• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Waziri Mkuu Awasili Mkoani Kagera na Kutoa Wito Kwa Wakandarasi Wazawa Kukamilisha Miradi Kwa Wakati Wanayopewa na Serikali Bila Visingizio

Imewekwa : February 20th, 2019

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa Majaliwa amewasili Mkoani Kagera leo tarehe 20 Februari, 2019 kwa ziara ya siku mbili ambapo mara baada ya kuwasili Nyakanazi Wilayani Biharamulo akitokea Mkoani Kigoma aliongea na wananchi katika Mkutano wa hadhara na kuwaeleza wananchi jinsi Serikali inavyoendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo hasa katika Mkoa wa Kagera.

Katika Mkutano wa hadhara Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitoa wito kwa Sekta binafsi pale zinapoaminiwa na Serikali na kupewa miradi ya kutekeleza kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa na kukamilika kwa wakati. Waziri Mkuu alisikitishwa na Mkandarasi anayeendelea kujenga barabara ya Nyakanazi Kibondo Kilometa 50 (Nyanza Roadworks Ltd) kutomaliza barabara hiyo kwa wakati pamoja na  kuwa Serikali tayari imeilipa Kampuni hiyo ya Kitanzania fedha za kujenga barabara hiyo.

“Sijaridhishwa na kiwango cha ujenzi wa barabara ya Nyakanazi Kigoma, jana nimeongea na Mkandarasi anasingizia hana malori na hana vifaa wakati tayari tumemlipa fedha. Serikali imekuwa ikakaa na Sekta binafsi na kuongea nao na kilio chao kilikuwa ni kuaminiwa na kupewa kazi na Serikali lakini walio wengi hawatekelezi miradi hiyo na kuimaliza kwa wakati mfano hii barabara imeanza tangu mwaka 2014 mpaka sasa bado Mkandarasi anajikongoja tu.” Alieleza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema kuwa kama Mkandarasi huyo atashindwa kukamilisha barabara hiyo ifikapo mwezi Aprili 2019 Serikali itamfukuza kazi. Barabara ya Nyakanazi Kibondo kilometa 50 ilianza kujengwa mwaka 2014 na kulingana na Mkataba ilitakiwa kuwa imekamilika ifikapo Juni 2016 lakini mpaka sasa bado haijakamilika.  Aidha gharama za ujenzi wa barabara hiyo ni bilioni 45.986 mpaka kukamilika hadi kiwango cha rami.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa pia aliwaeleza wananchi wa Nyakanazi waliokusanyika kumsikiliza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano itahakikisha inakamilisha kwa asilimia 90% miradi yote ya maendeleo ambayo ilihaidiwa wakati wa uchaguzi mwaka 2015 katika sekta za Elimu, Maji, Afya na Miundombinu ya barabara na umeme kwa wananchi ifikapo mwaka 2020.

Pia Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliwaeleza wananchi wa Nyakanazi kuwa Serikali tayari imetabiri eneo la Nyakanazi kuwa litakuwa mji mkubwa hapo baadae kutokana na eneo hilo kukaa kimkakati  ambapo kuna barabara kuu za kwenda nchi jirani za Rwanda , Burundi na Serikali tayari imeamua kupaboresha Nyakanazi kwa kutoa fedha shilingi bilioni tatu  kujenga miundombinu mbalimbali ya kimkakati ili kuliandaa eneo hilo kuwa mji mdogo na wananchi wafanye biashara na na Serikali kuingiza mapato.

“Tayari mkataba umesainiwa kati ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo na Wizara ya Fedha ili ujenzi uanze na tunatarajia kujenga Kituo kikubwa cha Mabasi, Kituo cha kuegesha magari makubwa, Soko kubwa la kisasa, na Jengo kubwa la maduka na kituo kikubwa cha ukaguzi. Fedha tayari zipo na kinachosubiriwa ni kutangaza tenda. Tunataka Nyakanazi pabadilike kwa kasi kubwa na wananchi wanufaike na eneo hili la kimkakati.” Alisisitiza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliwakemea viongozi wa Wilaya ya Biharamulo kuacha malumbano na ugomvi kati yao na wawe mfano kwa watumishi na wananchi wanaowaongoza na kushikamana na kushirikiana kuleta maendeleo kwa wananchi. Waziri Mkuu aliwaonya viongozi hao na kusema kuwa kama hawataacha ugomvi wao na malumbano atamshauri Rais wa Jamhuri ya Muungano aangalie upya uteuzi wao upya.

Mwisho Waziri Mkuu aliwataka watumishi wa Halmashauri ya Biharamulo kuhakikisha wanasimamia na kukusanya mapato ya Serikali ipasavyo. Pia aliwakumbusha wananchi wa Nyakanazi kuhakikisha wanakuwa wazalendo kwa kutumia mfumo wa nyumba kumi za usalama kuimarisha ulinzi na usalama hasa kwa wahamiaji haramu kutoka nchi jirani ambao wamekuwa wakija nchini na kufanya vitendo vya uharifu.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa