• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Wanafunzi wa Shule za Msingi Mkoani Kagera Wakipita Mbele ya Mgeni Rasmi Katibu Tawala wa Mkoa Kagera CP Diwani Athuman Wakati wa Kufunga Mashindano ya UMISHUMITA

Imewekwa : June 12th, 2018

Kambi ya Umishumita Mkoani Kagera Yaaswa Kuchagua Vipaji Halali na Si Mamluki Ili Kuleta Ushindani Kitaifa – CP Athumani

Katibu Tawala Mkoa wa Kagera CP Diwani Athuman ambaye ni Mwekiti wa Michezo Mkoani Kagera afunga rasmi mashindano ya UMISHUMITA ya mkoa kwa kutoa rai kwa wakufunzi na Walimu wa michezo kuhakikisha wanafuata vigezo vilivyotolewa na Serikali kuunda timu bora isiyokuwa na mamluki  itakayoshiriki mashindano hayo ngazi ya Kitaifa na kuleta ushindi.

Katibu Tawala CP Athumani alitoa rai hiyo chuoni Katoke Wilayani Muleba kwenye kambi ya mashindano ya Mkoa yaliyohusisha  shule za Msingi kutoka Halmashauri za Wilaya za Mkoa wa Kagera  ambapo mara baada ya kushindanishwa katika michezo mbalimbali inatakiwa kuundwa timu moja kila mchezo itakyowakilisha Mkoa katika Mashindano ya Kitaifa Jijini Mwanza.

Rai hiyo ilitolewa na Katibu Tawala wa Mkoa Juni 10, 2018 baada ya Afisa Michezo Mkoa Bw. Kepha Elias kueleza kuwa katika kambi hiyo wanakumbana na changamoto kubwa ya baadhi ya Halmashauri za wilaya kutaka kwenda tofauti na maelekezo ya Serikali ya kuzingatia umri wa watoto wanatakiwa kushiriki mashindano hayo lakini pia kuwahusisha Mamluki Wasiokuwa walimu kuendesha mashindano ya michezo hiyo

“Ndugu mgeni Rasmi kuna baadhi ya Halmashauri za Wilaya zinaleta watoto wasio na vigezo vya kushiriki mashindano ambapo umri ni miaka 14 lakini shule kwa kushirikiana na walimu wanawaleta watoto waliozidi umri huo, pia wanashirikisha walimu mamluki yaani walimu wasiostahili kufundisha michezo na kuwahalalisha kushiriki katika zoezi hili tofauti na maelekezo ya Serikali.” Alisisitiza Bw. Kepaha

Katibu Tawala CP Athumani alisisitiza sana kuwa mkoa haupo tayari kufanya kinyume na maelekezo ya Serikali bali Maelekezo na miongozo itazingatiwa kwa kufauata vigezo vilivyopo na kama ikitokea maelekezo hayo yamekiukwa atakikisha anamchukulia hatua yeyote atakaekuwa amehusika kwa njia moja au nyingine.

MAAGIZO

Mwekiti huyo wa Michezo Mkoani Kagera CP Diwani Athumani alitumia fursa hizo kuziagiza Halmashauri za Wilaya kwanza kuahakikisha Maandalizi ya Michezo ya UMISHUMITA katika ngazi za Wilaya yafanyike mapema sana ili kuhakikisha katika Ngazi ya mkoa wanaletwa watoto wanamichezo wenye vipaji haswa.

Pili ni kuhusu michango ya fedha kwa ngazi ya Mkoa, Kila Halmashauri ya Wilaya ihakikishe inatoa michango yake mapema ili maandalizi kwa ngazi ya mkoa ifanyike mapema kuliko ilivyokuwa mwaka huu kwani fedha hizo zinatolewa na Serikali kwahiyo hamna sababu ya ucheleweshwaji kutoka katika Halmashauri za Wilaya.

Tatu Kila Halmshauri ya Wilaya kuhakikisha kila wiki ya pili ya mwezi inashiriki kikamilifu katika michezo ambapo wananchi wote na watumishi wanatakiwa kushiriki katika mazoezi ili kuweka miili yao sawa na kujikinga na magonjwa yanayosababishwa na kutoafanya mazoezi , aidha watoto nao washirikishwe kwani wakijengewa utamaduni huo wa kufanya mazoezi wakiwa wadogo watauzoe na kuwa sehemu ya maisha yao.

Mwisho Mkuu wa chuo cha Ualimu Katoke akiishukuru Serikali ya Mkoa kufanyia kambi ya Michezo kwa Watoto wa Sekondari na Shule za Msingi  chuoni hapo alisema michezo hiyo imewapa changamoto ya kurekebisha mitaala yao na masomo ya michezo kuyapa umuhimi ili walimu wanaohitimu katika chuo hicho waweze kwenda kuwafundisha watoto michezo shuleni.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa