• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Shughuli za Mahakama Mkoani Kagera Zafunguliwa Rasmi Mwaka 2019 Kesi ya Mauaji ya Mwanafunzi Spelius Eradius Yasikilizwa Kwa Mara ya Kwanza

Imewekwa : February 6th, 2019

Mkoa wa Kagera katika kuadhimisha kilele cha wiki ya Sheria Februari 6, 2019 Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Bukoba chini ya Jaji Mfawidhi Lameck M. Mlacha imeweza kusikiliza kwa mara ya kwanza kesi Namba 56 ya mwaka 2018 ya Mwalimu Respikius Patrick Mtazangira na Mwalimu Erieth Gerald dhidi ya mauaji ya Mwanafunzi marehemu Spelius Eradius wa Kibeta Shule ya Msingi Manispaa ya Bukoba aliyepigwa hadi kupelekea mauti ya kifo chake tarehe 27.08.2018

Katika shauri hilo upande wa Jamhuri uliwakilishwa na Wakili Msomi Chema Maswi Kaimu Mwendesha Mashitaka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambapo aliwasilisha mashahidi saba kutoa ushahidi katika shauri hilo. Shahidi wa kwanza Bw. Benius Benezeth ambaye ni dereva bodaboda aliyembeba Mwalimu Erieth Gerald siku ya tukio alitoa ushahidi mbele ya Mahakama jinsi alivyombeba mwalimu huyo na kumfikisha shuleni Kibeta na kupokelewa mizigo na wanafunzi.

Baada ya kutoa ushahidi mbele ya Mahakama shahidi wa kwanza Bw. Benius Benezeth na kuhojiwa na pande zote mbili upande wa Jamhuri  na upande wa utetezi Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba Lameck M. Mlacha alihairisha kesi hiyo hadi tarehe 8.02.2019 ambapo mashahidi wengine sita wataendelea kutoa ushahidi wao mbele ya Mahakama.

Kesi hiyo namba 56 ya mwaka 2018 ilisikilizwa mara baada ya hafla fupi ya ufunguzi wa mwaka mpya wa shuguli za Mahakama kumalizika katika viwanja vya Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Bukoba ambapo wananchi na wageni waalikwa waliruhusiwa kuhudhuria na kusikiliza kikao hicho cha Mahakama Kuu kilichoashiria kuwa sasa shughuli za Mahakama Mkoani Kagera zimefunguliwa rasmi.

Kabla ya kikao hicho cha Mahakama Kuu Jaji Mfawidhi Lameck M. Mlacha akitoa hotuba yake mbele ya wageni waalikwa alisema kuwa maana ya kuadhimisha kilele cha maadhimisho ya wiki ya Sheria kwanza ni kiashiria cha kuanza rasmi kwa shughuli za Mahakama, Pili ni kuomba dua ili haki itendeke kwa wananchi Mahakamani, na tatu ni kufanya tathimini ya utendajikazi wa Mahakama kwa kipindi kilichopita na kujisahihisha.

Akiwapongeza baadhi ya wadau wa Mahakama Jaji Mfawidhi Lameck M. Mlacha alilipongeza Jeshi la Polisi kwa kutekeleza majukumu yake kwa wakati akitolea mfano wa upelelezi wa kesi ya mauaji ya Mwanafunzi Marehemu Spelius Eradius wa Shule ya Msingi Kibeta aliyefikwa na Mauti baada ya kupigwa na Mwalimu Respikius Patrick Mtazangira kufanyika kwa weledi na kwa wakati jambo ambalo lilipelekea kesi kufikishwa mahakani kwa wakati.

Onyo, Jaji Mfawidhi Mlacha alitoa onyo kwa baadhi ya Mahakimu Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi, na baadhi ya Makarani katika Mahakama ambao bado wanajihusisha na kupokea au kushawishi kupewa rushwa kuwa wakigundulika watachukuliwa hatua kali kwani zama hizi si zile walizozizoea vinginevyo wabadili mienendo ya tabia hizo mara moja na kutenda haki kwa wananchi.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Elisha Gaguti akitoa salamu za Serikali katika hafla hiyo aliipongeza Mahakama kwa kudumisha utamaduni wa kuadhimisha Wiki ya Sheria tena kwa kutoa msaada wa kisheria na elimu kwa wananchi na baadhi ya makundi mbalimbali ili yaweze kuelewa vizuri namna ya kutafuta haki Mahakamani.

Mkuu wa Mkoa Gaguti alisema kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na Mahakama kupitia vyombo mbalimbali ambavyo vipo chini ya Serikali kukomesha Wanasheria na Mawakili Vishoka wanaowarubuni wananchi na kufanya kazi za kisheria bila weledi wa kutosha na kuwafanya wananchi kuendelea kupoteza muda mwingi Mahakani bila sababu.

“Kila mmoja hapa anajua kuwa Mkoa wa Kagera una wasomi wengi hasa Maprofesa lakini nasikitika sana kusema kuwa wakati mwingine wasomi hao wamekuwa kichocheo cha wananchi kushinda Mahakamani wakati mwingine hata kama mwananchi huyo hana haki lakini analazimika kuendelea kufuatilia kesi kisa tu ana ndugu ambaye ni Profesa.” Alifafanua Mkuu wa Mkoa Gaguti.

Aidha Mkuu wa Mkoa Gaguti alitoa onyo kwa wananchi wanaojichukulia sheria mikononi katika Mkoa wa Kagera kuacha tabia hiyo kwani vitendo hivyo vinaupa mkoa sifa mbaya kama ilivyokuwa katika ujambazi wa kutumia siraha. Alisisitiza kuwa hapo nyuma Mkoa wa Kagera ulisifika kwa matendo ya ujambazi lakini Serikali ilikomesha vitendo hivyo na sasa Kagera ipo katika mikoa inayofanya vibaya katika kujichukulia sheria mikononi.

Akihitimisha Salamu za Serikali Mkuu wa Mkoa Gaguti aliwaomba Viongozi wa dini kuendelea kuhubiri amani, uvumilivu na upendo kwa waamini wa madhehebu yote ili wananchi waache vitendo viovu na kumrudia Mwenyezi Mungu jambo ambalo litapunguza kesi Mahakamani na kuwafanya wananchi kutumia muda mwingi kuzalisha na kufanya kazi za kujiingizia kipato.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa