• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Waziri Jafo Aridhishwa Na Utekelezaji wa Miradi ya Elimu Kagera Asema Shule ya Sekondari Ihungo Viwango Vyake Hakuna Tanzania Nzima

Imewekwa : June 5th, 2020

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI) Selemani Jafo aridhishwa na utendaji kazi  wa viongozi wa Mkoa wa Kagera wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti katika usimamizi wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na  Serikali na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Waziri Jafo ameyasema hayo akiwa Mkoani Kagera Manispaa ya Bukoba katika ziara ya siku moja  Juni 5, 2020 wakati akitembelea na kukagua miradi ya maendeleo katika Shule za Sekondari za Rugambwa (wasichana) na shule ya Sekondari ya Ihungo (Wavulana) pia na mradi wa barabara za kilometa tano wenye gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 7.3.

Akiwa katika Shuleza Sekondari Ihungo na Rugambwa Waziri Jafo alisema kuwa ameridhishwa  sana na ukarabati wa shule hizo kongwe ulivyofanyika na kuzifanya shule hizo kuwa mpya kabisa. Pia aliwashukuru wanafunzi wa kidato cha sita katika shule hizo kutii maelekezo ya Serikali baada ya janga la ugonjwa wa KORONA kwa kurudi shule kwa asilimia 99 kuendelea na masomo yao.

Waziri Jafo aliwapongeza Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kwa kutekeleza mradi mkubwa wa ujenzi wa Shule ya Sekondari Ihungo kwa viwango vya hali ya juu sana ambapo alisema kuwa ubora wa majengo  ya shule hiyo ni wa kwanza nchini na kutoa rai kwa uongozi wa Mkoa wa Kagera kuacha ndoto za kugeuza shule hiyo kuwa Chuo Kikuu  badala yake wanafunzi wasome katika mazingira bora zaidi.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kagera akitoa taaarifa katika shule hizo alisema kuwa  Mkoa wa Kagera unazo shule za Sekondari za Kidato cha Tano na Sita 36 zenye wanafunzi wa kidato cha sita 3,590 na wanafunzi 3,393 tayari wameripoti katika shule hizo kuendelea na masomo yao ya kidato cha sita  wanafunzi 197  asilimia 5 bado hawajaripoti.

Ikumbukwe kuwa Serikali ilitoa zaidi ya shilingi milioni 872 kwaajili ya ukarabati wa shule ya Sekondari Rugambwa na zaidi ya shilingi  bilioni 11 kuijenga upya shule ya Sekondari Ihungo baada ya Tetemeko la Ardhi lililotokea Septemba 10, 2016 na kufanya uharibifu wa  miundombinu yote ya Shule hiyo na kulazimika kujengwa upya.

Katika hatua nyingine Waziri Jafo alitembelea na kukagua mradi wa barabara za kilometa (5) tano katika Manispaa taya Bukoba ambapo hakuridhishwa na utekelezaji wa barabara hizo kwa kusuasua na kutumia muda mrefu kukamilika ujenzi wake ambapo alitoa maagizo kwa Mkandarasi  JASCO ROAD CONSTRUCTION kuhakikisha anakamilisha kazi ya barabara zote ifikapo Juni 15, 2020 vingnevyo asipokamilisha barabara hizo hatopewa tena kazi yoyote katika Wizara yake ya TAMISEMI.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa