu ambazo ni nyavu za kuvulia samaki zisizoruhusiwa au kukidhi viwango zenye thamani ya shilingi 1,821,200,000 ambapo aliongoza zoezi la kuzichoma moto zana hizo haramu.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa