• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Tutaendelea Kuimarisha Ulinzi wa Mipaka ya Nchi Yetu Mkoa Sasa Tunachukua Hatua za Kuanza Kuchonga Barabara ya Kiusalama Kwetu– RC Gaguti

Imewekwa : February 28th, 2019

Mkoa wa Kagera waendelea kuweka mikakati madhubuti ya kuimarisha mipaka yake na nchi jirani hasa kulinda ili kukuza uchumi wa mkoa na Taifa kwa ujumla  lakini pia kuhakikisha wahamiaji haramu hawaingii wala kuingiza mifugo yao nchini bila kufuata taratibu kanuni na sheria za nchi.

Ni baada ya Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti Mkuu wa Mkoa wa Kagera kutembelea na kukagua mipaka ya Tanzania na Uganda kuanzia Kakunyu hadi Mtukula Wilayani Missenyi ili kujionea changamoto mbalimbali  katika mpaka huo ili hatua ziendelee kuchukuliwa kuimarisha mpaka huo.

Akitembele na kukagua mpaka huo Februari 27, 2019 Mkuu wa Mkoa Gaguti na msafara wake walilazimika kuingia nchini Uganda na kurudi chini katika baadhi ya maeneo ili kuyafikia mawe ya mpaka yanayotenganisha  nchi mbili za Tanzania na Uganda kutokana na upande wa Tanzania kutokuwa na barabara ya usalama ya mpaka ambayo inatakiwa  kutoka Mtukula Wilayani Missenyi hadi Murongo Wilayani Kyerwa.

Mkuu wa Mkoa Gaguti baada ya kutembelea na kukagua mawe ya mpaka namba 27 (Kakunyu), 28 (Kalola) na jiwe namba 29 Bugango alisema kuwa pamoja na kuwa Serikali ina mpango wa kutenga fedha za kujenga barabara ya usalama kwa upande wa Tanzania kutoka Mtukula hadi Kakunyu lakini mkoa kwa kuona changamoto ya mpaka huo utaanza kuchonga barabara kidogokidogo ili kupunguza kero ya kuingia nchi jirani wakati doria na ukaguzi wa mpaka ukiendelea.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa Gaguti alifanya mikutano ya hadahara na wananchi katika Vijiji vya Bugango, na Rwengiri Kata Kakunyu na kuwaeleza umuhimu wa kuwa wazalendo kulinda mipaka ya nchi yao na kutoa taarifa pale wanapogundua kuwa kuna wahamiaji haramu au watu kutoka nje ya nchi wameingia bila kufuata utaratibu na sheria za nchi.

Mkuu wa Mkoa aliwasisitiza wananchi kuhakikisha wanautumia vizuri mfumo wa nyumba kumi za kiusalama kuhakikisha wanawabaini wahamiaji haramu na kutoa taarifa kwa uongozi wa Serikali ili hatua za kisheria zichukuliwe kwa wahusika pia kutowaficha wahamiaji haramu katika nyumba zao jambo ambalo linaweza kuhatarisha usalama wa nchi.

“Nyinyi wananchi nawombezi sana kuwa wazalendo wa kwanza kwa kulinda mipaka ya nchi yenu, ulinzi wa mipaka ya nchi hautegemei Vyombo vya Ulinzi na Usalama peke yake  bali na wananchi tunatakiwa kuwa wazalendo wa hali ya juu kwa kutoisaliti  nchi yetu. Pia kama hatutotoa taarifa ya wahamiaji haramu ni kosa la jinai kufanya hivyo.” Aliwasisitiza wananchi Mkuu wa Mkoa Gaguti

Mwisho alivipongeza Vyombo vya Ulinzi na Usalama Wilayani Missenyi kwa kuendelea kuilinda mipaka ya nchi vizuri na kuendelea kuondoa wahamiaji haramu wanaoingia nchini bila kufuata sheria za nchi lakini pia na kuondoa mifungo inayoingizwa wilayani humo kinyemera ili kupatiwa marisho kutoka nchi jirani.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa