• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Auagiza Uongozi na Jeshi la Polisi Mkoani Kagera Kukomesha Magendo ya Kahawa Mara Moja Wilayani Kyerwa

Imewekwa : October 7th, 2018

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassimu Majaliwa aendelea na ziara yake Mkoani Kagera Wilayani Kyerwa na Karagwe ambapo Kyerwa alitembelea Chama cha Msingi Nkwenda na Kumuagiza Mkuu wa Mkoa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera kuhakikisha wanachukua hatua mara moja kukomesha magendo ya Kahawa Wilayani Kyerwa.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitoa onyo kali kwa Kamanda wa Polisi Wilaya ya Kyerwa kuhakikisha anakomesha magendo ya Kahawa na kuacha tabia ya kushiriki kusindikiza kahawa za magendo kutoroshwa kuelekea nchi jirani wakati jukumu la Jeshi la Polisi ni kudhibiti magendoi ya kahawa.

“OCD (Kamanda wa Polisi Wilaya ya Kyerwa) wewe na baadhi ya Maafisa wenzako mnalichafua Jeshi la Polisi kwa kusindikiza kahawa za magendo, acha tabia hiyo mara moja tutakuvua vyeo na kusimamisha kazi wakati bado familia yako inakutegemea. OCD simamia kahawa, OCD simamia Kahawa, OCD simamia Kahawa.” Alimuonya Kamanda wa Polisi Wilaya ya Kyerwa Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa.

Aidha, katika hatua nyingine alimuagiza Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti kwa kushirikiana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera Augustine Olomi kuhakikisha wanashughulika na Wilaya ya Kyerwa kwa kukomesha Magendo ya Kahawa katika Wilaya ya Kyerwa ili kahawa iuuzwe kwa mfumo halali wa Ushirika na kumnufaisha mkulima moja kwa moja.

Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa alirudia kauli ya Serikali alaiyoitoa Oktoba 6, 2018 akiwa Manispaa ya Bukoba  ya kuuboresha mfumo mpya wa kunuanua kahawa Mkoani Kagera na kusema kuwa  kuanzia msimu ujao wa mwaka 2019/2020 Mnada wa Kahawa utafanyika Mkoani Kagera ili kupunguza gharama za makato kwenye fedha za Wakulima.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliwahakikishia wananchi ambao tayari wamekusanya kahawa yao kwenye Chama Kikuu cha Ushirika KDCU Limited na hawajalipwa fedha zao kuwa  watalipwa kwani  Benki ya Maendeleo ya Kilimo tayari imetoa fedha kwa chama hicho ili kuwalipa wakulima hao. Pia alikiagiza Chama cha Msingi Nkwenda ambacho alitembelea kiwanda chake cha Kukoboa kahawa kuwa kitangaze mara moja mnada wa kahawa ambayo tayari wameikusanya ili kuwalipa Wakulima.

Vile vile Mbunge wa Kyerwa Innocent Bilakwate na Mbunge wa Viti Maalum Oliver Semguruka waliwasilisha kero za wananchi katika Sekta za Maji, Afya, Elimu na Ardhi ambapo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imeendelea kutatua changamoto mbalimbali za wananchi katika maeneo mbalimbali nchini mfano kwa kuongeza ujenzi wa vituo vya afya, madawa na watumishi.

Aidha, katika Sekta za Maji na Ardhi Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliwahidi wananchi wa Wilaya ya Kyerwa kuwa atawatuma Mawaziri wa Sekta hizo kwenda Wilayani Kerwa  kusikiliza kero hizo kuzitatua na kuchukau hatua kama kutakuwa na uzembe uliofanyika kwa kusababishwa na Watendaji  wa Serikali.

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa alitembelea kiwanda cha KADERES cha kukoboa kahawa chenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.5 kinachomilikiwa na Mwekezaji Leonard Kachebonaho Wilayani Karagwe na kupongeza juhudi za mwekezaji huyo za kuajili wananchi wenzake na kupunguza uhuhitaji wa ajira kwa vijana nchini.

Kiwanda hicho cha KADERES kinakoboa kahawa na kuzipanga kwa madaraja, pia kinaajili wananchi wazawa 30 hadi 200 na kinawahudumia wakulima 1800 ambapo kwa msimu huu wa mwaka 2018/2019 kitaanza kulipa wakulima waliokusanya kahawa yao kwa kiasi cha shilingi 1,700/=  kwa kilo na baadae wakulima hao watalipwa shilingi 100/= na kukamilisha jumala ya shilingi 1,800/=.

Mara baada ya kukitembelea kiwanda hicho Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano itaendelea kuunga Mkono wawekezaji katika Sekta ya Viwanda kwa kusema kuwa viwanda vina mambo makuu muhimu matatu. Kwanza kuboresha mazao mbalimbali ya kilimo na biashara kwa kuyaongezea thamani, Pili viwanda vinpunguza sana tatizo la ajira kwa kuajili wananchi wengi kwa wakati mmoja.

Tatu, ni kutoa fursa kwa wananchi wazawa Watanzania kujifunza teknolojia na ujuzi wa kuendesha viwanda wazawa wenyewe bila kutegemea wataalam kutoka nje ya nchi. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alimalizia kuwa Viwanda vimeondoa vijiwe vya vijana kwa kutoa ajira nyingi kwa vijana nchini. Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa alimalizia ziara yake Wilayani Karagwe kwa kuongea na wananchi katika Mkutano wa hadhara Uwanja wa Changarawe Kayanga.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa