• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Walimu Wawili Watuhumiwa wa Mauaji ya Mwanafunzi Sperius Eradius Wafikishwa Mahakamani na Kusomewa Shitaka Linalowakabili

Imewekwa : September 3rd, 2018

Watuhumiwa wawili Mwalimu Respicius Patrick Mtazangira na Mwalimu Herieth Gerald wa mauji ya Mwanafunzi Sperius Eradius (13) aliyekuwa akisoma Shule ya Msingi Kibeta Manispaa ya Bukoba wamefikishwa Mahakama ya Wilya ya Bukoba  leo Septemba 3, 2018 na kusomewa shitaka la mauaji linalowakabili mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi John Kapogoro.

Katika kesi hiyo ya Mauaji Namba 18 ya Mwaka 2018 watuhumiwa hao wawili Mwalimu Respicius Patrick na Mwalimu Herieth Gerald hawakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa Mahakama ya Wilaya haina mamlaka ya kusikiliza kesi yao bali Mahakama Kuu, mara baada ya kusomewa shitaka linalowakabili walirudishwa Mahabusu.

Kesi hiyo Namaba 18 ya Mwaka 2018 ilihairishwa hadi tarehe 17 Septemba, 2018 kwaajili ya kukamilisha taratibu za Kimahakama ili iweze kuhamishiwa Mahakama Kuu kwa ajili ya kusikilizwa. Hakimu Mkazi Mfawidhi John Kapogoro mara baada ya watuhumiwa kusomewa shitaka alimuru warudishwe mahabusu kwani shitaka linalowakabili halina dhamana.

Akitoa ufafanuzi wa kesi hiyo Kaimu Wakili wa Serikali Mfawidhi Athuman Matuma Kirati alisema kuwa ushaidi wa kesi hiyo umekamilika kwa asilimia 100% na ofisi yake inaendelea na utaratibu wa kufungua jarada la kesi hiyo Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba ambapo alisema kuwa leo mchana Septemba 3, 2018  jarada la kesi hiyo litaweza kufunguliwa katika Mahakama Kuu.

Wakili wa Serikali Matuma alisema kuwa katika kesi hiyo ya mauji Namba 18 ya mwaka 2018 kulingana na ushahidi uliokusanywa na kukamilika kwa asilimia 100% unaonesha kuwa mauaji ya Mwanafunzi Sperius Eradius yalikuwa ni mauaji ya kukusudia kutokana na siraha alizoshambuliwa nazo mwanafunzi huyo.

“Ushahidi wetu unaonesha kuwa Mwalimu Respicius Mtazangira alikuwa anamshambulia Mwanafunzi Sperius Eradius kwa vipande vya kuni vilivyokuwa vimekusanywa na wanafunzi wa darasa la saba kwaajili ya kupikia chakula chao, Pili pamoja na Marehemu Sperius Eradius kupiga kelele sana kuwa anauwa akiomba msaada kwa wanafunzi wenzake waende kumnusuru bado Mwalimu Mtazangira aliendelea kumpiga mwanafunzi huyo.” Alieleza Wakili Matuma.

Pamoja na ushahidi huo lakini Wakili wa Serikali Matuma alieleza kuwa baadhi ya Walimu walimwendea Mwalimu Respicius Mtazangira kumuomba aache kumpiga mwanafunzi huyo lakini aliendelea kumpiga jambo ambalo linaonesha alikusudia kumuua mwanafunzi Sperius Eradius.

Marehemu Sperius Eradius alifariki dunia Agosti 27, 2018 muda mchache baada ya kupigwa shuleni Kibeta na Mwalimu Respicius Patrick Mtazangira aliyekuwa Mwalimu wa nidhamu katika shule hiyo kwa kutuhumiwa kuiba mkoba (pochi) ya Mwalimu Herieth Gerald. Marehemu Sperius Eradius alizikwa Agosti 31, 2018 nyumbani kwa baba yake Mzazi Kata Mubunda Kijiji Kitoko Wilayani Muleba.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa