• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

WAZIRI MKUU ATOA SIKU 5 KITUO CHA AFYA KAKUNYU KIANZE KUTOA HUDUMA

Imewekwa : September 22nd, 2023

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi kupeleka vitendea kazi na vifaa tiba kituo cha afya Kakunyu ndani ya siku tano ili kianze kutoa huduma


Akizungumza na wananchi mara baada ya kukagua mradi huo uliogharimu Tsh. milioni 610 kwa fedha za mapato ya ndani na Serikali kuu, unaotarajiwa kuhudumia wakazi wapatao elfu 26 ameeleza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi kila baada ya miezi mitatu inapokea fedha Tsh. milioni 135 kwa ajili ya kununua dawa, hivyo fedha zipo.Halmashauri ikamilishe taratibu za ununuzi wa madawa na vifaa tiba huduma ianze kutolewa


"Nawapa siku 5, jengo hili la mapokezi na magonjwa ya kawaida lianze kazi. Nikimaliza ziara leo mlete samani, vitendea  kazi, madaktari tayari wapo hapa, fedha za madawa zipo hivyo wananchi waanze kupata huduma," ameeleza Mhe. Majaliwa


Ameendelea kueleza kuwa Serikali ya Awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa fedha nyingi kwa Wilaya ya Missenyi ndani ya miaka miwili shule, barabara, zahanati na vituo vya afya vimejengwa. Umeme unaendelea kusambazwa katika vijiji vyote na miradi ya maji imetekelezwa kama ambavyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alidhamiria kumtua mama ndoo kichwani.


Amesisitiza juu ya utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji kwa kuwataka Serikali za Vijiji na kamati za mazingira kusimamia na kuchukua hatua kwa watu wanaoharibu mazingira na vyanzo vya maji ili Nchi iendelee kupata mvua na maji ya kutosha ya matumizi ya majumbani, kilimo na mifugo.


Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tamisemi Dkt. Festo Dugange amemshukuru Waziri Mkuu kwa kufika na kutembelea kituo hicho cha afya huku akieleza kuwa kwa Wilaya ya Missenyi, Rais Dkt. Samia ametoa fedha Tsh. bilioni 4.8 kwa sekta ya afya na kati ya hizo hospitali ya kisasa ya Wilaya imejengwa.


Mbunge wa Jimbo la Nkenge, Florent Kyombo ameeleza kwa miaka miwili shule ya sekondari kubwa ambayo ilikuwa hitaji kubwa la wananchi imejengwa, miradi ya maji na kituo cha afya kimejengwa, vijiji vya Bugango na Kakunyu nguzo za umeme zinajengwa kuwaunganishia umeme wananchi.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa