• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Tunataka Msimu Huu wa Kahawa Mkulima Kwanza Apate Fedha Zake Tutahakikisha Kero Zote za Msimu Uliopita Zinatatuliwa – RC Kagera

Imewekwa : May 23rd, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti akitembelea Chama Kikuu cha Ushirika cha Karagwe Development Co operative Union Limited (KDCU LTD) akikagua na kujionea maandalizi ya ukusanyaji na ununuzi wa Kahawa kwa msimu mpya wa mwaka 2019/20 ili kutatua kero zilizojitokeza katika msimu uliopita wa 2018/19 zisijitokeze msimu huu.

Akiwa Wilayani Karagwe Mei 23, 2019 Mkuu wa Mkoa Gaguti alikutana na Bodi na uongozi wa  Chama Kikuu cha Ushirika KDCU LTD na kufanya nao mazungumzo pia kupata taarifa ni jinsi gani chama hicho kimejiandaa kukuksanya na kununua kahawa kutoka kwa wakulima katika wilaya za Karagwe na Kyerwa.

Mara baada ya kufanaya mazungumzo na Uongozi na Bodi ya KDCU LTD Mkuu wa Mkoa Gaguti aliwaagiza wajumbe wa bodi kuhakikisha wanaondoa kero zilizojitokeza msimu uliopita 2018/19 ikiwa ni pamoja na ucheleweshwaji wa fedha kuwafikia  wakulima katika Vyama vya Msingi au fedha hizo kutumika kabla ya wakati akimaanisha fedha za wakulima kuingizwa katika matumizi ya Chama Kikuu cha Ushirika kabla mkulima hajalipwa.

Pili, Mkuu wa Mkoa Gaguti aliwaagiza KDCU LTD kuhakikisha wanakuwa na mpango mkakati ulio thabiti wa kupata fedha mapema kabla ya kukusanya kahawa ya waulima katika vyma vya msingi  ili kuondoa kero za ucheleweshaji wa fedha na kupelekea wakulima kuuza kahawa yao kwa njia ya magendo ili kupata fedha ya kujikimu.

Tatu, Mkuu wa Mkoa Gaguti aliwataka KDCU LTD kuhakikisha wanatoa ushirikiano thabiti kwa Serikali ili kudhibiti magendo ya kahawa kwa kuondoa kero zote za mwaka jana zilizopelekea wakulima baadhi yao kuuza kahawa kimagendo kwa kuweka mfumo thabiti wa kupata fedha na fedha hizo kumfikia mkulima kwa wakati mara baada ya kukusanya kahawa yake katika chama cha msingi.

Katika hatua nyingne Mkuu wa Mkoa Gaguti alitembelea shamba bora la mkulima wa Kahawa Katika Kijiji cha Katembe Kitongoji Kibugu Kata Kituntu ambapo aliwataka wakulima wa Kahawa kuhakikisha wanazalisha kahawa bora kwa kuvuna kahawa iliyokomaa na kuanika kwa kuzingatia ubora ili kahawa hizo zipate bei nzuri kwenye soko la dunia

Aidha, Mkuu wa Mkoa Gaguti aliwaagiza viongozi wa Vyama vya Msingi kuacha tabia ya kutumia fedha za wakulima katika matumizi ya vyama vyao kabla ya fedha hizo kumfikia mkulima. Pia aliwataka wakulima kufungau akaunti katika taasisi za kifedha kama benki ili malipo ya fedha zao yafanyike moja kwa moja katika akaunti zao na kuondoa migogoro ya fedha kupita katika mikono mingi kabla ya kuwafikia.

Mwisho Mkuu wa Mkoa Gaguti alitoa rai kwa wananchi ambao ni wakulima wa kahawa kutoa ushirikiano kwa Serikali katika kupambana na biashara ya magendo ya kahawa kwa kutoa taarifa katika Serikali. Pili aliwataka Makarani katika vyama vya msingi kuhakikiaha wanapima kahawa ya wakulima kwa usahihi ikiwa ni pamoja na pointi kuziandika katika kilo za mkulima ili kuondoa malalamiko ya wakulima kuibiwa kahawa yao katika mizani.

“Sisi tayari tumejipanga vyema Serikalini kudhibiti magendo ya kahawa na tuhakikisha kila kahawa itakayokamatwa inataifishwa na fedha itakayokuwa inapatikana asilimia 30% tutaitoa kama zawadi ya mtoa taarifa, pili asilimia 50% tutaitoa kwa vijana watakokuwa wanashiriki katika ukamataji wa kahawa ya magendo.” Alisisitiza Mkuu wa Mkoa Gaguti.

Naye Mrajisi msaidizi wa Vyama vya Ushirika Mkoani Kagera Bw. Robert Kitambo alisema kuwa katika msimu huu wa mwaka 2019/20 vyama vikuu vya Ushirika Mkoani Kagera vinatarajia kukusanya kahawa kilo milioni 50 hadi 52 ikiwa KDCU LTD watakusanya kilo milioni 35 na KCU 1990 LTD watakusanya kilo milioni 12.6 na vyama vingine kukusanya kilo milioni 4.4 ambapo katika msimu uliopita wa mwaka 2018/19 zilikusanywa kilo milioni 58.9 za kahawa kwa mkoa mzima wa Kagera.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa