• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Uzinduzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Maziwa Kitaifa Mkoani Kagera Kyakailabwa Manispaa ya Bukoba

Imewekwa : May 30th, 2017

Maadhimisho ya Wiki ya Maziwa Kitaifa Mkoani Kagera Yazinduliwa Rasmi na Naibu Waziri Ole Nasha Kyakailabwa Manispaa ya Bukoba

Maadhimisho ya Wiki ya Maziwa Kitaifa Mkoani Kagera yazinduliwa rasmi Mei 28, 2017 na Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi  Mhe. Tate William Ole Nasha katika Viwanja  vya Kyakailabwa Manispaa ya Bukoba na kuzinduzia rasmi uhamasishaji wa unywaji wa Maziwa kwa wananchi wote ili kupunguza udumavu na kuongeza viinilishe muhimu mwilini. Kaulimbiu ikiwa ni “Kunywa Maziwa, Furahia Maisha”

Katika uzinduzi huo Naibu Waziri Ole Nasha alisema kuwa kwa sasa Serikali imeamua kuja na mkakati wa wa uhamasishaji wa wananchi wote kunywa maziwa nchini  kwani maziwa yana viinilishe ambavyo hupunguza udamavu kwa watoto pia viinilishe hivyo havipatikani katika vyakula vingine ispokuwa maziwa tu ambavyo pamoja na kupunguza udumavu lakini huongeza uwezo akili kufanyakazi.

“Unywaji wa maziwa umekuwa ukisistizwa kwa watoto tu na si kwa watu wazima lakin imegundulika kuwa kila mtu anatakiwa kunywa maziwa kwa wastani angalau wa kitaifa lita 47 kwa mwaka ili kuongeza viinilishe na kupunguza udumavu kwa watoto wadogo hasa kwa Mkoa wa Kagera ambapo una udumavu wa watoto ni asilimia 52.” Alisistiza Naibu Waziri Ole Nasha .

Tanzania inazalisha maziwa takribani lita bilioni 2.1 kwa mwaka ambapo maziwa mengi asilimia 70 huzalishwa na ng’ombe wa asili ambao uzalishaji wao ni kati ya lita 1 hadi 3 kwa siku. Lakini kuna ng’ombe wachache wa maziwa wanaokadiririwa kuwa 782,000 ambao huzalisha kati ya lita 8 hadi 20 kwa siku.

Aidha, maziwa  yanayoingia viwandani kusindikwa kati ya maziwa yanayozalishwa nchini ni asilimia 3 tu ambapo hapa nchin tunavyo viwanda 75 vya kusindika maziwa  vyenye uwezo wa kusindika lita 640,000 kwa siku, lakini kwa sasa ni viwanda 65 tu vinavyofanya kazi na vinasindika lita 167,070 kwa siku ambayo ni sawa na asilimia 26 ya uwezo  wote uliopo.

Katika Mkoa wa Kagera mtu mmoja anakunywa wastani wa lita 16 kwa mwaka chini ya kiwango cha Kitaifa ambapo mtu mmoja anakunywa lita 47 chini ya kiwango cha Kimaitaifa ambapo mtu mmoja anatakiwa kunywa wastani wa lita 200 kwa mwaka. Kiwango cha wastani wa lita 200 kwa mwaka kilipendekezwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) na Shirika la Chakula na Kilimo (FAO).

Mkoa wa Kagera unazalisha maziwa takribani lita 46,858,481 za maziwa kwa mwaka. Uzalishaji huo unatokana na  ng’ombe 550,070 ambao kati yao  ng’ombe 21, 438 ni wa maziwa. Wanakagera wanatakiwa kuyatumia maadhimisho haya kujifunza mbinu za ufugaji bora na namna ya kusindika maziwa na bidhaa zake.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenelari Mstaafu Salum M. Kijuu alitembelea maadhimisho hayo na kukagua mabanda mbalimbali ya wadau ambao ni wafugaji, wenye viwanda na wasindikaji wa bidhaa mbalimbali zinazotokana na maziwa. Akiwa katika maadhimisho hayo Mhe. Kijuu alitoa msistizo juu ya Elimu kuhusu unywaji wa maziwa kwa wananchi wa Mkoa wa Kagera ambao wanahitaji sana elimu hiyo.

Katika Banda la Bodi ya Maziwa Tanzania Mkuu wa Mkoa aliutaka uongozi wa Bodi ya Maziwa Tanzania kuhakikisha unatoa elimu ya kutosha juu ya usindikaji na unywaji wa maziwa kwani wananchi walio wengi hawana uelewa kuhusu unywaji wa maziwa na elimu hiyo haitolewi mara kwa mara kuonesha umuhimu wa wananchi kunywa maziwa na faida zake.

Ili kuhakikisha Maadhimisho ya Wiki ya Maziwa inafanikisha lengo lake kwa wananchi kunywa maziwa  na kufuhia maisha Mhe. Naibu Waziri Ole Nasha wakati wa uzinduzi alizindua unywaji wa Maziwa kwa wananchi ambao ni watu wazima na watoto pia.

Aidha Mkuu wa Mkoa Mhe. Kijuu naye tarehe 29.05.2017 alitoa maziwa kwa Makundi maalum ambayo ni Kituo cha makao ya Wazee Kiilima na shule ya Msingi Mugeza Mseto ambapo wazee wa Kiilima na wanafunzi  hao waligawiwa maziwa na kunywa kama uhamasishaji wa unywaji wa maziwa .

Kaimu Msajili wa Bodi ya Maziwa Tanzania Bw. Nelson Kilongozi alisema katika maadhimisho hayo kuwa uongozi wa Bodi ya Maziwa uliamua kuleta maadhimisho ya Wiki ya Maziwa Mkoani Kagera Ili kuhamasisha na kutoa elimu kwa wananchi wa Mkoa wa Kagera juu ya umuhimu wa kunywa maziwa, kusindika maziwa na bidhaa zake pia kutoa elimu kwa wadau kuwekeza katika sekta ya maziwa ikiwa ni pamoja na ufugaji bora wa ng’ombe wa  maziwa ambao wanao uwezo wa kuzalisha maziwa kwa wingi.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa