• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Mkoa wa Kagera Wazindu Mkakati wa Nyumba Kumi Bora za Kiusalama Kukomesha Mauaji Uhalifu Magendo na Uhamiaji Haramu

Imewekwa : November 2nd, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti azindua rasmi mkakati wa kuimarisha usalama katika Mkoa wa Kagera uliopewa jina la “Nyumba Kumi Bora za Kiusalama”. Mkakati huo ukilenga kuimarsha Ulinzi na Usalama wa mkoa kuanzia ngazi ya chini katika jamii kwa kila nyumba kumi kuwa na kiongozi ambaye atakuwa na jukumu la kutambua wanafamilia wanaoishi katika kila nyumba anayoiongoza.

Mkuu wa Mkoa Gaguti ambaye ni Mhasisi na Mwanzilishi wa Mkakati huo wa kukomesha uhalifu, ujambazi na vitendo vya uvunjifu wa amani katika Mkoa wa Kagera alizindua Mkakati huo kimkoa wa “Nyumba Kumi Bora za Kiusalama” wenye kaulimbiu isemayo: 10 Bora! Usalama wa Nchi, katika Kijiji cha Chabuhola Kata Nyakabanga Tarafa Nyakakika Wilayani Karagwe Novemba 1, 2018.

Akitoa ufafanuzi namna mkakati wa  “Nyumba Kumi Bora za Kiusalama” utakavyofanya kazi Mkuu wa Mkoa Gaguti aliwaeleza wananchi waliofurika katika hafla fupi ya uzinduzi kijijini Chabuhora Wilayani Karagwe kuwa Mkoa wa Kagera bado haufanyi vizuri  katika suala la ulinzi na usalama hasa watendaji wa Serikali katika ngazi za chini hawawajibiki ipasavyo katika kutekeleza majukumu yao katika suala zima la kiulinzi.

“Katika Mkoa wetu wa Kagera bado tuna changamoto kubwa ya kiusalama hadi kufikia mwezi Septemba 2018 Mkoa ulikuwa na kesi za mauji 107, katika Kata hii tu tuliyopo hapa sasa ya Nyakabanga kufikia Septemba 2018 kulikuwa kumebainika wahamiaji haramu 997 na bado tunalo tatizo la magendo. Haya mambo makuu matatu yanonesha vyema kuwa bado tuna changamoto kubwa ya Kiusalama katika Mkoa”. Alieleza Mkuu wa Mkoa Gaguti.

Mkuu wa Mkoa Gaguti alisema kuwa inashangaza sana kuona Mkoa wa Kagera wenye wasomi wengi na bado ni Mkoa unaoendelea kufanya vizuri katika Sekta Elimu lakini bado wananchi wake wanashiriki katika imani potofu na kupelekea kushiriki katika vitendo vya mauaji na kuifanya Kagera kuwa kati ya Mikoa ambayo inaongoza kwa vitendo vya mauaji.

Jukumu la Ulinzi na Usalama si jukumu la Vyombo vya Ulinzi na Usalama tu bali ni jukumu la kila mwananchi kulinda usalama wake mwenyewe na Usalama wa nchi na jukumu la Vyombo vya Ulinzi na Usalama ni kuongoza katika juhudi za kiulinzi na kiusalama pale panapotokea uvunjifu wa amani. Mwananchi mmoja mmoja anatakiwa kulinda usalama popote pale anapokuwa katika nchi ya Tanzania.

Mkuu wa Mkoa Gaguti alisema kuwa Mkoa wa Kagera unatakiwa kuwa mbele sana katika suala la kiusalama kwani unapakana na nchi jirani nne kati ya nchi nane zinazopakana na nchi ya Tanzania. “Mtu akiingilia hapa Nyakabanga anajifanya mwenyeji na mwisho wa siku anatupigia bao Dodoma katikati ya nchi akishafika huko anajifanya ametokea Chabuhora Nyakabanga Karagwe kumbe mhamiaji Haramu.” Alifafanua Mhe. Gaguti.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Karagwe Bw. Godfrey Mheluka akito taarifa kwa Mkuu wa Mkoa alisema baada ya Wilaya ya Karagwe kupewa heshima ya kuzindua Mkakati wa “Nyumba Kumi Bora za Kiusalama” uongozi wa Wilaya uliamua kufanya uzinduzi huo katika Kata ya Nyakabanga kwasababu kata hiyo inaongoza kwa mauaji na wahamiaji haramu kutoka nchi jirani na mkakati huo ulizinduliwa hapo kuanza kukomesha vitendo hivyo.

Namna Mkakati wa Nyumba Kumi Bora za Usalama Utakavyofanya Kazi.

Kila Kijiji zinatengwa nyumba kumi kumi na kila nyumba kumi anachaguliwa kiongozi mmoja ambaye anajua kusoma na kuadika. Kila nyumba au kaya wanaorodheshwa wanafamilia wanaoishi katika nyumba hiyo na kunakuwa na orodha ya kila nyumba kwa nyumba zote kumi.

Majukumu ya Kiongozi ni kuhakikisha katika nyumba zake kumi hakuna mgeni anayeingia au kuishi bila kuwa na taarifa za mtu huyo ametokea wapi au amekuja kufanya nini katika eneo hilo. Jukumu la mwananchi ni kutoa taarifa kwa Kiongozi wa Nyumba Kumi za Kiusalama apatapo wageni na taarifa za muhimu za mgeni huyo ili kuzuia uvunjaji wa amani kwa watu wasiojulikana wanatokea wapi au wamekuja kufanya nini.

Aidha, katika kuzuia wizi wa mifugo wananchi watatakiwa kutoa taarifa kwa Kiongozi wao pale wanapotaka kuchinja mbuzi au ngombe kwaajili ya kuuza au kitoweo cha nyumbani katika familia zao ili Kiongozi ahahkikishe kuwa mnyama huyo si wa wizi

Viongozi wa Nyumba Kumi za Kiusalama wanapewa mihuli iliyo na namba ziatakazotofautisha Vijiji na Kata ambapo wataruhusiwa kuandika barua za kuwatambua wakazi wao na kuwatolea taarifa mbalimbali kwa viongozi wao wa juu. Wasimamizi wakuu wa viongozi wa Nyumba Kumi Bora za Kiusalama ni Watendaji wa Vijiji pamoja na Watendaji wa Kata.

Kila Nyumba Kumi za KIusalama wananchi na kiongozi wao watatakiwa kufanya mikutano ya kujadili ulinzi na usalama kila mwezi na kuandaa taarifa na kuiwasilisha kwa mtendaji wa Kijiji ambapo naye ataunganisha taarifa hizo na kuziwasilisha kwa Afisa Mtendaji wa Kata. Taarifa hizo zitaenda mpaka ngazi ya Wilaya hadi Mkoa ili kama kuna changamoto kubwa ya kiusalama ifanyiwe kazi kwa wakati.

Katika hafla hiyo fupi ya uzinduzi wa Nyumba Kumi Bora za Kiusalama zilitolewa mada kuhusu Urai kutoka Ofisi ya Kamanda wa Uhamiaji Mkoa, Usalama wa Raia kutoka kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera . Aidha, uzinduzi huo ulihudhuriwa na Wakuu wa Wilaya zote za Mkoa wa Kagera. Kuwa kiongozi wa Nyumba Kumi Bora za Kiusalama si ajira ya kulipwa mshahara wala posho bali ni uzalendo wa mwananchi mwenyewe kushiriki katika kulinda usalama wan chi.

Nao wananchi wa Kata ya Nyakabanga walifurahi na kupokea mkakati huo kwa mikono miwili ambapo walisema kuwa sasa huo unakwenda kuwa mwarobaini wa kukomesha uhalifu, mauaji na magendo. “Wahamiaji haramu wanakuja hapa wanafanya matendo maovu kama mauaji alafu tunaonekana ni sisi wakazi wa hapa kumbe siyo sasa huu mpango wa Nyumba Kumi Bora za Kiusalama utatusaidia sana katika kuwatambua haraka na tunamshukuru Mkuu wa Mkoa.” Alieleza Bw. Amosi Balikweba.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa