• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Uongozi wa Mkoa wa Kagera Waweka Mikakati ya Kuthibiti Utoroshwaji wa Madini ya Bati Wilayani Kyerwa Kuuzwa Nchi Jirani

Imewekwa : February 4th, 2019

Mkoa wa Kagera waanza kuchukua hatua za dhati za usimamizi wa rasilimali madini zinazopatikana mkoani humo kwa kuweka mfumo thabiti wa kuhakikisha kila mdau aliyeko kwenye mnyororo wa thamani ya  madini na kuwajibika ipasavyo ili madini hayo  yawanufaishe wananchi na kuinua pato la mkoa na taifa kwa ujumla.

Hatua zinazoendelea kuchukuliwa ni pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti kufanya ziara katika machimbo ya madini ya bati Nyaluzumbura Wilayani Kyerwa na kuzungumza na Wachimabaji Wadogo juu ya changamoto mbalimbali wanazokutana nazo katika uchimbaji na kufanya biashara ya madini.

Mkuu wa Mkoa Gaguti akieleza lengo la kutembelea machimbo hayo Februari 3, 2019  alisema kuwa baada ya kufanya kikao cha wadau wa madini cha Taifa chini ya Rais John Pombe Magufu Januari 22, 2019 Jijini Dar es Salaam iliazimiwa kuwa kila mkoa uhakikishe unasimamia kikamilifu rasilimali  madini na kuondoa kero na vikwazo  vyote vinavyopelekea madini kuuzwa kimagendo na nchi kukosa mapato.

Mkuu wa Mkoa Gaguti alitoa nafasi kwa Wachimbaji  Wadogo wa Mdini ya Bati kumweleza changamoto mbalimbali  wanazokumbana nazo katika uchimbaji na biashara ya madini ya Bati. Wachimbaji hao wadogo walimweleza Mkuu wa Mkoa kuwa changamoto kubwa ni bei ya madini ya bati  kuwa ndogo, Utoroshaji wa madini hayo na kuuuzwa nchi jirani, Mitaji midogo ya kununulia vifaa vya kisasa vya uchimbaji.

Mara baada ya kusikiliza changamoto hizo Mkuu wa Mkoa aliyeongozana na Kamati ya Ulinzi na Usalaama ya Mkoa aliwaeleza Wachimabji Wadogo kuwa changamoto hizo tayari mkoa umezitafutia ufumbuzi ambao kama wao watatoa ushirikiano zitaisha kwa muda mfupi na wataanza kuneemeka na uchimbaji wa madini hayo lakini pia mkoa utakuza pato lake aidha na taifa kwa ujumla.

“Tofauti na ilivyo sasa sisi Serikali ya Mkoa tumeamua kuanzisha mfumo sahihi katika sekta ya madini, tumeamua kuweka mfumo wenye utaratibu mzuri wa uchimbaji, pili mfumo wa kuyatunza madini ghafi ya bati baada ya kuchimbwa kabla ya kuuzwa, na mwisho ni mfumo sahihi wa kuuza mdini hayo na soko lake yakiwa yameongezewa thamani ndani ya Wilaya ya Kyerwa.” Alifafanua Mkuu wa Mkoa Gaguti.

Ili kuhakikisha Madini ya Bati hayatoroshwi na kuuzwa nchi jirani tayari Serikali imewapata wawekezaji wa kuongeza thamani madini ya bati ambapo tayari mmoja amejenga kiwanda cha kuongeza thamani madini hayo naye ni TANZAPLUS na kiwanda chake kipo Wilayani Kyerwa. Wa pili ni Africa Top Minerals Limited (ATM) ambaye anaendelea na mazungumzo na Serikali ili kuanza kuongeza thamani Madini ya Bati.

MAAGIZO

Mkuu wa Mkoa Gaguti alimwagiza Afisa Madini wa Mkoa wa Kagera  Mhandisi Lucas Mlekwa kuhakikisha anaanza utekelezaji wa kuanzisha maghara ya kuhifadhi madini ghafi mara baada ya kuchimbwa, pili kuwasimamia wachimbaji wadogo kujiunga katika vikundi ili watambuliwe na kupatiwa mikopo. Tatu ni kuhakikisha madini yote yatakayochimbwa Kyerwa yaongozewe thamani Wilayani hapo na soko lake liwe humo.

Maagizo hayo yanatakiwa kuwa yametekelezwa ifikapo mwishoni mwa mwezi Februari 2019 ili Waziri wa Madini aweze  kualikwa mwanzoni mwa Mwezi Machi 2019 kuzindua mfumo rasmi wa uchimbaji, uongezaji thamani na uuzaji wa Madini ya Bati Mkoani Kagera ambao utakuwa unawanufaisha wadau wote waliopo kwenye mnyororo wa thamani ya madini hayo.

Madini ya Bati Nyaluzumbura Wilayani Kyerwa yalianza kuchimbwa tangu mwaka 1924 na katika machimbo hayo kwa sasa yanachimbwa Madini ya Bati kwa wastani wa nusu tani (Kilo 500) kila mwezi na idadi ya Wachimbaji Wadogo katika mgodi huo ni 1,350.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa