• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Mche wa Zao la Vanilla

Imewekwa : May 2nd, 2017

Wakulima Wanuia Kulifanya Zao la Vanilla Kuwa Mbadala wa Kahawa na Chai na Kuinua Tena Uchumi wa Mkoa wa Kagera

Wananchi wa Mkoa wa Kagera wanuia kulifanya zao la Vanilla kuwa zao mbadala wa mazao ya biashara mkoani hapa ambapo mazao hayo ambayo ni Kahawa na Chai yalikuwa mazao makuu ya kibiasahara yaliyochangia katika kukuza uchumi wa Mkoa wa Kagera.

Zao la Vanilla huenda likawa zao mkombozi kwa wananchi wa mkoa huu baada ya kupata soko na kuwa na bei nzuri hasa katika soko la dunia jambo linalohamasisha kilimo chake ambapo kwa sasa vanilla mbichi inauzwa Shilingi 70,000/= hadi 100,000/= kwa kilo moja .

Mara baada ya Kuonekana kuwa zao la Vanilla linaweza kuwa mkombozi wa uchumi wa Mkoa wa Kagera uongozi wa mkoa uliamua kuitisha kikao cha wakulima na wadau wa Vanilla ili kuweka mikakati thabiti  wa jinsi ya kulifanya zao hilo kuwanufaisha wakulima na kukuza uchumi wa Mkoa wa Kagera.

Akifungua kikao hicho Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Deodatus Kinawilo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa  wa Kagera alisema kutokana na zao la Kahawa na Chai kuanguka bei na kusababisha kuyumba kwa  uchaumi wa wananchi sasa zao la vanilla linaweza kuwa mkombozi na kuuinua mkoa wa Kagera kiuchumi tena.

Katika kikao hicho kilichoratibiwa na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji Bw. Adam Swai alisema dhumuni kubwa ilikuwa ni kuwaleta pamoja wakulima, wanunuzi na wadau wote wa zao la vanilla ili kuweka mikakati ya pamoja kuhakikisha zao hilo linakuwa na mfumo rasmi hasa katika kautafuta masoko na jinsi ya kuwaendeleza wakulima ili wanufaike.

Wakulima na wadau wa vanilla walikubaliana kuwa sasa zao la vanilla lipewe kipaumble katika mkoa wa Kagera kama zao kuu la biashara. Pili, yaruhusiwe tu makampuni yaliyosajiliwa na kupata reseni za biashara za kununua vanilla. Tatu, bei ya vanilla itangazwe kwa maoteo mapema kulingana na maoteo ya soko la dunia na kama bei ya soko la duni ikiwa ubwa kuliko iliyotangazwa na makampuni hayo awali wakulima walipwe malipo ya pili.

Wanunuzi halali wa vanilla yaani Makampuni yalenge kumuendeleza mkulima na siyo kupatikana wakati tu wa ununuzi wa vanilla  ili kuhakikisha wakulima hao wananufaika na kilimo chao kuliko kuwaacha wanahaingaika na kupelekea kuuza vanilla zao kwa bei ndogo kwa kurubuniwa na wajanja wachache.

Aidha, Serikali iwadhibiti wanunuzi kutoka nchi jirani ambao wanawarubuni wakulima na kununua vanilla zao kwa bei ndogo na kukwepa kulipa ushuru na kodi na kupelekea kuikosesha Serikali mapato yake. Serikali ilitakiwa na wadau wa zao la vanilla kudhibiti magendo ya vanilla ili zao hilo lisije kuwa kama mazao ya kahawa yanayotoreshewa nchi jirani.

Katika hatua nyingine mwanzilishi wa kilimo cha vanilla na Meneja Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Wakulima(MAYAWA)  katika Mkoa wa Kagera Bw. Charles Kamando alisema zao la vanilla lilianza kulimwa mkoani Kagera kuanzia mwaka 1997 baada ya zao hilo kuletwa na vijana wawili kutoka Nchini Uganda waliokuwa wanafanya kazi katika shamba la Mzungu.

“Kilimo cha zao la Vanilla kilianza mwaka 1932 nchini Uganda lakini mwaka 1997 vijana wawili wa Kitanzania waliiba marando na kuja nayo Mkoani Kagera na ndipo hapo kilimo cha vanilla kilianza kwa shirika letu na tulianza kuwafundisha wakulima 85 na ndiyo mwanzo wa vanilla kuanza kulimwa Mkoani Kagera na nchini Tanzania.” Alitoa historia Bw. Kamando

Kwa sasa MAYAWA ndilo shilrika halali ambalo linajishughulisha na kuwafunza wakulima Mkoani Kagera kulima vanilla, kununua vanilla zinazozalishwa na wakulima, kuzikausha vanilla hizo kwa viwango vinavyohitajika na kutafuta masoko hasa katika soko la dunia. Kikao hicho kiliketi tarehe 28.04.2017 na vikao kama hivyo vitakuwa vinafanyika mara tatu kwa mwaka kila mwaka.

Zao la vanilla linatumika katika matumizi mbalimabli kama vinywaji, madawa ya binadamu, vyakula na vitafunwa pamoja na manukato mablimbali.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa