• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Dk. Magdalena Akitoa Maelzo ya Maharage Lishe Mbele ya Mkuu wa Mkoa na Mwakilishi wa FAO Katika Shamba la Viazi Lishe Maruku Chuo cha Utafiti wa Kilimo

Imewekwa : January 25th, 2018

Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa Tanzania Aridhishwa na Ufanisi wa Mradi wa Kusaidia Waathirika wa Tetemeko Mkoani Kagera

Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) nchini Tanzania Bw.Fred Kafeero afanya ziara ya siku tatu Mkoani Kagera kuona shughuli za mradi wa kusaidia kaya 5000 katika Halmashauri za Bukoba, Bukoba Manispaa, Kyerwa Missenyi na Muleba zilizoathiriwa na Tetemeko la Ardhi Septemba 10, 2016.

Baada ya Tetemeko la Ardhi Septemba 10, 2016 Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) lilitoa msaada wa mbegu za mazao mbalimbali yanayovumilia ukame kama mihogo, viazi lishe, mahindi ya muda mfupi na migomba inayovumilia magonjwa, mbuzi wa maziwa, ufuaji wa kuku na ufugaji wa samaki ili kuzikomboa familia hizo 5000 na baa la njaa na kuinua kipato kwa ngazi ya familia.

Bw. Kafeero akiwa mkoni hapa na kutembelea baadhi ya kaya zinazonufaika na mradi FAO alisema kuwa ameridhishwa na ufanisi wa mradi huo katika kaya hizo ambapo mafanikio yanajionesha yenyewe kwa wanakaya hao kunufaika na mbegu ambapo mashamba yapo, ufugaji wa kuku na samaki unaendelea vizuri.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu akiambatana na Bw.Fred Kafeero katika ziara hiyo alimhakikishia Mwakilishi Mkazi huyo kuwa mkoa unafanya ufuatiliaji wa karibu sana kwa kaya 5000 zilizonufaika na mradi ili kuhakikisha zinakuza kipato kupitia mradi kwa kupata chakula pamoja na ziada ya kuuza na kupata kipato cha fedha.

Aidha, Mhe. Kijuu aliendelea kuwasisitiza wananchi wanaonufaika na mradi wa FAO kuhakikisha wanafanyakazi kwa kujituma ili mradi unapomalizika mwaka 2019 wawe wameweza kujikomboa katika shida za chakula pamoja na kipato pia kuiendeleza miradi yao wenyewe bila kutegemea Shirika la Umoja wa Mataifa.

Kwa ujumla Mradi FAO umeongeza uzalishaji wa chakula, umeongeza kipato kwa wananchi na kupunguza umasikini, umeboresha lishe kupitia maharage ya lishe (yenye madini ya chuma na zinki na protini) na viazi lishe vyenye vitamin A. Pia radi umeongeza uzalishaji na upatikanaji wa mbegu bora wa mazao yanayovumilia ukame na magonjwa.

Aidha, mradi umekua kiunganishi kati ya watafiti na wakulima kwenye teknolojia ya kilimo (Research Extension Farmer Linkage) kwa njia ya mafunzo kupitia Mashamba darasa (Farmer Field Schools FFS). Mradi tayari umetoa msaada wa mafunzo kwa kaya 2500 kuanzia Julai 2017 hadi sasa. Pia Bw. Kafeero baada ya kufurahishwa na kilimo kizuri cha mihogo aliwahaidi wakulima katika kijiji cha Nsambya kuwanunulia mashine ya kuchakata mihogo.

Aidha, gharama za mradi hadi Februari 2019 utakapokuwa umekamilika ni takribani Shilingi Milioni 700 Ziara ya Bw. Kafeero Mkoani Kagera ni ya siku tatu kuanzia tarehe 23 hadi 25 Januari, 2018.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa