• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Uzinduzi wa Mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III) Mkoani Kagera

Imewekwa : July 13th, 2017

Vijiji 321 Mkoani Kagera Kunufaika na Nishati ya Umeme Baada ya Mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III)  Kuzinduliwa Rasmi na Utagharimu Bilioni 45.43

Wananachi Mkoani Kagera wapata neema ya nishati ya umeme baada ya Serikali kuzindua  Mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu  (REA III) utakaogharimu jumla ya  shilingi bilioni 45.43 na kuvinufaisha vijiji 321 ambavyo havikupata nishati ya umeme kwenye awamu ya kwanza na  ya pili.

Akizindua Mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III) Kijijini Rwabigaga Kata Kamuli Wilayani Kyerwa Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani alisema mradi huo wa Umeme vijijini Awamu ya Tatu  umelenga kuvifikia vijiji na vitongoji vyote na kila mwananchi ambaye hakupata umeme kwa awamu zilizopita.

“Mradi utavilenga vijiji vyote ambavyo havikufikiwa kabisa katika awamu ya kwanza na ya pili. Pili, mradi utavifikia vitongoji vyote ambavyo viliachwa kwenye vijiji katika awamu ya kwanza na ya pili. Tatu, mradi huo umelenga kufukisha umeme kwenye maeneo ambayo hayafikiki kirahisi kama visiwani ambapo Kagera visiwa 176 vitafikishiwa umeme wa jua.” Alisistiza Dkt Kalemani

Mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III) Mkoani Kagera  utatekelezwa kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza jumla ya vijiji 141 vitafikishiwa umeme na kazi hiyo inaanza kuanzia sasa mpaka mwezi Machi 2019. Awamu ya pili itafuata mara baada ya awamu ya kwanza kukamilika na vijiji 180 katika awamu ya pili vitafikishiwa umeme na awamu hiyo itakamilika mwaka 2021.

Naibu Waziri Dkt. Kalemani alisema kuwa katika awamu ya tatu kila mwananchi atafikishiwa umeme katika nyumba yake bila kubagua aina ya nyumba hata iwe ya tembe  kwani lengo la Serikali ni kuhakikisha kila mwananchi ananufaika na umeme. 

Baada ya uzinduzi huo Naibu Waziri Dkt. Kalemani alimkabidhi Mkandarasi  ambaye ni NAKUROI CONSTRUCTIONS  COMPANY  LIMITED atakayetekeleza Mradi huo Mkoani Kagera  na kumwagiza ahakikishe anawaajili  Wakandarasi wadogo wadogo kutoka katika maeneo husika ili kupunguza gharama na kutoa ajira kwa wazawa wa maeneo husika.

Pili, aliwaagiza Shirika la TANESCO kuhakikisha wanafungua madawati katika Tarafa na kata kwa maeneo ambayo ofisi zao zipo mbali ili kuwaondolea wananchi usumbufu wa kulipia gharama za kuwekewa umeme. Aidha, aliagiza viongozi wote wa Serikali kushirikiana na Mkandarasi kuhakikisha Tasisi zote za Serikali zinafikiwa na umeme huo katika vijiji vitakavyotekelezewa mradi.

Kitaifa Mradi wa Umeme Vijijni Awamu ya Tatu (REA III) unatarajia  kutekelezwa kwenye vijiji 7,873 na tayari umezinduliwa katika Mikoa ya Simiyu na Kagera pia utazinduliwa katika Mkoa wa Geita. Aidha, kwa upande wa mkoa Mkuu wa Mkoa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu kwaniaba ya wananchi alimshukuru Naibu Waziri Dkt. Kalemani kwa kuzindua mradi huo na alihaidi kumsimamia kikamilifu Mkandarasi ili utekelezwe na kukamilika kwa wakati.

Baada ya uzinduzi huo uliofanyika Julai 11, 2017 Mkoani Kagera wananchi waliaswa kutumia fursa hiyo ya kupata umeme kwa kujiajili kwa kuanzisha viwanda vidogo vidogo na kujipatia ajira ili wajiingizie kipato.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa