• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Bw. Fred Kafeero Mwakilishi wa (FAO) nchini Tanzania Akitoa Hotuba Wakati wa Uzinduzi wa Kurejesha Hali za Wananchi Baada ya Tetemeko

Imewekwa : May 11th, 2017

Kaya Elfu Tano za Kagera Kunufaika na Mradi wa Kilimo na Ufugaji Ili Kurejesha Hali zao Katika Maisha ya Kawaida Baada ya Tetemeko

Kaya elfu tano (5000) za wananchi wa Mkoa wa Kagera zilizoathirika na Tetemeko la ardhi lililotokea mwaka jana Septemba 10, 2016 zatarajia kunufaika na mradi wa miaka miwili wenye thamani ya zaidi shilingi milioni 600 kupitia kilimo na ufugaji chini ya ufadhili wa Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO).

Mradi huo wa kurejesha hali za wananchi baada ya tetemeko chini ya ufadhili wa (FAO) ulizinduliwa rasmi Mkoani Kagera Mei 5, 2017 na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu pamoja na Mwakilishi wa (FAO) nchini Tanzania Bw. Fred Kafeero ikiwemo na wadau ambako mradi utatekelezwa.

Malengo ya mradi ni kuvisaidia vikundi vya wakulima hasa vijana na akina mama kupitia mfumo wa mashamba darasa na stadi za maisha. Kuwajengea uwezo wa matumizi ya mbinu na teknolojia zinazokabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ili kuongeza uzalishaji na kupunguza upotevu wa mazao kwa kulinda rasilimali ardhi na misitu.

Aidha, kuimarisha kilimo kinachozingatia lishe bora ili kupunguza utapiamlo hasa kwa wtoto wadogo na  kuwaelimisha wakulima na wafugaji namna bora ya kupata masoko ya mazao yao ili kujiongezea kipato.

Mwakilishi wa (FAO) nchini Tanzania Bw. Fred Kafeero alisema kuwa mradi huo utatekelezwa kwa kutumia raslimali zilizopo siyo kwamba utatekelezwa kama mradi mpya. “Tunalenga kutumia raslimali na njia ambazo tayari zilikuwepo awali mfano kutumia vikundi vya vijana na wakulima au wafugaji ambao tayari wapo ili kutekeleza mradi huu.” Alisistiza Bw. Kafeero

Bw. Kafeero alisema  kuwa mradi huo umekuja Kagera baada ya yeye kutembelea mkoani hapa mwaka jana Oktoba 16, 2017 akiwa na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Charles Tizeba na kujionea hali ya ukame wa muda mrefu na madhara ya tetemeko jinsi vilivyoathiri uzalishaji wa chakula hasa zao la ndizi na kupelekea wananchi kukosa chakula na kipato kutokana na kutopata mavuno ya kutosha.

Katika ripoti ya utafiti wa Afya ya mwaka 2015/16 mkoa wa Kagera ulikuwa na asilimia 41.7% ya udumavu na kiwango kikubwa cha upungufu wa damu mwilini kwa watoto asilimia 39.1%  na akinamama asilimia 57.2% jambo ambalo lilionekana kuathiri matumizi ya lishe bora kwa ngazi ya kaya na kupelekea utapiamlo kwa watoto.  Pia majanga ya asili na ukosefu wa ujuzi katika kilimo kwa wakulima wadogo ni changamoto kubwa katika uzalishaji wa chakula na lishe bora kwa wananchi.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Kijuu alilishukuru Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO)kupitia mwakilishi wake nchini Bw. Fred Kafeero kuleta mradi huo kwa wananchi wa Kagera hasa baada ya kupata majanga ya ukame na tetemeko. “Kwaniaba ya wananchi wangu nawashukuru sana kwani mradi huu utakuwa faraja kwa wananchi hasa baada ya kupata majanga ya asili.” Alisistiza Mhe. Kijuu.

Mkuu huyo wa Mkoa alitumia fursa hiyo kuwaagiza Watendaji na watekelezaji wa mradi huo kuhakikisha wantekeleza mradi huo kwa ufanisi mkubwa ambapo alisema kuwa Serikali imekuwa ikitekeleza miradi mingi lakini mwisho wa miradi hiyo hakuna tija kama inavyokuwa imetarajiwa hapo awali. Alisistiza kuona matokeo mazuri katika jamii na wananchi wenyewe mradi utakakokuwa unatekelezwa.

Mradi wa kurejesha hali za wananchi baada ya Tetemeko Kagera ambao utafadhiliwa na Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) utatekelezwa katika Halmashauri za Wilaya za  tano ambazo ni Muleba, Kyerwa, Missenyi, Bukoba na Bukoba Manispaa.

Watekelezaji wakuu wa mradi huo ni Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kama mtekelezaji mkuu wa mradi kwaniaba ya Serikali, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera  kama msimamizi wa karibu wa mradi, Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) wafadhili wa mradi, na Halimashauri za Wilaya ambazo ndiyo wanaohusika moja kwa moja katika kutekeleza mradi huo.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa