• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Kijuu (Katikati) Akikagua Majengo ya Kituo cha Afya Nyakayanja Wilayani Karagwe

Imewekwa : February 7th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Akagua Miradi ya Afya Kuona Shilingi Bilioni 3.5 Fedha za Serikali Zinatumika Kama Ilivyokusudiwa

Mkuu wa Mkoa Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu afanya ziara katika Halmashauri za Wilaya nane   kukagua matumizi ya shilingi bilioni 3.5 fedha zilizotolewa na Serikali  kukarabati baadhi ya Vituo vya Afya Mkoani Kagera pia  kuwahamasisha wananchi kuendelea kuchangia gharama za ujenzi wa Zahanati na Vituo vya Afya ambavyo havijakamilika katika maeneo yao kwa kushirikiana na Serikali.

Akiongea  na wananchi katika Kituo cha Afya Nyakanazi  Wilayani Biharamulo Mkuu wa Mkoa Kijuu alisema kuwa alifika  kituoni hapo pamoja na Vituo vingine vya Afya ambavyo vimepewa fedha na Serikali ili vikarabatiwe ili ajionee kama fedha hizo zinatumika ipasavyo ikiwa ni pamoja na michango ya wananchi  wa eneo husika na kuhakikisha ujenzi unakamilika ifikapo Machi 30, 2018.

Serikali imetoa kiasi cha shilingi bilioni 3.5 kwa vituo vinane katika Mkoa wa Kagera  ambapo awamu ya kwanza ilitolewa  shilingi milioni 500 kwa kila kituo Vituo vya Nyakanazi (Biharamulo) na Kayanga (Karagwe).  Awamu ya pili Serikali ilitoa  shilingi milioni 500 kituo cha Katoro (Bukoba) na  Vituo vya Kishanje (Bukoba), Mabawe na Murusagamba (Ngara), Kimea (Muleba), na Murongo (Kyerwa) vilipewa shilingi milioni 400 kila kimoja.

Akitoa ufafanuzi Mkuu wa Mkoa Kijuu kwenye Mikutano ya hadhara na wananchi alipotembelea na kukagua ukarabati  wa Vituo vilivyopata fedha kutoka Serikalini alisema kuwa Vituo hivyo vilipata fedha katika awamu ya kwanza kutokana na juhudi za wananchi wenyewe katika maeneo husika kuonesha juhudi katika uchangiaji wa ujenzi wa Vituo vyao vya Afya.

Mkuu wa Mkoa Kijuu aliwahamasisha wananchi katika maeneo mengine ambayo vituo vyao havijapata fedha kutoka Serikalini kuendelea kuchaangia ujenzi wa Vituo na Zahanati ili majengo na miundombinu yote inayotakiwa ikamilike, kupitia juhudi hizo za wananchi Serikali pia itaweza kuchangia fedha kwa maeneo yale ambayo wananchi wataonesha juhudi za kuchangia maendeleo yao.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa alisistiza mambo makuu manne kama ifuatavyo, Kwanza, Vituo vya Afya vilivyopata fedha za Serikali zitumike kwa kusimamiwa na Kamati za Vituo pia watumike mafundi wa eneo husika bila kuwatumia Wakandarasi na Wakandarasi washauri katika ujenzi  ili kuepuka gharama kubwa za ujenzi aidha, ujezi uzingatie viwango kwa usimamizi wa Wahandisi wa Halmashauri.

Pili, Mkuu wa Mkoa aliwaagiza Wakurugenzi  Watendaji wa Halmashauri kuhakikisha wanatenga na kuyapima  maeneo ya Vituo vya Afya na Zahanati kwa manufaa ya upanuzi wa baadae na kuondoa migogoro na wananchi jirani. Tatu, wananchi wanatakiwa kuendelea kujishughulisha na kilimo ili kujipatia chakutosha na kuchangia maendeleo yao kama ujenzi wa Zahanati na Vituo vya Afya.

Nne, wananchi, Taasisi za Serikali na zisizokuwa za Serikali zinatakiwa kupanda miti ya matunda kuzunguka maeneo ya Taasisi hizo na wananchi  wapande miti ya matunda ya aina mbalimbali isiyopungua mitano kuzunguka kaya zao ili kupunguza tatizo la utapiamlo katika Mkoa wa Kagera ambalo linatokana na wananchi wa Kagera kutokula matunda na mchanganyiko sahihi wa vyakula.

Katika hatua nyingine kwenye ziara hiyo Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mganga Mkuu wa Mkoa Dk. Thomas Rutachunzibwa ambaye alipata fursa ya kuwaelimisha wananchi juu ya miundombinu inayotakiwa katika Vituo vya Afya na Zahanati ambapo ili kituo cha Afya kiitwe Kituo cha Afya kinatakiwa kuwa na miundombinu ifuatayo:

Kituo cha Afya kilichokamilika na kuruhusiwa kutoa huduma kwa wananchi kinatakiwa kuwa na Jengo la Wagonjwa nje na wagonjwa wa ndani, Jengo la Maabara, Wodi ya akinamama, Jengo la upasuaji, Wodi nyingine za wagonjwa, Vyoo vya watumishi na wagonjwa, Nyumba za watumishi wawili, Kichomea taka, Maji ya kutosha, Nishati ya umeme na Nyumba ya kuhifadhia maiti.

Dk. Rutachunzibwa aliwakumbusha wananchi katika ziara hiyo ya Mkuu wa Mkoa kuwa kwa sasa Serikali imetoa ramani ya ujenzi wa Vituo vya Afya na Zahanati ambapo wananchi wanatakiwa kuzingatia ramani hizo wakati wa ujenzi ili majengo ya kutolea huduma za afya yakidhi viwango.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa