• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba Akiongea na Wananchi Wakati Uzinduzi wa Uandikishaji wa Vitambulisho vya Taifa Mkoani Kagera.

Imewekwa : February 16th, 2018

Waziri Mwigulu Azindua Uandikishaji Wa Vitambulisho vya Taifa Kagera,

Aagiza Jeshi la Polisi Kuchunguza Mauaji Nchini na Kutoa Taarifa.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk. Mwigulu Lameck Nchemba azindua rasmi zoezi la uandikishaji wa Vitambulisho vya Taifa Mkoani Kagera katika Kijiji cha Kasindaga Kata Kabitembe Wilayani Muleba leo Februari 16, 2018.

Katika uzinduzi huo Waziri Mwigulu aliwasisitiza wananchi kuhakikisha kila mmoja  kuanzia umri wa miaka 18 nakuendelea kujiandikisha au kutambuliwa  na kusajiliwa kwaajili ya kupata kitambulisho cha Taifa ambacho ni muhimu sana kwa kila Mtanzania kwa maisha ya kila siku.

Waziri Mwigulu alisema kuwa Kitambulisho cha Taifa ni muhimu sana kwa masuala ya kiusalama ambapo kila mwananchi atatambuliwa, Wakimbizi wote watatambuliwa na wale wote wanaotoa huduma za kiubalozi watatambuliwa na hakuna Mtanzania ambaye anatakiwa kubaki bila kutambuliwa.

Pia Waziri Mwigulu amewaasa wananchi wa Mkoa wa Kagera kuwa na wivu wa uzalendo na nchi yao na mkoa wao pia kwa kutoa taarifa sahihi  kwa wasio raia wa Tanzania  kwa kuwa Kagera kuna vivutio vingi  na  unapakana na nchi nyingi jambo ambalo linawavutia watu au wahamiaji haramu kuingia nchi jirani.

“ Katika Mahabusu za Mkoa wa Kagera kuna waharifu wenye kesi za uharifu wa kikatili kuliko mahabusu za mikoa mingine lakini ukichunguza kwa undani utagundua wahalifu hao siyo Watanzania bali ni kutoka nchi za jirani ambapo hawana huruka za Kitanzania bali ukatili tu,” Alitoa mfano Waziri Mwigulu.

Katika Hatua nyingine Waziri Mwigulu alimwagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania Simon Sirro kutumia vyombo vyake vyote  vya uchunguzi kuhakikisha anachunguza mauaji  ya  wananchi katika maeneo mbalimbali nchini (Akitolea mfano wa Kijana aliyeuawa Kinondoni wa chama cha CHADEMA) na baada ya uchunguzi Jeshi hilo litoe taarifa kwa wananchi ili kujua chanzo cha mauaji hayo.

Kwaniaba ya Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Hamelore M. Manyanga ambaye ni Kamishna wa Huduma za Sheria katika uzinduzi huo alitoa rai kwa wananchi kutoa taarifa sahihi wakati zoezi la utambuzi na usajili  wa Vitambulisho vya Taifa likiendelea. Pia aliwaasa watendaji kuhakikisha wanajiepusha na vitendo vya rushwa katika zoezi hilo vinginevyo hatua kali za kisheria zitachukuli kwa atakayebainika.

Aidha, Bw. Alphonce Malibicha Kaimu Mkurugenzi wa Uzalishaji wa Vitambulisho vya Taifa kwaniaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NIDA alisema kuwa wananchi wanaotakiwa kusajiliwa ni umri kuanzia miaka 18 na kuendelea na raia wa Tanzania . Pia alisema kuwa uandikishaji unaendelea katika Mikoa 19 sasa Tanzania Bara na Kagera sasa imeongezeka baada ya kufanyika uzinduzi rasmi.

Bw. Malibicha alizitaja faida za Vitambulisho vya Taifa kuwa ni pamoja na huduma mbalimbali za kijamii, Vitambulisho vya Taifa vitatumika katika kusajili Makampuni ambapo mmiliki taarifa zake lazima zionekane kwenye kitambulisho, Vitatumika wakati wa kupata Hati ya kusafiria, Vitatumika katika mifuko ya Hifadhi za jamii katika kutoa huduma za mafao kwa wananchama wake pia na kubaini Wahamiaji Haramu.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu katika uzinduzi huo alitoa maagizo kwa Watendaji wa ngazi zote kuhakikisha wanashiriki kikamilifu kufanikisha zoezi la uandikishaji  kwa kusimamia zoezi zima hasa Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya chini ya Wenyeviti wake Wakuu wa Wilaya.

Aidha, Mkuu wa Mkoa Kijuu alitoa wito kwa watendaji kutojihusisha na vitendo vya rushwa katika zoezi hilo kwani wakibainika hatua kali zitachukuliwa mara moja. Pia aliwaasa wananchi kuhakikisha wahudhuria kujiandikisha kwa muda watakaopewa na wasisubiri muda wa mwisho na kusababisha msongamano.

Mwisho Mh. Kijuu aliwaomba viongozi wa dini kuwahamasisha waamini wao kujiandikisha kila mmoja. Pia alisistiza kuwa zoezi la uandikishaji lisichukuliwe kidini wala kisiasa kwa kuwapotosha wananchi na mwisho wake baadhi yao wakabaki bila kujisajili na kupata Vitambulisho vya Taifa.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa