• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa Kufanya Ziara ya Siku Nne Mkoani Kagera Oktoba 06 - 09, 2018

Imewekwa : October 5th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti anawataarifu  Wananchi wote wa Mkoa wa Kagera kuwa Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (MB) Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atafanya ziara ya Siku nne hapa Mkoani kwetu Kagera kuanzia tarehe 6 Oktoba, 2018 hadi tarehe 9 Oktoba, 2018.

Mhe. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anatarajia kuwasili Mkoani kwetu tarehe 06/10/2018 siku ya Jumamosi saa 7:00 Mchana katika Uwanja wa Ndege wa Bukoba.  Mhe. Waziri Mkuu mara baada ya kuwasili Mkoani atapokea taarifa ya Mkoa na mara baada ya kupokea taarifa hiyo ataanza ziara yake katika Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba na atatembelea Kituo cha Utafiti wa Kilimo Maruku, atatembelea pia Kiwanda cha kukoboa kahawa cha BUKOP LTD na Kiwanda cha TANICA katika Manispaa ya Bukoba na ataongea na wadau mbalimbali wa Kahawa pamoja na Viongozi wa Vyama vya Ushirika Mkoani Kagera katika Ukumbi wa Hoteli ya ELCT Bukoba. Tarehe 07/10/2018 Mhe. Waziri Mkuu ataendelea na ziara yake Wilayani Kyerwa kwa kutembelea AMCOS ya Nkwenda baada ya hapo ataelekea Wilayani Karagwe ambapo atatembelea Kituo cha Afya Kayanga, Kuzindua Kiwanda cha Kukoboa Kahawa cha KADERES na kuongea na wananchi katika Mkutano wa Hadhara Uwanja wa Changarawe Kayanga. 


Mhe. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ataendelea na ziara yake Mkoani Kagera tarehe 08/10/2018 Wilayani Muleba na Biharamulo ambako atetembelea Shamba bora la Kahawa, Kituo cha Afya Kimeya na kuongea na Watumishi na Wananchi. Aidha, Mhe. Waziri Mkuu ataelekea Biharamulo ambako atatembelea Mgodi wa STAMIGOLD na kuongea Wananchi katika Mkutano wa Hadhara Nyakanazi.


Mhe.  Waziri Mkuu atahitimisha ziara yake Mkoani Kagera tarehe 9 Oktoba, 2018 atakapopokea Vyumba vya Madarasa Katika Shule ya Msingi Nyakato na Kashozi vilivyojengwa kwa msaada wa Ubalozi wa nchi ya Japan baada ya kuathiriwa na Tetemeko la Ardhi mwaka 2016. Pia atetembelea kiwanda cha Kahawa cha Amir Amza na kuongea na Wananchi wa Manispaa ya Bukoba na Viunga vyake Katika Uwanja wa Uhuru (Mayunga).


Mkuu wa Mkoa Mhe. Gaguti anawaomba wananchi wote wa Mkoa wa Kagera kuonesha ushirikiano, bashasha na ukarimu kwa Mhe. Waziri Mkuu kwa kufika kwa wingi katika maeneo yaliyotajwa kumpokea na kumkaribisha katika Mkoa wetu wa Kagera. Pia Wilayani ambako Mhe. Waziri Mkuu atatembelea wananchi wanahamasishwa kufika kwa wingi kumsikiliza kwa muda utakaokuwa umepangwa kuongea na wananchi katika Mikutano ya Hadhara.


Aidha, Mkuu wa Mkoa Gaguti anatoa wito kwa wananchi kudumisha umoja, amani na mshikamano wakati wote wa ziara ya Mhe. Waziri Mkuu na kutojihusisha na vitendo vya uhalifu kwa kuwa Vyombo vya Ulinzi na Usalaama vipo tayari muda wote kushughulika na wananchi wasiopenda amani. Aidha, kama ilivyo kawaida ya wananchi wa Mkoa wa Kagera kudumisha usafi wa mazingira tunaomba kudumisha utamaduni huo  ili kuweka maeneo yetu katika hali ya usafi.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa