• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Wahujumu Uchumi Mkoani Kagera Hawana Nafasi Zaidi ya Tani Kumi za Kahawa Zakamatwa Zikitoroshwa Kwenda Nchi Jirani

Imewekwa : September 1st, 2018

Mkoa wa Kagera waendelea juhdi za kupambana na wahujumu uchumi wanaosafirisha Kahawa kwa njia za magendo kwenda nchi jirani huku wakikwepa kulipa za kodi za Serikali zinazotumika kuleta maendeleo ya wananchi katika Mkoa.

Ni baada ya Jeshi la Polisi Mkoani hapa usiku wa kuamukia Agosti 31, 2018 kukamata Magari mawili aina ya FUSO yenye namba T 182 ARG na T 424 AMY yakiwa yamepakia Kahawa zilizokobolewa zaidi ya tani 10 katika Kijiji cha Katarabuga Kata Bwanjai yakiwa barabara kuu ya kuelekea Katoma hadi Kanyigo Wilayani Missenyi  mpakani mwa Tanzania na Uganda.

Akikagua Kahawa hizo zilizokamatwa Septemba Mosi, 2018 katika Kijiji cha Katarabuga Kata Bwanjai Mkuu wa Mkoa wa  Kagera Brigedia Marco E. Gaguti alilipongeza Jeshi la Polisi Mkoani Kagera kwa kutekeleza wajibu wake ipasavyo pamoja na ushirikiano kutoka kwa wananchi ambao kwa kiasi kikubwa walisaidia katika ukamatwaji wa Kahawa hizo.

Mkuu wa Mkoa Gaguti alisema kuwa katika Mkoa wa Kagera haitawezekana kuruhusu wahujumu uchumi kuendelea na vitendo vya biashara ya magendo na katika kuhakikisha hilo halifanyiki alisisititiza Kamati za Ulinzi na Usalama za Kata na Vijiji kuhakikisha zinatimiza wajibu wake ipasavyo kwa kuwashirikisha wananchi katika maeneo yao ili wawadhibiti watu kama hao.

“Katika Mkoa wetu mwaka huu 2018 tumelenga kukusanya tani 81,000 za Kahawa lakini kwa vitendo hivi vya utoroshaji Kahawa kimagendo bila kufuata utaratibu wa kulipa kodi hatuwezi kufikia lengo. Sisi Serikali ya Mkoa hatuwezi kurusu ardhi yetu itumike bure alafu mchana tunashangilia maendeleo ya nchi kumbe usiku kuna watu wanafanya biashara haramu tena kwa kutumia miundombinu yetu iliyogharamiwa na kodi za wananchi wakati wao wanakwepa kodi hizo, hiyo haikubaliki.” Alisisitiza Mhe Gaguti.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera Augustne Olomi alisema kuwa Jeshi hilo linawashikilia watuhumiwa wanne kutokana na tukio hilo. Aidha, Kamanda Olomi alisema baada ya taratibu zote kukamilika Kahawa hizo zilizokamatwa zaidi ya tani 10 zitauzwa kwa njia ya mnada na fedha zikazopatikana zitaingizwa kwenye mfuko wa mapato ya Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.

Wananchi au wafanyabiashara ya Kahawa wanashauriwa kuachana na biashara ya magendo bali wauze Kahawa yao kwa mfumo sahihi uliowekwa na Serikali ili kodi husika zilipwe. Kama kuna mwanachi au mfanyabiashara anataka kuuza kahawa yake nje ya nchi ni shariti kufuata utaratibu uliopo na kulipa kodi zote za Serikali na ataruhusiwa kuuza Kahawa yake popote pale nje ya nchi.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa