• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Taasisi ya Best Dialogue Yaendesha Mafunzo ya Siku Mbili Kuondoa Mkwamo wa Biashara na Uwekezaji Mkoni Kagera

Imewekwa : July 27th, 2018

Mradi wa Uimarishaji Mazingira ya Biashara Tanzania (BEST Dialogue) kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam pamoja na Chemba ya Wafanyabiashara, Wakulima na Wenye Viwanda Tanzania (TCCIA) waendesha mafunzo ya siku mbili kwa viongozi wa Serikali na Sekta Binafsi katika Mkoa wa Kagera  ili kujadili namna bora ya kuboresha mazingira ya biashara kwa ushirikiano wa Serikali na Wadau wa biashara.

Mafunzo hayo kwa kiasi kikubwa yalilenga hasa kujadili kwa pamoja namna nzuri ya kuweka Mazingira bora ya Biashara na Ushawishi wa Sekta Binafsi katika kutekeleza miradi mbalimbali katika Mkoa wa Kagera na Tanzania kwa ujumla ili lengo la maendeleo liweze kufikiwa kwa pamoja.

Katika mafunzo hayo Viongozi wa Serikali pamoja na Wadau mbalimbali walifundishwa juu ya mfumo wa ushawishi na majadiliano kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi  ambapo sekta hizo mbili zilikumbushwa kushirikiana na kujadiliana mara kwa mara katika kuhakikisha biashara zinafanyika vizuri katika mazingira wezeshi.

Akiwasilisha mada ya kuweka mazingira mazuri ya biashara Dkt. Swabiri Khalid kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alisema kuwa Sekta ya Umma inatakiwa kuweka mazingira mazuri ya biashara ili Sekta binafsi waweze kufanya biashara zao bila wasiwasi pia kama kuna changamoto zozote katika sekta hizo mbili ni vyema kukaa pamoja na kuzitatua changamoto hizo kwa pamaoja na uelewa wa mmoja.

Sekta ya Umma ambao ni Viogozi mbalimbali wa Serikali kwa kushirikiana na Sekta Binafsi katika mafunzo hayo walibainisha changamoto mbalimbali za kila Wilaya katika mkoa wa Kagera zinazokwamisha au kuweka mazingia yasiyokuwa rafiki katika biashara na kuweka mikakati ya kutatua changamoto hizo ili kuweka mazingira rafiki ya biashara.

Changamoto kubwa zilizobainishwa katika mafunzo hayo ni Sekta binafsi kuiona Sekta ya Umma kama adui yake badala ya kuiona rafiki na kushirikiana. Pili Wadau wa Sekta Binafsi walilalamikia kodi kuwa nyingi lakini Sekta ya Umma nao walilalamikia ukwepaji wa kodi kwa wafanyabiashara. Tatu, wafanyabiashara kutopendana na kushirikiana katika kutafuta fursa za biashara. Nne, migogoro mingi ya ardhi.

Katika kuweka mikakati ya kutatua changamoto hizo Sekta hizo mbili za Umma na Binafsi zinatakiwa kushirikiana kwa kufanya mikutano ya pamoja na kutafuta njia mbadala ya kutatua tatizo. Aidha, elimu kwa wafanyabiashara inatakiwa kutolewa ili waelimishwe juu ya biashara zao, fursa mpya pamoja na umuhimu wa kulipa kodi za Serikali.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Bw. CP Diwani Athuman akitoa rai katika mafunzo hayo aliwaasa washiriki wa mafunzo, watumishi wa umma na wafanyabiashara Mkoani Kagera kubadilika kimtazamo ili kuchangamkia fursa nyingi zilizopo. Pili CP Athumani alisisitiza kuzitangaza fursa za uwekezeji katika mkoa kwa nguvu zote hasa kwa kutumia njia mbalimbali zikiwemo Tovuti ya Mkoa na Halmashauri za Wilaya .

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu akifunga mafunzo hayo aliishukuru Taasisi ya BEST Dialogue kwa kuwezesha mafunzo kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi  na kusema kuwa mafunzo hayo yalichelewa sana kama yangelifanyika miaka miwili nyuma mkoa ungekuwa mbali kimaendeleo kwani wafanyabiashara wangekuwa wamechangamkia fursa bila vikwazo.

Mkuu wa Mkoa Kijuu aliziagiza Halmashauri zote za Wilaya Mkoani Kagera kufanya vikao vya kubainisha changamoto zinazoweka mkwamo wa mazingira mazuri ya biashara na kuzitafutia ufumbuzi Sekta ya Umma kwa kushirikiana na Sekta binafsi ili kuwa na uelewa wa pamoja.

Pia aliwaagiza  viongozi Chemba ya Wafanyabiashara, Wakulima na Wenye Viwanda  Tanzania (TCCIA) Mkoa wa Kagera kuandaa kikao cha wafanyabiashara Mkoani Kagera pamoja na Serikali ili kutatua changamoto mbalimbali zinazokwamisha biashara mkoani hapa.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa