• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Kagera Katika Kuadhimisha Siku ya Redio Duniani Februari 13, 2018

Imewekwa : February 12th, 2018

Jenga Uchumi na Redio Zetu Kagera “Redio Ni Wewe”

Tunapoelekea kuadhimisha Siku ya Redio Duniani Mkoa wa Kagera unajivunia kuwa na Vituo vya Redio Vipatavyo tisa sasa vinavyorusha matangazo yake ndani na nje ya Mkoa. Vituo hivyo vikiwa na malengo ya kuhabarisha, kuelimisha na kuburudisha wananchi vinarusha matangazo yake katika mfumo wa FM (Frequency Modulation) mfumo ambao unarusha mawimbi yake na kusikika vizuri kwa wananchi.

Kaulimbiu ya mwaka  huu katika Maadhimisho Siku ya Redio Duniani Februari 13, 2018 inasema "Redio ni Wewe" ikilenga kuwa mifumo ya matangazo ya redio imebadilika kwa kuendana na teknolojia kiasi kwamba matangazo husikika hata kupitia simu za mkono,  kwa hiyo mwananchi haitaji kubeba redio kubwa bali hata simu yake anaweza kusikiliza redio mahala popote atakapokuwa.

Mkoa wetu wa Kagera tunajivunia kuadhimisha siku hii muhimu sana kwani imekuwa ni hatua kubwa mkoa kuwa na vituo tisa sasa ambavyo vinarusha matangazo yake hapa mkoani. Vituo hivyo ni Kwizera FM, Kasibante FM, Vision FM, Karagwe FM, FADECO FM, Bukoba FM, Kagera Community Radio FM, Shinuz FM, na Mbiu FM (Ambayo ipo katika hatua za mwisho kuanza kurusha matangazo yake).

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu anasema haya ni mapinduzi makubwa katika Mkoa kuwa na vituo hivyo tisa vinavyorusha matangazo yake ndani na nje ya mkoa kwani vimekuwa chachu ya kuhamasisha maendeleo kwa wananchi, wananchi wenyewe hupata habari muhimu na kuelimika juu ya mambo mbalimbali kuhusu maendeleo yao.

“Sisi Serikali Redio hizi za kijamii zimetusaidia sana katika kuwapelekea wananchi jumbe mbalimbali hasa zinazohusu maendeleo ya mkoa katika kukuza uchumi. Lakini pia hata sisi viongozi wa Serikali hizi Redio zimetusaidia sana kujua kero mbalimbali za wananchi pale wanapopaza sauti zao kupiti redio hizo nasi kuzifanyia kazi mara moja. Kwahiyo unaweza kuona ni jinsi gani redio zetu zinavyoweza kutuunganisha na kuwa wamoja ,”  Alifafanua Mkuu wa Mkoa Kijuu.

Ikumbukwe kuwa hadi kufikia miaka ya 1990 Mkoa wa Kagera ulikuwa hauna kituo hata kimoja cha redio bali Redio zilizosikika wakati ule ni kutoka nje ya mkoa na zilikuwa Redio Tanzania Dar es Salaam (RTD), Redio Free Africa, Redio One, KBC (Kenya), Redio West (Uganda), na nyinginezo nyingi.

Mwaka 1995 ndipo Redio Kwizera ilianziashwa Wilayani Ngara lakini ikilenga kutoa habari zihusuzo Wakimbizi waliokuwa wamekimbilia Tanzania kutoka Rwanda na Burundi katika Vita vya wenyewe kwa wenyewe. Baadae zilifuata Redio za  Karagwe FM na FADECO FM mwaka 2007, Kasibante mwaka 2008 na nyinginezo zilifuata miaka ya 2010 hadi sasa.

Katika kuangalia utendaji na ufanisi wa Redio zetu za Mkoa wa Kagera mwanadisi wa makala haya aliongea na Katibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Kagera (KPC) Bw. Phinias Bashaya amabaye alisema kuwa Redio  za Mkoa wa Kagera zimekuwa mkombozi kwa mwananchi wa kawaida tena wa kijijini kwani kupitia redio hizo wananchi wameweza kupaza sauti zao na wanasikika jambo ambalo hawakuwahi kulitarajia katika miaka ya 1990.

Bw. Bashaya  Mwandishi Nguli anayeandikia Gazeti la Mwananchi alitoa ushari wake kwa Wamiliki wa Vituo vya Redio Mkoani kagera , Wahariri na Waandaji wa vipindi vya Redio kuzipa zaidi vipaumbele habari za wananchi ambapo alitoa mfano kuhusu Bomba la Mafuta linatoka nchini Uganda na kupita mkoani Kagera,  kuwa wananchi wanatakiwa kuelimishwa juu ya fursa hiyo kupitia redio zetu za jamii.

“Tunapoadhimisha Siku ya Redio Duniani nawakumbusha wenzangu wandaaji wa vipindi kuangalia kwa jicho la tatu suala la utamaduni wetu, mfano naona redio zetu hazijajikita zaidi kuelimisha hasa vijana kuhusu utamaduni wa mwananchi wa Mkoa wa Kagera ili kulinda maadili ya Wanakagera. Mfano vijana wa leo wanatakiwa kujua wazee wetu walifanya nini wakati wa kuchumbia wake zao. Vipindi hivi ni vichache au wakati mwingine havisikiki kabisa, ningependa navyo vipewe kipaumbele pia,” Alisistiza Bw. Bashaya.

Aidha, Bw. Bashaya alitoa ushauri kuwa pamoja na Redioza Kagera  kurusha vipindi vizuri lakini vituo hivyo vipunguze kurusha habari ambazo tayari zimerushwa na vyombo vya Kimataifa badala yake redio zetu zijikite katika habari za wananchi kwani Redio za kimataifa zinapenda kurusha habari mbaya tu lakini habari zetu nzuri hazirushwi kwahiyo redio zetu ziwe chachu ya kutangaza habari nzuri kwa wananchi wake.

Kwa upande mwingine Mkurugenzi wa Redio Kwizera FM Padri Damas Missanga aliwashauri wamiliki wa Vituo vya Redio Mkoani Kagera Kuhakikisha wanapata wawakilishi wa vituo vyao kila eneo ili kupata habari za wananchi. Alisistiza kuwa wananchi wanapenda kusikia habari zao wenyewe kuliko habari za kutokea sehemu nyingine.

Ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres  kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Redioa Duniani. Redio inawafikia watu wengi Duniani, Katika kipindi cha maendeleo makubwa katika mawasiliano, redio ina nguvu za kuburudisha, kuelimisha, kujulisha na kuhamasisha. Redio inao uwezo wa kuziunganisha na kuziwezesha jamii pia kutoa sauti kwa waliopotea.

Mwaka 2018 na Michezo ya Olimpiki ya Majira ya baridi sasa inaendelea, tunaweza pia kutambua njia nyingi ambazo utangazaji wa michezo huleta watu pamoja, karibu na msisimko na mafanikio. Siku ya Radio Duniani, hebu tufurahie redio na michezo kama njia ya kuwasaidia watu kufikia mafanikio yao kwa ujumla.

 


 

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa