• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Sipo Tayari Kuona Magendo ya Sukari Inaendelea Katika Mkoa wa Kagera Wakati Tunazalisha Sukari Katika Mkoa Wetu – RC Gaguti

Imewekwa : September 19th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti atembelea kiwanda cha Kagera Sukari kilichoko Wilayani Missenyi na kuhaidi kushughulikia masuala makuu matatu ambayo yanasababisha kiwanda hicho kuzalisha sukari ya kutosha lakini kwasasa inakosa soko kutokana na sukari kutoka nje ya nchi kuingizwa kimagendo katika masoko ndani ya nchi.

Akiwa kiwandani hapo Septemba 18, 2018 lengo likiwa ni  kutembelea kiwanda hicho na kuona changamoto ambazo zinasababisha sukari kukwama kwenda sokoni Mkuu wa Mkoa Gaguti baada ya kupokea taarifa ya kiwanda hicho iliyowasilishwa kwake na Meneja Mkuu wa Kiwanda Bw. Ashwin Rana alibainisha mambo makuu matatu ambayo alisema kuwa atayafanyia kazi ili kutatua changamoto ya sukari ya magendo kutoka nje ya nchi.

Kwanza, Magendo ya Sukari kutoka nje ya nchi, Mkuu wa Mkoa Gaguti akilitolea ufafanuzi suala hilo alisema kuwa hayupo tayari kuona suala hilo linaendelea katika Mkoa wa Kagera na atahakikisha anakomesha magendo ya sukari kwa njia yoyote ile ili kulinda soko la kiwanda cha Sukari Kagera. “Kwa kutumia Vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na wananchi tutahakikisha suala hilo linakomeshwa mara moja.” Alifafanua Mkuu wa Mkoa Gaguti.

Pili, Mkuu wa Mkoa Gaguti ili kutatua kero ya sukari kutoka Kiwanda cha Sukari Kagera kukosa soko na kupelekea kiwanda hicho kuwa na shehena kubwa ya sukari ambayo haitoki alitoa ushauri kwa uongozi na menejimenti ya kiwanda hicho kuangalia upya mfumo wao wa usambazaji wa sukari katika masoko kuwa rafiki kwa wafanyabiashara  na usiokuwa na mashariti magumu sana ili kuhakikisha sukari inasambaa kila kona kudhibiti sukari ya magendo kutoka nje ya nchi katika soko la ndani.

Tatu, Mkuu wa Mkoa Gaguti aliushauri pia Uongozi na Menejimenti ya kiwanda  cha Kagera kuangalia bei ya sukari yao  katika masoko ili kuendana na bei ya viwanda vingine vya nchini kiushindani jambo ambalo litapunguza ushindani wa wafanyabiashara wasiokuwa waaminifu kuingiza sukari ya magendo kutoka nje ya nchi au kuagiza sukari kutoka katika viwanda vya mikoa mingine wakati Kagera kunzalishwa sukari ya kutosha.

“Hivi karibuni natarajia kukutana na Wakuu wa Mkioa ya Kanda ya Ziwa Mkoani Shinyanga katika mambo muhimu nitakayozungumza nao mojawapo ni suala la kudhibiti magendo ya sukari na kuona namna bora ya kuhakikisha kiwanda cha Sukari Kagera kinasambaza sukari katika mikoa hiyo na kuweka mikakati endelevu ya kuvilinda viwanda vyetu vya ndani maana nimejionea shehena ya suakari ilivyo hapa ni ya kutosha.” Alisisitiza Mkuu wa Mkoa Gaguti

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa Gaguti alipongeza juhudi za kiwanda hicho katika uwekezaji kwa kuweza kuzalisha hadi tani 75,000 za sukari kwa msimu wa mwaka 2017/2018 ulioishia mwezi Juni 2018. Pia alipongeza juhudi za kiwanda kuzalisha ajira 6,000 kwa wananchi wenye takribani familia 30,000. Aidha, alipongeza  huduma zinazotolewa pia kiwandani hapo kwa jamii mfano huduma za matibabu zinazotolewa bure kusaidia wafanyakazi na wananchi wanaozunguka kiwanda cha Sukari Kagera.

Kiwanda cha Sukari Kagera tangu kuanza uzalishaji wa sukari katika msimu wa mwaka huu 2018/2019 mwezi Julai tayari kimezalisha jumla ya tani 26,000 za sukari na matarajio ya uzalishaji kwa msimu mzima ni tani 84,000 za sukari. Aidha, tani 12,800 za sukari bado hazijaingia sokoni  na bado zipo katika kiwanda hicho kutokana na tatizo la sukari ya magendo katika masoko.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa