• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Ng'ombe Ambaye Tayari Amepigwa Chapa Kama Utambulisho Katika Halmashauri ya Wilaya Bukoba

Imewekwa : November 4th, 2017

Waziri Luaga Mpina Ahamasisha Wafugaji Kagera  Ng’ombe Wao Kupigwa Chapa Kukomesha Uingizwaji wa Mifugo Toka Nje.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luaga Mpina afanya ziara ya siku mbili Mkoani Kagera kuhamasisha kasi ya upigaji chapa wa ng’ombe ili kutambua idadi ya mifugo hiyo ikiwa ni pamoja na  kukomesha wizi  wa ng’ombe pia na kukomesha uingizwaji wa ng’ombe hao  nchini kutoka nchi za  jirani.

Akiwa Mkoani hapa Waziri Mpina alishiriki katika zoezi la kupiga chapa ng’ombe katika Wilaya ya Bukoba Kijijini Kyema Kata Katerero ambapo mara baada ya kushiriki zoezi hilo akiongea na wafugaji walioleta ng’ombe wao kupigwa chapa katika zoezi hilo alisema,

“Lengo kuu la kupiga chapa ng’ombe ni  kuzuia wizi wa ng’ombe, kupata takwimu halisi za ng’ombe nchini ili kuisaidia Serikali kuweka mipango sahihi ya uendelezaji wa ufugaji nchini. Lakini pia kuhakikisha ng’ombe wa Tanzania wanakuwa na alama ambapo itasaidia kutambua ng’ombe kutoka nchi jirani wanaoingizwa kulishwa nchini kwetu. Aidha zoezi la kupiga chapa ng’ombe ni la nchi nzima ambapo mwisho wa zoezi hilo utakuwa tarehe 31.12.2017” Alisistiza Waziri Mpina.

Pia Waziri Mpina akiwa Mkoani Kagera alizitembelea Ranchi za Missenyi na Pori la Akiba la Burigi na kujionea jinsi mifugo kutoka nchi jirani ilivyoondolewa kutoka katika mapori hayo. Pia alishuhudia ng’ombe zaidi ya 6000 walioingizwa katika mapori hayo  kutoka nchi jirani waliokatawa mara baada ya Operesheni Ondoa Mifugo Kagera na kuagiza ng’ombe hao kupigwa mnada mara moja.

Waziri Luaga mpina katika ziara yake ya siku mbili Kagera alitembelea pia kiwanda cha kusindika minofu ya Samaki cha SUPREME PERCH kilichopo eneo la Nyamkazi Manispaa ya Bukoba ambapo uongozi wa kiwanda hicho ukitoa taarifa ulisema kuwa hadi sasa kiwanda hicho kina uwezo wa kusindika tani 60 za minofu ya samaki lakinikwasasa kinasindika tani 17 tu kutokana na uhaba wa Samaki.

Mara baada ya kupokea taarifa hiyo Waziri Mpina aliuagiza uongozi wa kiwanda hicho kuhakikisha ndani ya mwaka mmoja ujao kiwe kimefikia  angalau uzalishaji wa tani 25 na kufikia mwaka 2020 kizalishe tani zote 60 kwani Serikali inakwenda kuhakikisha inakomesha vitendo vyote vya uvuvi haramu katika Ziwa Victoria.

Vilevile Waziri mpina alitembelea shamba la mabwawa ya kufuga samaki katika eneo la Luhanga  Wilayani Muleba na kujionea ufugaji wa samaki wa kisasa na ambapo alisema kuwa Serikali itaendelea kuhamasisha wananchi kufuga samaki katika mabwawa ili kutoa nafasi ya kupumzisha ziwa ili samaki wazaliane kwa wingi.

Mwisho Waziri Luaga Mpina aliupongeza uongozi wa Mkoa wa Kagera kwa kufanya operesheni ondoa mifugo Kagera na kuhakikisha Ng’ombe wote kutoka nje ya nchi wameondolewa katika Mapori ya Akiba na hifadhi za Taifa. Waziri Mpina alifanya ziara ya siku mbili kuanzia tarehe  1 hadi 2 Novenba, 2017 na kumalizia ziara yake Wilayani Biharamulo ambapo aliondoka kuelekea Mkoani Kigoma.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa