• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Atatua Changamoto la Zao la Kahawa Mkoani Kagera Kwa Kueleza Namna Bora ya Mfumo Mpya Utavyofanya Kazi

Imewekwa : October 6th, 2018
  • Atoa Wito Kwa Wananchi wa Kagera Kuacha Mazoea na Kuukubali Mfumo,
  • Awaonya Polisi Kuacha Kusindikiza Magendo,

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa katika siku yake ya kwanza ziarani  Mkoani Kagera aeleza na kufafanua juu ya mfumo mpya wa ununuzi wa kahawa na jinsi Serikali ilivyojipanga kuhakikisha mkulima ananufaika pia mfumo mpya utakavyobershwa  katika Msimu wa Kahawa  wa mwaka 2019 ili Vyama Vikuu vya Ushirika visifanye biashara ya Kahawa bali Wafanyabiashara tu..

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alieleza hayo Oktoba 6, 2018 kwenye kikao cha wadau wa Kahawa Manispaa ya Bukoba katika ukumbi wa Hoteli ya ELCT Bukoba mara baada ya kupata taarifa fupi kutoka kwa  Waziri wa Kilimo Dk.Charles Tizeba kuhusu ukusanyaji, uuzaji wa Kahawa na malipo ya wakulima pamoja na changamoto za mfumo mpya katika uuzaji wa Kahawa  Mkoani Kagera.

Waziri wa Kilimo Dk. Charles Tizeba alimweleza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika kikao hicho kuwa changamoto kubwa iliyojitokea katika Msimu huu wa 2018 kwenye zao la Kahawa Mkoani Kagera Moja ni Kahawa kushuka bei katika soko la dunia kuliko ilivyowahi kushuka kwa miaka 12 iliyopita kutokana na wazalishaji wakubwa wa Kahawa duniani kuzalisha Kahawa kwa wingi sana.

Pili ni Kahawa kununuliwa kwa kiwango kidogo na kusababisha mlundikano wa kahawa iliyokusanywa kutoka kwa wakulima katika maghara ya Vyama Vikuu vya Ushirika na kusababisha Wakulima kutolipwa fedha zao kwa wakati ambapo jumla ya tani 11,000 za Kahawa bado zipo magharani. Tatu  Waziri Tizeba alisema kuwa ni propaganda za kuishusha Kahawa bei iliyokuwa ikiendelea kwa baadhi ya wafanyabiashara ili kunufaika kwa kununua Kahawa  kwa bei ndogo.

Baada ya kupata taarifa hiyo Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa alisema kuwa Serikali inasisitiza uchumi wa viwanda ili Tanzania iweze kusonga katika uchumi wa kati ambapo mazao ya sita ambayo Serikali imeyawekea mkakati wa kuhakikisha yanapewa kipaumbele na kuchakatwa katika viwanda ili kuleta mapinduzi katika kilimo na kwenye sekta ya Viwanda kwa kujenga viwanda vya kusindika au kuongeza thamani ya mazao hayo.

Akitaja mazao hayo Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa alisema kuwa Pamba, Chai, Tumbaku, Korosho, Kahawa na Mchikichi ndiyo mazao ya kimkakati kwa sasa katika kuleta mapinduzi ya kilimo na viwanda. Aidha, alisema katika maeneo yote mfumo wa kununua na kuuza mazao hayo unaenda vizuri isipokuwa zao la Kahawa Mkoani Kagera bado lina shida kubwa kutokana na kutokubalika kwa mfumo huo mpya ulioletwa na Serikali kukusanya na kuuza Kahawa kutokana na baadhi ya watu kujikita mizizi kwenye “Obutura”.

Mfumo Mpya wa Kuuza Kahawa

“Nimezunguka kote nchini na mfumo wa kuuza mazao yote  ya kimkakati umekubalika maeneo yote kwenye Pamba, Korosho, Ufuta lakini Kagera imeshindikana kwasababu ya watu wachache kufanya biashara ya “Obutula”. Niwashauri wakulima wa Kagera kubadilika katika mfumo wenu wa kutaka malipo ya awali na ndiyo inayosababisha matatizo haya yote, lakini tukiacha mazoea ya kulipwa kwanza tutafanikiwa kwa kiwango kikubwa na lazima tusubiri malipo ya pamoja. “Alieleza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.”

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema kuwa ili kutatua changamoto ya malipo ya wakulima kuchelewa na kahawa kuendelea kukaa kwenye maghara tani 11,000 alimua kukaa na Wafanayabiasha wa Kahawa ili kuwasikiliza na kukubaliana nao namna bora ya kununua Kahawa ambapo alikubaliana nao katika kikao chake cha awali kuwa watanunua kahawa yote tani 11,000 ambayo Vyama Vikuu vya Ushirika tayari vimeikusanya kwa wakulima na ipo katika mghara ya Vyama hivyo.

Serikali Kuboresha Mfumo Wa Ununzi Msimu wa 2019

Waziri Mkuu alisema kuwa kuanzia msimu ujao wa Kahawa wa Mwaka 2019 minada yote ya uuzaji wa Kahawa haitafanyika Moshi Mkoani Kilimanjaro bali itafanyika Mkoani Kagera. Pili alisema lazima tozo za Kahawa zifanane katika Vyama vya Ushirika na alitolea mfano wa KDCU LTD na KCU 1990 LTD kuwa tozo zao zinatofautiana wakati zao la Kahawa ni moja na linatoka mkoa mmoja.

Chama Kikuu cha KCU 1990 LTD kati ya tozo 23 zilizokuwepo awali kimepunguza tozo tano tu na kubaki na 18 wakati KDCU LTD wao wamepunguza tozo tatu tu na kubaki na tozo 20. Kwanini zitofautiane wakati Kahawa ni ileile na inatoka Mkoa wa Kagera. “Aliuliza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa”

Vyama Vikuu Kutofanya Biashara Ya Kahawa Msimu wa 2019

Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa alisema kuanzia Msimu wa 2019 Vyama vyote Vikuu vya Ushirika havitarusiwa tena kufanya biashara ya Kahawa ambapo vimekuwa vikisababisha hasara kubwa kwa ubadhirifu wa fedha na kusabisha Serikali kulipa madeni ya Vyama hivyo na watakaoruhusiwa kufanya biashara ya Kahawa ni Wafanyabiashara tu.

Aidha, Benki ya Maendeleo ya Kilimo haitatoa tena fedha kwenye Vyama Vikuu vya Ushirika bali kwa Wafanyabiashara tu wa kununua na kuuza Kahawa. Viongozi wa Vyama vya Ushirika watasimamia utaratibu wa wafanyabiashara kununua na kuuza Kahawa Katika Vyama vya Msingi na kuvisimamia Vyama hivyo katika mfumo huo mpya vilevile kutoa vibali vya kusafirisha Kahawa nje ya nchi kwa wafanyabiashara.

Katika Mfumo huo mpya wa kuuza Kahawa ya Wakulima Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitoa wito kwa wakulima na wananchi wa Mkoa wa Kagera kuhakikisha wanafungua akaunti katika Benki za NMB na CRDB ili malipo yao yawe yanapitia katika benki hizo badala ya kulipwa fedha mkononi na alisisitiza kuwa Wanankagera kuwa ni waelewa hawahitaji kusukumwa katika hilo.

Jukumu la vyama vya Msingi ni kuhakikisha vinawatambua wakulima wake kila mahali walipo na kujua mkulima mmoja mmoja ana uwezo gani wa kuzalisha Kahawa ili mfumo wa ununuzi ukiwa mzuri mkulima aweze kunufaika na kuboresha shamba lake na kuvuna zaidi.

Akifafanua juu ya Vyama Vikuu vya Ushirika kufanya Biashara Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema kuwa Chama Kikuu chaUshirika KCU 1990 LTD kinadaiwa mabilioni ya fedha na taasisi mbalimbali za Serikali na zisizokuwa za Serikali kutokana chama hicho kujiingiza kwenye biashara. Pili alisema kuwa chama hicho kutokana na kukopa fedha sehemu mbalimbali bila kulipa kina kesi zaidi ya 10 Mahakamani nyingi zikiwa za Madai.

Magendo Ya Kahawa Obutura

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliwaagiza Wakuu wa Wilaya kuhakikisha wanasimamia magendo ya kahawa katika maeneo yao kikamilifu. Aidha, alimwagiza Kamanda wa Polisi Mkoa Agustine Olomi kuwaonya Askari walio chini yake hasa Katika Wilaya ya Kyerwa kuacha tabia ya kusindikiza kahawa za Magendo bali wafanya kazi yao kama sheria inavyowaelekeza.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitoa onyo kwa Viongozi wa Serikali na Watumishi kutojihusisha kwenye biashara ya magendo hasa katika Wilaya ya Kyerwa na kama hawataacha tabia hiyo Serikali itawachukulia hatua za kisheria mara moja.

Katika Hatua nyingine Waziri Mkuu Kassim majaliwa alivitembelea Viwanda vya BUKOP na Kiwanda cha TANICA vilivyopo katika Manispaa ya Bukoba na kuongea na watumishi wa viwanda hivyo na kupongeza Menejimenti za Viwanda hivyo kuajili watanzania zaidi ya 1800.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa