• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Usichukulie Poa Nyumba ni Choo Kuzinduliwa Kanda ya Ziwa Mkoani Kagera Kupambwa na Mrisho Mpoto Pamoja na Fainali za JPM Bodaboda Cup 2019

Imewekwa : May 24th, 2019

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kuzindua Kampeini ya Kitaifa ya Usafi wa Mazingira yenye kauli mbiu isemayo  “Usichukulie Poa, Nyumba ni Choo” katika mkoa wa Kagera Mei 25, 2019.

Akitoa ufafanuzi wa Kampeini ya “Usichukulie Poa, Nyumba ni Choo” Mkuu wa Mkoa Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti katika mkutano na vyombo vya habari alisema kuwa anaishukuru Serikali kuamua kufanya uzinduzi wa kampeini hiyo kwa  Kanda ya Ziwa katika Mkoa wa Kagera ili kuhamasisha wananchi kujenga vyoo bora katika ngazi ya kaya na taasisi.

Kabla ya Kampeini ya Usichukulie Poa, Nyumba ni Choo’ kuanza nchini mwaka 2012 katika mkoa wa Kagera asilimia 35 ya kaya hazikuwa na vyoo kabisa ambapo vyoo bora ilikuwa ni asilimia 20% tu. Lakini kutokana na juhudi za mkoa hasa kupitia idara ya Afya kuhamasisha wananchi  na kufanya ukaguzi wa kaya kwa kaya hadi sasa kaya zisizokuwa na vyoo zimepungua kutoka asilimia 35% hadi asilimia 5% tu.

Aidha, vyoo bora katika kaya mkoani Kagera vimeongezeka kutoka asilimia 20% hadi asilimia 55% na lengo ni kuhakikisha ifikapo Juni 2021 angalau asilimia 80% ya vyoo bora iwe imefikiwa katika . Vilevile Mkuu wa Mkoa Gaguti alisema kuwa mkoa umejipanga katika kipindi cha miezi mitatu kufikia Agosti 2019 kila kaya lazima iwe na choo na kukitumia ili kuondoa asilimia 5% ya kaya ambazo hazina vyoo kabisa kwa sasa.

Pia kwa kunesha mfano Mkuu wa Mkoa Gaguti alisema kuwa uhamasishaji wa vyoo bora unajikita kwa wananchi tu lakini taasisi mbalimbali za Serikali na zisizokuwa za Serikali zinasaulika na kwa kulitambua hilo ndiyo maana yeye Mkuu wa Mkoa akishirikiana na wadau mbalimbali aliamua kujenga choo bora katika uwanja wa Kaitaba kuzikumbusha taasisi mbalimbali kuwa nazo zinatakiwa kuwa na vyoo bora katika maeneo yao.

Vilevile Mkuu wa Mkoa Gaguti  alikemea tabia ya kujisaidia ovyo ijulikanayo kama "kuchimba dawa" kwa wasafiri na madereva wa vyombo vya moto katika barabara kuu za Bukoba hadi nyakanazi na Bukoba hadi Mtukula kuwa kwa sasa hakuna haja ya kusingizia kuwa hakuna vyoo na kujisaidia hovyo na kuchafua mazingira wakati kuna maeneo yenye huduma za vyoo bora vya kujisaidia.

“Naagiza Wakuu wote wa Wilaya katika Mkoa wa Kagera kuhakikisha wanasimamia uchafuzi huu wa mazingira ili kuzuia kuenea kwa magonjwa ya kuambukiza kama kuhara na kuhara damu, kipindupindu na minyooo.” Aliagiza Mkuu wa Mkoa Gaguti.

Naye Bw. Anyikite Mwakitalima mwakilishi wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika mkutano huo wa Mkuu wa Mkoa na Waandishi wa Habari alisema kuwa wakati kampeini ya “Usichukulie Poa, Nyumba ni Choo” inaanza mwaka 2012 kitaifa kaya ambazo hazikuwa na vyoo bora zilikuwa milioni 1.4 lakini hadi kufikia sasa kutokana na kampeini hiyo takwimu hizoo zimeshuka hadi kufikia kaya elfu 70,000 tu nchini.

Naye Msanii Maarufu wa kughani mashairi Mrisho Mpoto maarufu kama Mjomba alisema kuwa katika mkoa wa Kagera mkoa wenye watu wanaojipenda, mkoa wenye wasomi wa kutosha haamini kuwa asilimia 5% ya kaya hazina vyoo na kusisitiza kuwa pengine hizo ni takwimu za miaka mingi iliyopita. Mrisho Mpoto alisema kuwa labda angependa kuona mwenyewe kama ni kweli wakati akifanya uhamasishaji katika Wilaya zote za mkoa wa Kagera kwenye kampeini ya “Usichukulie Poa, Nyumba ni Choo”.

Kampeini ya “Usichukulie Poa, Nyumba ni Choo” itazinduliwa rasmi Mei 25, 2019 katika uwanja wa Kaitaba Manispaa ya Bukoba ambapo uzinduzi huo utapambwa na Fainali ya mechi ya mpira wa miguu ya kombe la John Pombe Magufuli (JPM BODABODA CUP 2019) ambapo ligi hiyo iliyoanzishwa Machi 30, 2019 na kufadhiliwa na Mkuu wa Mkoa Gaguti na kuwahusisha vijana waendesha Bodaboda katika Manispaa ya Bukoba ili kuwaleta pamoja na kuwapa elimu juu ya ujasiliamali.

Katika Fainali hizo mshindi wa kwanza atanyakua zawadi ya shilingi milioni tatu pia na zawadi nyingine nyingi zitatolewa  kwa washiriki wananchi wa mkoa wa Kagera hasa Manispaa ya Bukoba wanakaribishwa kushiriki katika uzinduzi huo utakaopambwa pia Msanii Maarufu Mrisho Mpoto (Mjomba).

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa