• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Waziri Luhaga Mpina Aliyeshika Mtumbwi Akikagua Mitumbwi Zaidi ya 50 Iliyokamatwa na Katika Doria za Kudhibiti Uvuvi Haramu Mkoani Kagera

Imewekwa : December 6th, 2017

Waziri Mpina Amsimamisha Kazi Mtumishi Aliyeruhusu Samaki Kutoroshewa Nchini Burundi Bila Kufuata Sheria Za Nchi.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina amtumbua Afisa wa Kitengo cha Doria na Udhibiti wa Uvuvi mpakani Bw. Ayoub Ngoma ambaye aliruhusu gari lililokuwa limebeba samaki wasioruhusiwa kuvuliwa zaidi ya tani mbili ambapo samaki hao walikuwa wakitoroshwa kuelekea nchini Burundi kupitia mpaka wa Murusagamba Wilayani Ngara.

Waziri Mpina alimwagiza Katibu mkuu wa Wizara  yake Dk. Yohana Budeba kuhakikisha anamsimamisha kazi mara moja mtumishi huyo kabla ya saa 6:00 mchana na kupewa taarifa pia na taratibu za kumfukuza kazi zianze mara moja  baada ya kuonekana anashirikiana na waharifu kuihujumu Serikali.

Agizo hilo lilitolewa na Waziri Mpina akiwa katika siku yake ya pili ziarani Mkoani Kagera tarehe 6.12.2017 alipofanya ziara katika Idara ya Maendeleao ya Uvuvi Mkoa wa Kagera na kupokea taarifa kutoka kwa Kaimu Afisa Mfawidhi Usimamizi wa Raslimali zaUvuvi Kagera Bw. Gabriel Mgeni ambapo alitolea taarifa tukio hilo lililotokea Murusagamba Wilayani Ngara Desemba 3, 2017.

Bw. Mgeni alisema kuwa  tarehe 3.12.2017 majira ya saa 9:00 asubuhi Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya  Ngara walikamata gari lenye namba za usajili T 614 CLQ aina ya Mitsubishi Canter ikiwa imepakia samaki wenye uzito wa zaidi ya kilo 2,000 aina ya Sangara kilo 530 Samaki  aina ya Sato.

Kwa mujibu wa sheria namba 22 ya mwaka 2003 watuhumiwa waliokamatwa wanasafirisha samaki hao walikuwa wamekiuka   taratibu zifuatazo ; kuvua  samaki wenye ukubwa zaidi ya sentimita 85 na wadogo chini ya sentimita 50, kutokuwa na kibali cha kusafirisha mazao ya uvuvi, kutolipa mrahaba wa Serikali, kutokuwa na cheti cha afya pamoja na leseni ya kuuza mazao ya uvuvi nje ya nchi.

Bw. Mgeni alisema kuwa samaki hao baada ya kukamatwa Mahakama ilitoa kibali maalum na kugawa samaki hao kwenye taasisi za Serikali na wananchi. Waziri Mpina alizishukuru Kamati za Ulinzi na Usalama Mkoani Kagera kwa juhudi kubwa za kupambana na vitendo haramu vya kutorosha maliasili za nchi nje ya nchi.

Waziri Mpina pia alitoa rai kwa watumishi ambao wapo chini ya Mamlaka yake kuwa kwa yeyote ambaye atagundulika kujihusisha na vitendo vya kuihujumu Serikali hawezi kubaki  kazini  kwani akibainika tu lazima achukuliwe hatua kali ikiwa ni pamoja na kufukuzwa kazi moja kwa moja. Vilevile alimwagiza Mwanasheria wa Wizara yake kuhakikisha anaharakisha mchakato wa kuitaifisha gari lililokamatwa na samaki likiekea nchini Burundi.

Aidha, katika hatua nyingine Waziri Mpina alijionea mafurushi 6 ya samaki aina ya migebuka kilo 240 yaliyokamatwa katika kituo Kikuu cha Mabasi Bukoba yakisafirishwa kwenda nchini Uganda, Mabondo kilo 100 ambapo mtuhumiwa wake alikamatwa na kufikishwa kituo cha Polisi, Majora 200 yenye thamani ya shilingi milioni 20 na mitumbwi zaidi ya 50 iliyokamtwa katika doria .

Waziri mpina aliiagiza Idara ya Maendeleo ya Uvuvi Kagera kuhakikisha inaendelea na juhudi za kukamata wale wote wanaojihusisha na vitendo vya uvuvi haramu na utoroshaji wa samki nje ya nchi ambapo tani 100 hutoroshwa kila wiki kuelekea nchi jirani.  Waziri Mpina amehitisha Ziara yake ya Siku mbili Mkoani Kagera leo tarehe 6.12.2017 na kuelekea Mkoani Kigoma.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa