• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Hatuna Changamoto ya Fedha za Malipo ya Awali Kwa Wakulima wa Kahawa Napita Kuona Msimu Unaendeleaje – RC Gaguti

Imewekwa : September 3rd, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti afanya ziara katika wilaya tatu kukagua msimu wa kahawa wa 2019/2020 unavyoendelea hasa lengo kuu likiwa ni kuona wakulima kama wanalipwa fedha zao kwa wakati bila ucheleweshwaji na kama kuna changamoto zozote ziweze kutatuliwa.

Septemba 3, 2019 Mhe. Gaguti akiwa katika Chama cha Msingi Muungano na Nkwenda Wilayani Kyerwa akiongea na wananchi na wakulima wa kahawa alisema kuwa taarifa alizonazo na anazozipokea kila siku ni kuwa Vyama Vikuu vya Ushirika vya KDCU LTD na KCU 1990 LTD havidaiwi na Vyama vya Msingi kwa hiyo hakuna sababu ya malipo ya kwanza kwa wakulima kucheleweshwa.

“Ukiondoa wakulima ambao walipeleka kahawa zao kwenye vyama vya msingi ndani ya siku saba hadi kumi kufikia leo tarehe 3 Septemba, 2019 wakulima wote hakuna anayedai kwani fedha zipo za kuwalipa, taarifa nilizonazo hakuna mkulima yeyote anayedai fedha za mwezi wa saba mwisho wa kulipa ilikuwa ni tarehe 23.08.2019.” Alifafanua Mkuu wa Mkoa Gaguti

Katika Vyama vya Msingi  vya Muungano, Nkwenda Wilayani Kyerwa na Kamahungu Wilayani karagwe akiongea na wakulima Mhe. Gaguti alitoa nafasi kwa wakulima wanaovidai Vyama vya Msingi malipo ya kwanza ya muda mrefu kujitokeza ili ajue tatizo ni nini. Katika mikutano hiyo wakulima waliojitokeza ni wale ambao walipeleka kahawa zao kwenye vyama vya msingi mwishoni mwa mwezi wa Agosti, 2019 na malipo yao tayari yapo kwa taratibu za kulipwa tangu tarehe 3/08/2019.

Aidha, Mhe. Gaguti alimchukulia hatua za kinidhamu mkulima  mmoja wa Chama Msingi  Kamahungu Wilayani Karagwe kwa kumdanganya kuwa anadai chama hicho fedha zake tangu mwezi Julai 2019 ambapo alipohakiki katika vitabu vya chama hicho alikuta kuwa si kweli mkulima yule aliuza kahawa yake mwezi Julai bali  mwishoni mwa mwezi Agosti 2019.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa Gaguti alisema kuwa bado hajaridhishwa na matumizi ya ushuru unaokatwa kwenye kahawa ya wakulima na Vyama vya Msingi ambapo alisema kuwa tayari analifanyia kazi suala hilo kuona ushuru huo unapunguzwa na mkulima anapata fedha zaidi maana fedha hiyo inatumika bila ridhaa ya wakulima wa Vyama vya Msingi bali viongozi vinatumia fedha hizo na kutoa taarifa kwa wakulima jambo ambalo si sawa.

Katika suala hilo Mkuu wa Mkoa Gaguti alisema kuwa angependa kuona fedha za ushuru zinaboresha kwanza Vyama vya Msingi kuliko kwenda kwenye matumizi mengine. Fedha hizi zingeweza kununulia mizani ya kidigitali ambayo itaondoa utata katika upimaji wa kahawa ya mkulima, pili fedha hiyo inunue vifaa vya kupima unyevunyevu katika kahawa ili mkulima asiendelee kukatwa kilo moja ya unyevu kwenye kahawa yake.

“Hili tunalifanyia kazi na nitaunda timu ya wataalam ili kuhakikisha changamoto zote hizo katika zao la kahawa linapatiwa ufumbuzi na mkulima kuneemeka na jasho lake.” Alisistiza Mkuu wa Mkoa Gaguti. Katika Wilaya ya Missenyi Mhe. Gaguti alitembelea vitalu vya kuzalisha miche ya kahawa ambapo lengo ni kuinua uzalishaji katika Wilaya hiyo.

Katika msimu wa mwaka huu wa kahawa wa 2019/2020 tayari Vyama Vikuu vya Ushirika vya KCU 1990 LTD na KDCU LTD mkoani Kagera vimekusanya zaidi ya kilo milioni 35 sawa na asilimia 75 ya kahawa inayotarajiwa kukusanywa katika msimu mzima na zaidi ya shilingi bilioni 35 tayari zimelipwa kwa wakulima. Aidha, makisio ya ukusanyaji katika msimu huu ni kukusanya kilo milioni 52

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa