• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Washiriki wa Mafunzo ya PS3 Juu ya Utoaji Motisha kwa Watumishi Mkoani Kagera.

Imewekwa : November 4th, 2017

PS3 Yazinoa Halmashauri Mkoani Kagera Juu ya Motisha Kwa Watumishi Ili Kuboresha Utoaji Huduma Kwa Wananchi

Mradi wa kuimarisha Mifumo katika Sekta ya Umma Tanzania (PS3) wawanoa watendaji na Waajiri Mkoani Kagera namna bora ya kuwamotisha watumishi wao katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ili watumishi hao waweze kufikia malengo na matarajio ya utoaji wa huduma kwa wananchi.

Mafunzo hayo ya siku sita Mkoani Kagera yamewahusisha Wenyeviti, Wakurugenzi na  Wakuu wa Idara wa Halmashauri za Wilaya mbili za Biharamulo na Kyerwa ambazo zipo katika awamu ya kwanza ya Mradi wa PS3 pamoja na Wakuu wa Idara katika idara za Utawala na Raslimali Watu kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Kagera Kagera.

Mafunzo hayo yamelenga kuboresha utendaji na utoaji wa huduma bora kutoka kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa kwenda kwa wananchi ambapo mtumishi akipewa motisha mbalimbali anazozistahili hutekeleza majukumu yake kwa ufanisi mkubwa na mwananchi hupata huduma anayostahili kupata na kwa wakati.

Mafunzo hayo yamelenga kuwakumbusha Waajiri na Wakuu wa Idara hasa Idara za Utawala na Raslimali Watu kutoa motisha kwa watumishi wao jambo ambalo litawafanya watumishi hao kufanya kazi katika eneo lolote hata kama kuna changamoto za baadhi ya huduma za jamii mfano vijijini ambako huduma za maji na umeme hazijawafikia wananchi.

Akitoa ufafanuzi juu ya ufanisi wa mafunzo hayo Bw. Aloyce Msigwa kutoka PS3 Makao Makuu Dodoma alisema Mradi unalenga kuwakumbusha waajiri na wakuu wa idara juu ya utoaji wa motisha ili huduma kwa wananchi ziweze kuboreka lakini pia na kupunguza msongo wa mawazo kwa watumishi wakati wakitekeleza majukumu yao.

Akifunga mafunzo hayo Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu Ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Kagera Bw. Nesphory Bwana aliwakumbusha washiriki wa mafunzo hayo kuwa Serikali ilishatoa mwongozo wa namna ya kuwahamasisha watumishi ili waweze kutoa huduma bora kupitia utoaji wa motisha.

“Mwongozo huo ulitolewa kupitia Sera ya Malipo na Motisha ya mwaka 2010 na upo muda mrefu lakini kwa sababu mbalimbali waajiri na hasa Mamlaka za Serikali za Mitaa wamekuwa wazito katika kubuni mbinu za kuutekeleza. Wakati mwingine jambo hili halitekelezwi siyo kwa sababu ya uwezo mdogo wa Halmashauri bali kwa sababu ya Uongozi husika kutokuona umuhimu wake na hivyo kutolipa kipaumbele.” Alisistiza Bw. Nesphory 

Aidha, Bw. Nesphory alitoa wito kwa viongozi wote, watendaji na wanasiasa kubadilika na kulipa umuhimu jambo hilo kwa kuanza kulitengea bajeti kila mwaka kwa yale ambayo Halmashauri ina uwezo nayo.

Katika hatua nyingine Halmashauri za Wilaya za Biharamulo na Kyerwa ziliweza kupata fursa ya  kuandaa mipango ya motisha kwa watumishi wao na pia mikakati ya kuitekeleza mipango hiyo. Ambapo pia Halmashauri hizo mbili ziliweza kubadilishana mipango hiyo ya motisha kwaajili ya ufanisi zaidi.

Mafunzo hayo yalifunguliwa Oktoba 30, 2017 na Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Kamishna Diwani Athumani na yamefungwa leo Novemba 4, 2017.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa