• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina Akiangalia Shehena ya Samaki "Kayabo" Tani 65.6 Waliokamatwa Kisiwani Lubili Wilayani Muleba Mkoani Kagera

Imewekwa : January 8th, 2018

Serikali Mkoani Kagera Yakamata Tani Samaki Wenye Thamani ya Zaidi ya Milioni 200 Waliovuliwa Kwanjia Haramu Kisiwani Lubili

Serikali Mkoani Kagera yakamata na kutaifisha tani 65.6 za samaki aina ya sangara wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 200 waliovuliwa kwa njia haramu na kukaushwa kwa chumvi  (samaki hao wanajulikana kwa jina maarufu kama kayabo) ambao walikuwa wanaandaliwa tayari kusafirishwa kwenda nchi za nje kwa ajili ya kuuzwa.

Samaki hao waliovuliwa kwanjia haramu ni chini ya sentimeta 50 na juu ya Sentimeta 85 yaani samki watoto na samaki wazazi ambao hawaruhusiwi kishera kuvuliwa na walikamatwa katika Kisiwa cha Lubili Wilayani Muleba  tarehe 30.12.2017 na kusombwa kuletwa katika kituo cha Maendeleo ya Uvuvi Kagera.

Kaimu Mkurugenzi  idara ya Maendeleo ya Uvuvi  Bi Mwanaidi Mlolo  akiambatana na Waziri wa Mifugo na Uvuvi kujionea samaki hao katika kituo cha Maendeleo ya Uvuvi Kagera Januari 6, 2018 alisema  samaki hao walivuliwa kinyume na sheria namba 22 ya mwaka 2003 na kanuni zake za mwaka 2009. Ambapo pia sheria hiyo inatoa mamlaka ya kutaifisha vifaa vyote vilivyotumika katika zoezi zima la uvuvi haramu.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina akikagua tani 65.6 za samaki hao (Kayabo) katika kituo cha Maendeleo ya Uvuvi Kagera Januari 6, 2018 alisema kuwa samaki hao walivuliwa kwanjia haramu na walitarajiwa kutoroshwa kupelekwa nchi jirani kuuzwa bila kulipiwa mrahaba wa Serikali.

Waziri Mpina aliagiza samaki hao wauzwe kwa njia ya mnada kwa wafanyabiashara wenye vibali na  leseni za kusafirisha samaki (kayabo) nje ya nchi ili  Serikali iweze kupata mapato yake. Aidha, alitoa rai kwa wafanyabiashara wa samaki kufuata kanuni, taratibu na sheria  katika kufanya biashara zao na bila kufanya uharibifu kwa kufanya uvuvi haramu.

Agizo, Mhe. Mpina aliwaagiza Watendaji chini ya Wizara yake kuhakikisha kuwa kila mfanyabiashara atakayekwenda  kuhuwisha leseni yake ili kupata leseni mpya lazima mfanyabiashara huyo awe na kibali cha kulipia kodi (Tax Clearence) kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

“Kwa kuwa leseni za uvuvi hutolewa kila mwaka mwezi Januari, wafanyabiashara ambao bado hawajaomba leseni upya lazima waje na kibali cha kulilipa kodi (Tax Clearance) ndipo wapate leseni mpya. Aidha, kwa ambao tayari walikuwa wamepata leseni mpya wahakikishe wanawasilisha vibali vyao vya kulipia kodi ndipo wataendelea kuruhusiwa kufanya biashara ya samaki,” alisistiza Waziri Mpina.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu alitoa rai kwa wananchi wa mkoa wa Kagera kutoa taarifa walipojificha wahusika waliovua samaki hao katika Kisiwa cha Lubili ili Serikali iweze kuwachukulia hatua mara moja. Pia Mkuu wa Mkoa alisistiza kuwa pamoja na wahusika wa tukio hilo kutoroka lakini Serikali ina mkono mrefu itaweza kuwakamata na kuwafikisha katika mikona ya sheria.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa