• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Waziri Kangi Lugola Aliasa Jeshi la Polisi Mkoani Kagera Kutekeleza Majukumu Yake Kwa Weledi na Kulinda Raia na Mali Zao

Imewekwa : January 3rd, 2019

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Kangi Alphaxard Lugola awasili Mkoani Kagera na kuanza ziara yake ya siku saba kwa kutembelea Idara zilizoko chini ya Wizara yake ili kujionea utendaji kazi katika idara hizo ikiwa ni pamoja na kufanya mkutano wa hadhara kusikiliza na kutatua kero za  wananchi hasa zinazohusu Idara zilizopo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Waziri Kangi Lugola mara baada ya kuwasili Mkoani Kagera Januari 2, 2019 aliitembelea Idara ya Huduma za Uangalizi inayosimamia utekelezaji wa adhabu mbadala nje ya Magereza. Adhabu mbadala kwa kifupi ni aina ya hukumu itolewayo na Mahakama kwa mtu aliyepatikana na hatia kwa kosa la jinai ambapo kisheria mfungwa hupewa adhabu ya kufanya kazi ya kutoa huduma kwa jamii bila ya malipo kwa faida ya jamii.

Akiwa Katika ofisi ya Idara ya Huduma za Uangalizi yenye mtumishi mmoja Mkoani Kagera Waziri Kangi Lugola baada ya kusomewa taarifa ya idara hiyo alisema kuwa idara hyo ipo chini ya Wizara yake ya Mambo ya Ndani ya nchi na katika Idara zenye watumishi wengi ni pamoja na Idara hiyo yenye Watumishi 160 lakini shughuli zake hazifahamiki  na tija yake ni ndogo sana kwa wananchi.

“Idara hii zamani ilifahamika kama Bwana Huruma kwani ilikuwa inawasaidia wafungwa waliokuwa wanaonesha mwenendo mzuri katika Magereza kufungwa kifungo cha nje lakini baada ya kubadilishwa jina wananchi wengi haifahamu,” Alifafanua Waziri Kangi Lugola. Aidha, Waziri Lugola alitembelea Idara za Polisi, Uhamiaji, Jeshi la Zimamoto na Idara ya Vitambulisho vya Taifa NIDA na kujionea utendaji kazi wa idara hizo Mkoani Kagera.

Mkutano wa Hadhara

Akiwa katika Mkutano wa hadhara uwanja wa Uhuru Manispaa ya Bukoba Waziri Kangi Lugola aliongea na wananchi na kusikiliza kero mbalimbali hasa kero kubwa ililihusu Jeshi la Polisi Mkoani Kagera katika utendaji wake wa kazi hasa katika Upande wa usalama barabarani na Bodaboda. Waendesha Pikipiki maarufu kama Bodaboda walililalamikia Jeshi la Poilisi kuwakamata bila kuvaa sare za Jeshi hilo, kuwakimbiza na kuwasababishia ajali zinazopelekea ajali mbaya na pengine kupelekea vifo.

Akitoa ufafanuzi Waziri Kangi Lugola alisema kuwa Jeshi la Polisi wanatakiwa kufanya kazi kwa weledi wakiwa wameva sare za Jeshi hilo na hairuhusiwi kwa Askari Polisi yeyote kumkata Bodaboda bila kuvaa sare za Jeshi la Polisi kwani wamesababisha hata majambazi kuwadhuru Bodaboda wakijifanya ni Askari wa Jeshi la Polisi na kuwanyanganya Pikipiki zao.

Waziri Kangi Lugola alisema kuwa Jeshi la Polisi wanatakiwa kulinda raia na mali zao na si vinginevyo ambapo alitoa mfano kwenye ardhi kuwa wananchi wanyonge wamekuwa wakidhurumika sana katika upande wa ardhi lakini Jeshi la Polisi wapo na hawatekelezi wajibu wao bali matajiri wenye fedha wanaendelea kuwanyanyasa wananchi masikini kwa kuchukua ardhi zao na kuzitumia katika ujenzi.

Pia Waziri Kangi Lugola aliwaomba wananchi wa Mkoa wa Kagera kuwa wazalendo kwa kutowapa hifadhi wahamiaji haramu na kutoa msaada kwa Serikali kuisaidia Idara ya Uhamiaji kwa kutoa taarifa pale wanapogundua kuwa kuna wahamiaji haramu katika maeneo yao kwani Mkoa wa Kagera ni mkoa ambao unapakana nachi nyingi.

Katika hatua nyingine Waziri Kangi Lugola alitoa ufafanuzi mambo makuu mawili ambayo aliwahi kuyasema hapo awali. Kwanza, Askari wa Usalama Barabarani kukamata gari na kumhesabia dereva makosa zaidi ya moja na kila kosa kutozwa faini ya shilingi 30,000/=, Waziri Kangi Lugola alisema kuwa gari likibainika kuwa lina makosa zaidi ya moja dereva anatakiwa kulipia kosa moja tu la ubovu wa gari lakini si kila kosa kulipia faini tajwa hapo juu.

Pili, Waziri Kangi Lugola alitoa ufafanuzi juu ya suala la mabasi ya abiria kuanza safari alfajiri saa 11:00 badala ya saa12:00 asubuhi. Waziri Kangi Lugola alisema suala hilo linaendelea kufanyiwa kazi na Serikali na baada ya Januari 10, 2018 Serikali itatoa msimao wa suala hilo na utaratibu mzuri wa utekelezaji.

Waziri Kangi Lugola yupo Mkoani Kagera kwa ziara ya siku saba kuanzia tarehe 2.01.2019 hadi 8.01.2019 ambapo atafanya ziara katika  Wilaya zote za Mkoa kwa kufanya Mikutano ya Hadhara kuongea na wananchi na kutatuta kero zao pia kuongea na watumishi wa Idara zilizopo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa