• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

Imewekwa : March 14th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Hajjat Fatma Mwassa awakumbusha viongozi wa dini ya Kiislam Manispaa ya Bukoba kuendelea kudumisha amani mshikamano na kuwahimiza wananchi kuendelea na ushirikiano, upendo na amani hususani katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ili mkoa uendelee kupaa kiuchumi.

Mkuu wa Mkoa Fatma Mwassa aliyasema hayo katika semina fupi  ya viongozi wa dini ya Kiislam iliyofanyika  katika  ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera Machi12, 2025  akiwakutanisha Maimamu  wa Misikiti yote ya Manispaa ya Bukoba. wakiongozw na Sheikh Haruna kichwabuta Sheikh wa Mkoa wa Kagera.

"Katika mkoa kukiwa na magomvi, kelele na kutoelewana baina ya viongozi kwa viongozi au viongozi na waumini mkoa hauwezi kutulia na maendeleo yatasuasua, lakini nawashukuru viongozi wa madhehebu ya dini zote mkoani kagera kwa mshikamano na umoja jambo ambalo limepelekea kuleta maendelo chanya kwa wananchi wa Kagera" Alisistiza Mkuu wa Mkoa Mwassa.

Akitaja mafanikio yaliyofikiwa kutokana na utulivu wa mkoa na maombezi ya viongozi wa dini Mkuu wa Mkoa Mwassa alisema Mkoa umefanikiwa kupata fedha za kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo itakayochachua uchumi wa mkoa na wananchi kwa ujumla. Baadhi ya miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa soko Kuu la Bukoba na Stendi kuu ya Bukoba,Ujenzi wa kingo za Mto Kanoni, Upanuzi wa barabara ya njia nne na ujenzi wa Stendindi ya mjini kati.

Miradi mingine ni pamija na ujenzi wa Ofisi mpya ya mkuu wa mkoa, Ujenzi wa Uwanja mpya wa ndege, ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kampasi ya Bukoba, Upanuzi wa Bandari za Bukoba na Kemondo na ujenzi wa Kitega uchumi cha Machinga Manispaa ya Bukoba.

Naye Sheikh Haruna Kichwabuta, Sheikh wa mkoa wa Kagera katika semina hiyo aliwataka viongozi hao kuwa mfano wa kuigwa kwa waamini wao ikiwa ni katika utoaji wa sadaka na zaka hasa katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Aidha, viongozi hao wamemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuleta fedha nyingi za maendeleo katika mkoa wa Kagera na sasa miradi mikubwa inatekelezwa ambayo ilikuwa imekwama kwa kipindi kirefu pia walimshukuru Mkuu wa Mkoa Hajjat Fatma Mwassa kwa uongozi madhubuti na usimamizi wa miradi ya  maendeleo katika mkoa wa Kagera.

Katika semina hiyo Mkuu wa Mkoa Kagera Hajjati Fatma Mwassa alitoa sukari, mafuta ya kupikia, mchele, ngano na tende kwa Maimamu wa Misikiti yote ya Manispaa ya Bukoba ikiwa ni moja ya sadaka yake katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kwa viongozi hao wa dini ya kiislamu ili waendelee kutekeleza majukumu yao vyema.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa