• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Vitambulisho vya Wafanyabiashara Wadogo Awamu ya Pili Mkoani Kagera Vyakabidhiwa Kwa Wakuu wa Wilaya Watendaji Waonywa

Imewekwa : February 1st, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti agawa vitambulisho 35,000 vya awamu ya pili vya Wafanyabiashara Wadogo katika Mkoa wa Kagera na kuwaagiza Watendaji wa Serikali chini ya usimsmizi wa Wakuu wa Wilaya kuendelea na zoezi la ugawaji wa vitambulisho hivyo na kuhakikisha ifikapo Februari 28, 2019 vitambulisho vyote view vimegawiwa kwa Wafanyabiashara Wadogo.

Katika hafla fupi ya kukabidhi vitambulisho hivyo 35,000 vya awamu ya pili kwa Wakuu wa Wilaya iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba Februari 1, 2019 Mkuu wa Mkoa Gaguti alisema kuwa katika tahimini iliyowakutanisha Wakuu wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara Mkoa wa Kagera haukufanya vizuri sana wa vibaya katika ugawaji wa vitambulisho vya awamu ya kwanza 25,000 kwani ulishika nafasi ya sita kwa ugawaji wa asilimia 65%.

Mkuu wa Mkoa Gaguti katika hafla hiyo fupi aliziagiza Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha zinakusanya takwimu za Wafanyabiashara wote Wakubwa, wa Kati na wale Wadogo ifikapo Februari 15, 2019 takwimu hizo ziwe zimewasilishwa ofisini kwake lengo likiwa ni kuhakikisha kila mwananchi anayetoa bidhaa yoyote na kupokea fedha anatambuliwa na kulipa kodi au tozo stahiki za Serikali.

Hafla hiyo fupi iliyowashirikisha Wakuu wa Wilaya saba za Mkoa wa Kagera, Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Wilaya na Manispaa, Wenyeviti wa Halmashauri na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Bukoba, Watendaji wa Kata wa Manispaa ya Bukoba waliowawakilisha Watendaji wenzao katika mkoa ambao walitakiwa kutoa changamoto zinazowakumba katika ugawaji wa vitambulisho vya Wafanyabiashara Wadogo katika maeneno yao.

Wakitoa changamoto mbalimbali  kuhusu ugawaji wa vitambulisho Watendaji wa Kata walisema kuwa changamoto kubwa ni Elimu kwa wananchi kutojua ni mfanyabiashara yupi anatakiwa kupata kitambulisho na ni yupi hastahili kupata na changamoto hiyo inatokana na suala la mauzo ghafi kutoeleweka vizuri kwao wao wenyewe Watendaji  kama wahusuika wa ugawaji lakini pia wafanyabiashara jambo ambalo waliitaka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutoa uelewa kwao.

Changamoto nyingine iliyotajwa na Watendaji wa Kata waliohudhuria hafla fupi ya kukabidhi  vitambulisho kwa Wakuu wa Wilaya  ni suala la Mfanyabiashara Mdogo kuwa na namba ya utambuzi ya mlipa kodi ya TRA (TIN) wakati biashara yake ni ndogo na hastahili kupata kitambulisho cha mfanyabiashara mdogo wakati mtaji wake ni mdogo haufikii kiwango cha shilingi milioni 4,000,000/= kwa mwaka.

Akitoa majibu ya  changamoto zilizowasilishwa na Watendaji wa Kata Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Mkoa wa Kagera Bw. Adam Ntoga alisema kuwa Mfanyabiashara Mdogo anayestahili kupata kitambulisho ni yule ambaye mauzo yake kwa siku hayafikii shilingi 11,000/= kwa siku. Kama Mfanyabiashara anauza bidhaa zake na kupata kiwango cha fedha chini ya shilingi 11,000/= huyo anastahili kupata kitambulisho cha Mfanyabiashara Mdogo.

“Hata kama Mfanyabiashara ana mtaji wa shilingi 5,000/= lakini anauza bidhaa zake kwa siku na kupata shilingi 11,000/= au zaidi kwa siku huyo hastahili kupata kitambulisho, kinachoangaliwa hapa si mtaji wa mfanyabiashara alionao bali ni mauzo yake kila siku kama anapata kiasi cha shilingi 11,000/= au chini ya kiwango hicho.” Alifafanua Bw. Adamu Ntoga

Katika huatua nyingine Mkuu wa Mkoa Gaguti alitoa onyo kwa Wafanyabiashara ambao walidanganya na kupokea vitambulisho wakiwa tayari wametambuliwa na mfumo wa ulipaji kodi wa TRA kuwa tayari anayo amajina sita hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwao mara moja. Pia aliwaonya Watendaji wa Kata ambao wanaandika barua kuwatambulisha wafanyabiashara kuwa mtaji wao ni mdogo kuwa waache mara moja.

“Watendaji wa Kata acheni hizo tabia zenu za kuwaandikia barua wafanyabiashara na kuwatambulisha kuwa biashara zao ni ndogo, kama kuna Mfanyabiashara alipita TRA na kujisajiliwa mwacheni apite huko huko na kufanyiwa tathimini upya na TRA wao ndiyo watoe barua hizo vinginevyo mkiendelea hatua zitachukuliwa kwenu.” Alionya Mkuu wa Mkoa Gaguti.

Aidha, Mkuu wa Mkoa Gaguti alitoa ufafanuzi juu ya Wafanyabiashara Wadogo wanaopata vitambulisho kuendelea kuto tozo ndogo ndogo za Halmashauri husika katika maeneo wanayofanyia biashara mfano tozo za kukusanya taka au huduma za vyoo na usafi na kuwataka kutotumia kigezo cha vitambulisho na kuacha kulipa tozo hizo. Pia Wafanyabiashara ambao tayari wanatakiwa kulipa kodi katika Halmashauri wanatakiwa kuendelea kulipa kodi hizo baada ya kufanyiwa tathimini na TRA.

Mkoa wa Kagera katika awamu ya kwanza ulipatiwa vitambulisho vya Wafanyabiashara Wadogo 25,000 na Wilaya ya Bukoba ilipatiwa jumla ya vitambulisho 3,580. Wilaya za Missenyi, Karagwe, Kyerwa, Ngara, Muleba, na Biharamulo zilipatiwa vitambulisho 3,570 kila moja. Hadi tarehe 1 Februari,2019 vilikuwa vimegawiwa vitambulisho 16,369  sawa na asilimia 65% kwa Wilaya zote na kiasi cha shilingi milioni 327,380,000/= zilikuwa zimekusanywa na kupelekwa benki.

Vitambulisho vya awamu ya pili Mkoa wa Kagera ulipatiwa vitambulisho 35,000 na vitambulisho hivyo vimegawiwa katika Wilaya kulingana na Jiografia ya Wilaya, wingi wa watu na hali ya kiuchumi tofauti na awamu ya kwanza ambapo katika awamu ya pili Wilaya Bukoba iligawiwa vitambulisho 7,000 Biharamulo na Ngara kila moja iligawiwa vitambulisho 4,200. Kyerwa na Missenyi kila moja vitambulisho 4,400 na Wilaya za Karagwe na Muleba ziligawiwa vitambulisho 5,400.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa