• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Watumishi wa Sekta ya Afya Toeni Huduma Bora Kwa Wananchi Kama Ubora wa Majengo Unavyoonekana – RC Gaguti

Imewekwa : August 24th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti awataka watumishi wa Sekta ya Afya Mkoani Kagera kutoa huduma bora kwa wananchi kulingana na hadhi na ubora wa majengo yaliyojengwa ama kuboreshwa kwa fedha za Serikali kwa kiwango cha kuridhisha katika Vituo mbalimbali vya Afya  ili kuhakikisha huduma muhimu zinapatikana katika vituo hivyo hasa huduma za upasuaji kwa mama wajawazito.

“Nimeridhika na ubora wa majengo yaliyojengwa katika kituo hiki pamoja na thamani ya fedha inaonekana katika majengo haya, rai yangu kwenu watumishi wa Kituo hiki cha Afya na vituo vyote vilivyoboreshwa Mkoani Kagera ni kutoa huduma zinazofanana na majengo yalivyo, huduma safi kwa wananchi zenye kuwafariji wanapokuja kupata huduma za afya hapa.” Alisisitiza Mhe. Gaguti

Mkuu wa Mkoa Gaguti alitoa rai hiyo Augusti 24, 2018 katika Kituo cha Afya Kimeya Wilayani Muleba alipofanya ziara ya kujitambulisha katika Wilaya hiyo na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo ambapo alitembelea na kukagua ujenzi wa majengo matano yaliyogharimu kiasi cha shilingi milioni 456 zilizotolewa na Serikali pamoja na wananchi kuchangia kiasi cha shilingi milioni 11.7

Majengo yaliyojengwa ni pamoja na jengo la Mama na Mtoto, Jengo la Maabara, Nyumba moja ya Mtumishi, Jengo la upasuaji, na Jengo la kuhifadhi maiti. Mhe. Gaguti aliwashukuru wananchi kuchangia miradi ya maendeleo na kuwataka kuendelea kuchangia miradi mbalimbali ili kujiletea maendeleo na kuitunza pia miradi hiyo.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa Gaguti alitembelea shamba la kahawa lenye ekari 45 la Mkulima Bw. Shakiru Yahya lililoko Kijijini Karutanga kata ya Magata Karutanga na kujionea kilimo cha Kahawa cha kisasa na chenye tija ambapo shamba hilo ni la mfano kwa wakulima wengine ambao wanajishughulisha na kilimo hasa zao la Kahawa.

Akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa Mkulima wa shamba hilo Bw. Shakiru Yahya alisema kuwa alihamasishwa kulima kahawa na baba yake mzazi wakati akiwa mdogo baada ya baba yake kuwa analima Kahawa na kuuza na kupata fedha za kuendesha familia ikiwa ni pamoja na kuwapatia matumizi mbalimbali ya kifamilia na karo za shule.

Baada ya kujitegemea Bw. Shakiru mwaka 2000 alianza kulima kidogo kidogo na mpaka sasa amefikisha ekari 45 za shamba la mibuni aina ya Arabika na Robusta na amepata mafanikio makubwa kwani kwa msimu uliopita aliweza kuvuna tani 40 za kahawa  na kupata fedha za kitanzania shilingi milioni 60, anasomesha watoto wake, ameajili zaidi wafanyakazi 50, amenunua magari ya kusafirisha mizigo, amenazisha kiwanda cha kusindika kahawa chenye gaharama ya milioni 650.

Mara baada ya kutembelea na kukagua shamba hilo . Gaguti aliwataka wananchi wa Wilaya ya Muleba hasa wanaozunguka shamba hilo kwenda kwa Bw. Shakiru kujifunza kilimo cha Kahawa badala ya kuendelea kumtazama tu. Aidha, Mhe. Gaguti alimshukuru mkulima huyo kwa kuwekeza katika Sekta ya Kilimo na sasa kuanzisha kiwanda ambapo alimhakikishia kuwa Serikali itaendelea kushirikiana naye ili kuhakikisha lengo alilokusudia linatimia.

Katika Ziara hiyo pia Mkuu wa Mkoa aliweza kuongea na Watumishi wa Serikali, Wazee na Wadau mbalimbali wa Maendeleo ya Wilaya ya Muleba ambapo aliwakumbusha watumishi wa umma kuhakikisha wanatatua kero za wananchi kila  Mtumishi katika nafasi yake ili kupunguza migogoro mbalimbali katika jamii na kuwafanya wananchi waiamini Serikali yao.

Mwisho Mhe. Gaguti alitoa msisitizo wa kulipa kodi ya Serikali kwa wadau mbalimbali na wafanyabiasha ambapo alisema kuwa bado hajaridhishwa na kiwango cha ulipaji kodi katika Mkoa wa Kagera. Mhe. Gaguti alisema suala hilo ni kipaumbele chake katika Mkoa na anataka kuona Kagera inaongoza katikaulipaji wa kodi bila shuruti.

Mkuu wa Mkoa Gaguti anaendelea na ziara ya kujitambulisha katika Wilaya za Mkoa wa Kagera ili kuufahamu vizuri mkoa wake na maeneo yake ya utawala  lakini paia anaendelea na ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri za Wilaya.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa