• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Wananchi wa Kisiwa Cha Ikuza Waondokana na Adha ya Huduma za Afya Baada ya TANAPA Kukabidhi Zahanati Kwa Serikali Tayari Kwa Huduma

Imewekwa : April 16th, 2019

Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) yaikabidhi Serikali mradi wa ujenzi wa Zahanati uliojengwa kwa ushirikiano kati ya TANAPA, Halmashauri ya Wilaya ya Muleba na Wananchi wa Kijiji cha Ikuza kilichopo Kisiwani Ikuza ambapo mradi huo uligharimu kiasi cha shilingi milioni 280,953,625/= hadi kukamilika kwa hatua ya kwanza ya ujenzi wa vyumba kumi na moja vya vyakutolea huduma.

Akikabidhi Zahati hiyo Aprili 16, 2019 Naibu Kamishina Mkuu wa TANAPA Bw. Martin Leboki aiyemwakilisha Mkurugenzi Mkuu TANAPA Taifa Bw. Alani Kijazi alimweleza Mkuu wa Mkoa wa Kagera na wananchi waliohudhuria hafla fupi ya makabidhiano kuwa zahanati hiyo imejengwa na kukamilika kwa ushirikiano mkubwa kati ya Halmashauri ya Wilaya ya Muleba na wananchi wa kijiji cha Ikuza kutokana na ujirani mwema wa Hifadhi ya Taifa ya Rubondo.

Bw. Leboki alisema kuwa TANAPA ilitoa jumla ya shilingi milioni 144,725,675/= katika ujenzi wa zahanati hiyo yenye vyumba kumi na moja na kununua vifaa tiba kama vitanda vya wagonjwa, vitanda vya akinamama wajawazito kujifungulia pamoja na samani nyingine zitakazotumika katika zahanati hiyo. Aidha Halmashauri ya Wilaya ya Muleba ilichangia jumla ya shilingi milioni 124,392,340/= na wananchi walichangia jumla ya shilingi milioni 14,535,000/=

Pamoja na kukamilika kwa zahanati hiyo ya Kijiji Ikuza lakini wananchi walibainisha kuwa bado kuna changamoto ya kutokuwa na shimo la kutupia kondo la nyuma, upatikanaji wa umeme na maji katika zahanati hiyo. Pamoja na changamoto hizo lakini wananchi wa Kijiji Ikuza waliishukuru TANAPA kwa kukubali kushirikiana nao kuwajengea zahanati ili kutatua changamoto ya upatikanaji wa huduma ya afya katika kisiwa hicho na visiwa vya jirani.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti akipokea zahanati ya Kijiji Ikuza kwa niaba ya Serikali aliishukuru TANAPA kwa kushirikiana na wananchi wa Ikuza na kuwajengea Zahanati ya kuwahudumia na kuwaondolea changamoto ya upatikanaji wa huduma ya afya katika kisiwani humo pamoja na visiwa vya jirani.

Mkuu wa Mkoa Gaguti alisema kuwa pamoja na Serikali kuwa imeendelea kuboresha huduma za afya kwa kasi kubwa tangu mwaka 2015/16 lakini bado kuna uhitaji mkubwa hasa katika vijiji ambapo alisema kuwa mwaka 2015/16 mkoa wa Kagera ulikuwa unapokea fedha za afya shilingi milioni 800/= lakini hadi sasa mkoa unapokea shilingi bilioni 5 kwa mwaka, Wilaya ya Muleba ilikuwa inapokea shilingi milioni 400 lakini sasa inapokea shilingi bilioni 1 kwa mwaka.

Aidha, Mkuu wa Mkoa Gaguti alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano katika mkoa wa Kagera imejenga Vituo vya Afya 14 kwa gharama ya shilingi bilioni 6.9 na tayari imeto shilingi bilioni 4.5 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali za Wilaya .  “Pamoja na juhudi hizo zote kufanyika lakini uhuhitaji katika vijiji ni mkubwa na kama hatutajenga zahanati kama hizi mlundikano katika Vituo vya Afya utakuwa mkubwa mno.” Alisisitiza Mhe. Gaguti

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa Gaguti alitoa maagizo kuwa zahanati hiyo inatakiwa kuanza kutoa huduma mara moja isikae tena mwaka bila kutoa huduma kwa wananchi. Kuhusu changamoto za wananchi juu ya shimo la kondo la nyuma alitoa mifuko 50 ya saruji ili shimo hilo lianze kujengwa kwa kushirikiana na wananchi wa kijiji cha Ikuza.

Kuhusu umeme, Mkuu wa Mkoa Gaguti alimwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Bw. Emannuel Shelembi kufunga mara moja solar ambayo tayari ipo katika ofisi za Halmashauri pia kuhakikisha Mkurugenzi huyo anaandaa watumishi wa kwenda kutoa huduma katika zahanati hiyo. Na kuhusu suala la maji aliwahakikishia wananchi kuwa atatoa Sim tank ya lita 5000 na wao wachimbe mtaro kutokea ziwani ili maji yapatikane kwa haraka.

Mwisho, Mkuu wa Mkoa Gaguti aliwashukuru TANAPA kwa kuendelea kudumisha ujirani mwema na wananchi wanaopakana na Hifadhi za Taifa ambapo alimshukuru tena Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA Taifa kwa kumkubalia kushirikiana naye kujenga Zahanati katika vijiji vinavyopakana na Mapori yaliypandishwa hadhi na kuwa hifadhi za Taifa za Biharamulo Burigi na Kimisi, Ibanda na Rumanyika.

Naye diwani wa Kata ya Ikuza Mhe. Fortunatus Wazia Matta aliishukuru TANAPA na Serikali kwa kuwasogezea karibu wananchi huduma ya afya kwani alisema kuwa tangu alipochaguliwa kuwa diwani wa kata ya Ikuza mwaka 2010 hadi sasa wakina mama wajawazito wanne tayari wamepoteza maisha yao kutokana na changamoto ya afya katika kata hiyo iliyopo visiwani.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa