• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Wasimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mkoani Kagera Wala Viapo na Kuonywa Kuwa Waadilifu Katika Majukumu Yao

Imewekwa : September 12th, 2019

Serikali Mkoani Kagera yajipanga vyema kuhakikisha uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 24, 2019 haukwamishwi kwa kikwazo chochote hasa maandalizi muhimu ambapo Wasimamizi wa Uchaguzi huo  Katika ngazi za Halmashauri za Wilaya nane wameapishwa na kula viapo kusimamia uchaguzi huo.

Wasimamizi hao nane walioteuliwa rasmi Septemba 11, 2019 na Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Seleman Jaffo na wakila viapo vya uaminifu, utii na uadilifu mbele ya Mhe. Flora Kaijage Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya Bukoba Septemba 12, 2019 na kuwa wasimamizi rasmi wa uchaguzi wa Serikali za mitaa Mkoa Kagera.

Kabla ya viapo hivyo Mwanasheria wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera Wakili Jovini Rutahinurwa aliwakumbusha wasimamizi wateule kuwa viapo hivyo vipo kwa mujibu wa kanuni za sheria ya uchaguzi wa viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa ngazi za Vijiji, Vitongoji na Mitaa ya mwaka 2019

Kanuni hizo alizitaja Wakili Jovini kuwa ya kwanza ni Kifungu namba 44 kifungu kidogo cha 4 tangazo la Serikali namba 371 la mwaka 2019. Pili, Kifungu namba 46 kifungu kidogo cha 4 tangazo la Serikali namba 372 la mwaka 2019.Tatu, Kifungu namba 47 kifungu kidogo cha 4 tangazo la Serikali namba 373 la mwaka 2019. Nne, Kifungu namba 47 kifungu kidogo cha 4 tangazo la Serikali namba 374 la mwaka 2019 pamoja na Sheria ya Viapo na Matamko ya Kisheria  sura ya 34.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Profesa Faustin Kamuzora mara baada ya wasimamizi hao kula viapo vyao mbele ya Mhe. Flora Kaijage Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya Bukoba aliwapongeza na kuwakumbusha wajibu wao kuwa wameaminiwa na Serikali kwa kupitia mchujo mkali kwahiyo wanatakiwa kutekeleza majukumu yao kwa utii, uaminifu na uadilifu mkubwa kama walivyoapa.

Profesa Kamuzora aliwataka wasimamizi hao kusoma nyaraka na  miongozo yote kuhusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kuyaelewa maeneo yao ya utawala  ili kuhakikisha hakuna mapingamizi yanayoweza kujitokeza. Pia alisistiza kuwa Serikali kuanzia ngazi ya wizara hado mkoa imefanya maandalizi ya kutosha kuhakikisha uchaguzi huo unafanyika kwa ufanisi mkubwa ukilinganisha na uchaguzi wa miaka iliyopita.

Aidha, Profesa Kamuzora alitoa angalizo kwa Viongozi wa Vyama vya Siasa kuhakikisha wanatoa wagombea wenye sifa hasa katika Wilaya za mipakani za Missenyi, Karagwe, Kyerwa na Ngara kuepusha wahamiaji haramu kugombea nafasi hizo. “Kama ikibainika Serikali itachukua hatua za kisheria kwa wahusika lakini rai yangu ni kwa wananchi kutoa taarifaau  pingamizi pale mhamiaji haramu atakapopitishwa kugombea  itakapotokea.” Alisisitiza Profesa Kamuzora

Katika hatua nyingine Profesa Kamuzora alisema kuwa Mkoa wa Kagera unatarajia kuadikisha wapiga kura wapatao 1,288,370 na vituo vya kupigia kura vikiwa ni 3,738 kwenye vijiji 662 na  Vitongoji 3,665 katika Kata 92 aidha,  zikiwa Tarafa 27.

Wasimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mkoani Kagera walioteuliwa na kuapishwa rasmi Septemba 12, 2019 ni Bw. Richard Masanilo Mihayo Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba, Bablyus  Lubingo Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba, Bw. Albert Mamimo Msemwa Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi, Bw. Rajab Khasim Byoma Halmashauri ya Wilaya Karagwe.

Wengine ni Bw. John Mayuga Msafiri Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa, Bw. Lucas Haga Daudi Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, Bw. Costantino Francis Msemwa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo na Bi Essery Felician Pima Halmashauri ya Wilaya ya Muleba.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa