• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Waziri Luhaga Mpina (Wa tatu Kutoka Kushoto) Akikagua Sehemu ya Kunyweshea Maji Ng'ombe Katika Ranchi ya Kagoma

Imewekwa : December 6th, 2017

Waziri Mpina Amutimua Mwekezaji Mbabaishaji Agri Ranch Katika Ranchi ya Taifa ya Kagoma Mkoani Kagera

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina ampa  siku saba mwekezaji wa Ranchi za Kagoma, Mabale na Kikurula AGRI RANCHI  kuwa ameondoa  mifugo yake katika Ranchi hizo baada ya kukiuka masharti ya mkataba wake na Kampuni ya Huria (Ranchi)  za Taifa (NARCO) na kuendelea kutumia Ranchi hizo kwa miaka mitano bila kutimiza masharti ya Mkataba.

Waziri Mpina akiwa Mkoani Kagera kwa ziara ya siku mbili kuanzia tarehe 5 hadi 6 Desemba 2017 alitembelea Huria (Ranchi) ya Kagoma Wilayani Muleba na kukutana na Mwekezaji AGRI RANCH ambaye anawekeza katika Ranchi tatu za Kagoma, Mabale na Kikurula na kutembelea  mifugo yake,  kukagua miundombinu aliyowekeza katika Ranchi  ya Kagoma  pia na Kuongea na mwekeza ji huyo.

Baada ya kutembelea miundombinu katika Ranchi hiyo na kupata maelezo ya AGRI RANCH pamoja na Meneja Mkuu wa NARCO Profesa Philemon Wambura Waziri Mpina alitoa uamuzi kuwa anakubaliana na maamuzi ya NARCO ya kuvunja Mkataba na AGRI RANCH kwasababu Kampuni hiyo ilikiuka masharti ya Mkataba huo tangu mwaka 2012 ilipopewa Ranchi hizo tatu kuwekeza.

“Kuanzia sasa nakubaliana na maamuzi ya NARCO ya kuvunja Mkata ba na Kampuni hii kwani wamekiuka Mkataba tangu mwaka 2012 walipopewa Ranchi zetu kuwekeza. katika Mkataba huo AGRI RANCH ilitakiwa kujenga kiwanda cha kusindika nyama na machinjio ya kisasa lakini hadi sasa kwa miaka mitano hawajawahi kufanya lolote ,” alisisitiza Waziri Mpina.

Vilevile Waziri Mpina alisema kuwa AGRI RANCHI ilitakiwa kuilipa Serikali kiasi cha Shilingi bilioni tatu kila mwaka lakini hadi sasa haijawahi kulipa fedha hizo bali wamelipa kiasi kidogo sana katika Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba , kwahiyo kwa miaka mitano wanadaiwa kiasi cha shilingi bilioni 15 pia Kampuni hii  ilitakiwa kuwa na ng’ombe zaidi 25,000 katika Ranchi zetu lakini hadi sasa ng’ombe waliopo ni  4500 tu.

Aidha, Meneja Mkuu wa NARCO  Profesa Philemon Wambura alisema Kampuni ya AGRI RANCH imekiuka mashariti yote ya mkataba na tayari NARCO wameionya mara nyingi kampuni hiyo na kukaa nao kwa majadiliano mara kwa mara laikini AGRI RANCH hawakutekeleza chochote ambapo NARCO ikaamua kuvunja Mkatana kutoa “notice” ya mwekeza huyo kuondkoa tangu mwaka 2014 lakini bado ameendelea kukaidi hadi sasa.

Baada ya maelezo hayo Waziri Mpina alisema kuwa Serikali haiwezi kuendelea kwavumilia wawekezaji waongo ambao hawana mitaji lakini wanaidanganya Serikali na kutumia Raslimali za wananchi isivyopaswa  ambapo aliwaagiza NARCO kufanya tathimini ya kina juu ya hasara iliyosababishwa na Kampuni hiyo na kuilipa Serikali ikiwa ni pamoja na Bilioni 15 walizokwepa kulipa awali.

Katika hatua nyingine Waziri Mpina alimwagiza Meneja Mkuu wa NARCO Profesa Philemon Wambura kuhakikisha kuwa ndani ya Siku sana awe amepeleka Meneja Katika Ranchi ya Kagoma na walinzi wa kuilinda Ranchi hiyo isivamiwe wakati mwekezaji anaendelea kuondoa mifugo yake katika Ranchi hiyo.

Pia kuendelea kuweka mazingira mazuri  kwa wawekezaji  wa  Vitalu vya ufugaji Mkoani kagera Waziri Mpina alimwagiza Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mhandisi Richard Luyango kwa kushirikiana na NARCO kubaini mipaka halisi ya vitalu na kutoa mapendekezo juu ya wananchi waliovamia vitalu hivyo ili kuondoa kabisa tatizo la uvamizi wa vitalu vya wawekezaji.

Akijitetea mbele ya Waziri Mpina Meneja wa Kampuni ya AGRI RANCH Bw. Rutagwelela Mbelwa alisema hawakujenga kiwanda cha nyama kutokana na ng’ombe aina ya ankole kutokuwa na nyama inayokidhi viwango kwahiyo kampuni hiyo ilijikita katika ufugaji wa ng’ombe aina ya borani ili kupata nyama inayokidhi viwango vya kimataifa ndipo kiwanda kingejengwa.

Pili  Bw. Mbelwa alisema kuwa Kampuni yake AGRI RANCH inaomba kubaki na na Ranchi moja ya Kagoma lakini Mabale na Kikurula Serikari inaweza kuzitaifisha ambapo maelezo hayo hayakubatilisha msimamo wa Waziri Mpina na kusisitiza kuwa waondoe mifugo yao mara moja katika Ranchi za Serikali.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa