• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa Aongea na Watumishi Wa Umma na Kutoa Msimamo wa Serikali Katika Utoaji wa Huduma za Jamii Kwa Wananchi

Imewekwa : October 8th, 2018

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kaasim Majaliwa katika siku yake ya tatu akiwa ziarani Mkoani Kagera katika Wilaya ya Biharamulo Oktoba 8, 2018 aongea na watumishi wa umma na kuwakumbusha wajibu wao katika kutekeleza majukumu yao ya kuwahudumia wananchi na kutoa msimamo wa Serikali katika utendaji kazi wa Watumishi.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiongea na watumishi wa umma Wilayani humo aliwakumbusha watumishi wa umma kuwa wanatakiwa kutekeleza majukumu yao kwa matakwa ya Serikali na Kiongozi aliyepo madarakani na kusisitiza kuwa matakwa ya Serikali ya Awamu hii ya Tano ni Hapa Kazi Tu na kila mtumishi anatakiwa kuchapa kazi kwa bidii, kuwa na mpango kazi wa kazi zake na kufanya tathimini ya kazi zake anazozifanya kama zina tija kwa Wananchi.

“Mwananchi anatakiwa kupokelewa, kusikilizwa na kuhudumiwa na Watumishi wa Serikali za Mitaa mnatakiwa kukaa ofisini siku moja na kutumia siku nne kwenda vijijini kuwahudumia wananchi. Wakuu wa Wilaya ambao ndiyo Wakuu wa Shughuli za Serikali Wilayani mnatakiwa kuwasimamia Wakuu wa Idara kuhakikisha wanaenda vijijini kuwahudumia wananchi.” Alisistiza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliwasistiza watumishi kuwa wanatakiwa kuwahudumia wananchi bila kuwabagua kwa njia yoyote ile iwe siasa au kabila ambapo lengo kuu la Serikali likiwa ni kufikisha huduma za kijamii kwa wananchi hao na watumishi ambao hawatawajibika watachukuliwa hatua kulingana na Sheria, kanuni na taratibu.

Ukusanyaji wa Mapato na Matumizi ya Fedha za Serikali Yasiyoridhisha - Biharamulo

Katika utangulizi, Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti akimkaribisha Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuongea na watumishi alisema kuwa yeye kama Mkuu wa Mkoa haridhishwi na ukusanyaji wa mapato na matumizi ya fedha zinazokusanywa na Halmashauri ya Biharamulo na alichukua hatua za kwa kuwachunguza watumishi saba na wawili kati ya hao kuwasimamisha kazi ili kupisha uchunguzi kwa kumagiza Kamanda wa TAKUKURU Mkoa kufanya uchunguzi na kuchukua hatua.

Akiongelea suala hilo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema kuwa Halmashauri za Wilaya zina vyanzo vya mapato viwili, kwanza Mapato ya ndani ambayo yanakusanywa na Halmashauri inatumia fedha hizo katika kusaidia kujazia penye upungufu pale  wananchi wanapokuwa wametekeleza mradi na wananhitaji msaada wa Serikali.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisisitiza kuwa fedha za Serikali za mapato ya ndani katika Halmasauri za Wilaya zinatakiwa kukusanywa kwa mashine za kielektroniki sehemu zote za vyanzo vya kukusanyia mapato. Aidha, watumishi katika Halmashauri wanatakiwa kubuni vyanzo vya mapato na kukusanya mapato hayo na kwa watumishi wanaotakiwa kukusanya lakini hawakusanyi Mkuu wa Mkoa na Wakuu wa Wilaya waliagiza kuwachukua hatua za kisheria.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitoa angalizo kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inaendelea na vita kali ya kupambana na Rushwa kwa hiyo watumishi wanatakiwa kutojihusisha na Rushwa na alimkumbusha Kamanda wa TAKUKURU Mkoa kuwa wameagizwa kuhakikisha wanafanya kazi kila sehemu ili kubaini wala rushwa. Serikali hivi karibuni inatarajia kufanya marekebisho ya Sheria ili Makamanda wa TAKUKURU Mikoa waweze kuwafikisha watuhumiwa Mahakamani badala ya Makao Makuu tu.

Maagizo ya Waziri Mkuu Katika Utoaji wa Huduma za Kijamii Kwa Wananchi Wilayani Biharamulo

ELIMU, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aligiza Idara ya Elimu Wilayani Biharamulo kuhakikisha shule zinagawiwa vitabu na vinatumika kwa wanafunzi kuvisoma ili viwasaidie na si kuvibakiza vitabu hivyo katika makabati tu. Pili, Kuongeza Shule za Kidato cha Tano kama kuna sehemu ina uhitaji wa shule hizo. Nne, kudhibiti tatizo la Mimba za utotoni kuanzia Shule za Msingi hadi Kidato cha Sita na atakayebainika sheria itachukua mkondo wake na adhabu ni miaka 30 Jera.

MAJI, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliwaagiza Waandisi kuhakikisha kuwa wanapotekeleza miradi ya maji wahakikishe pale panapotakiwa kuchimbwa kisima cha maji pawe pamepimwa na kuwa na uhakika wa maji kupatikana hapo na siyo kuchimba tu na mwisho ndiyo inagunduika kuwa hakuna maji wakati fedha za Serkali zimeishatumika.

AFYA, Waziri Mkuu Kasim Majaliwa aliwaagiza Watendaji wa Halmashauri ya Biharamulo kuahakikisha wanawahamasisha wananchi kujenga maboma ya Zahanati katika vijiji na Halmashauri kutoa bati ili kumalizia Zahanati hizo. Waziri Mkuu alisema kuwa Serikali Kuu imejikita katika kuboresha huduma za Afya kwa kuboresha na kujenga vituo vya Afya na tayari Biharamulo wamepata Shilingi Milioni 100 kwa ajili kujenga na kuboresha Vituo vya Afya viwili.

Vilevile Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa alihaidi kuwa Wilaya ya Biharamulo kwa kuwa haina Hospitali ya Wilaya Serikali itatoa shilingi bilioni 1.5 katika awamu ya pili ili Hospitali ya Wilaya iweze kujengwa. Mganga Mkuu wa Wilaya aliagizwa kuhakikisha anasimamia mgawanyo wa dawa katika vituo vya kutolea huduma za Afya na kuwaelimisha wananchi ni dawa zipi zinatakiwa kupatikana katika kila ngazi ya kituo cha kutolea huduma za afya (Zahanati, Kituo cha Afya, Hospitali na Hospitali za Rufaa)

MIUNDOMBINU, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alimwagiza Meneja wa Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) kuhakikisha barabara za Vijijini zinapitika kwa wakati wote wa masika na kiangazi na kuendelea kujenga barabara za mijini kwa kiwango cha rami ili kuboresha maeneo ya miji.

NISHATI YA UMEME,  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imesambaza umeme hadi vijijini ili kutatua tatizo la uharibifu wa mazingira na kumuagiza Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Wilayani Biharamulo kusimamia kikamilifu na kuhakikisha kila mwanachi anapata umeme katika nyumba yake kwa gharama ya shilingi 27,000/= tu.

KILIMO, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliwaagiza Maafisa Kilimo kutoa elimu kwa wananchi ili walime na kuzalisha kwa tija mazao ya chakula na biashara katika maeneo madogo. Aidha, Waziri Mkuu alimuuliza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya  ya Biharamulo Bi Wende Ng’ahala kama agizo lake lilitekelezwa la kuwahamishia Maafisa Kilimo wote vijijini kuwasaidia wananchi ambapo Bi Wende alijibu kuwa agizo hilo halijatekelezwa.

Mkurugezi aliulizwa kuwa anao Maafisa wangapi wa Idara ya Kilimo Ofisini kwake ambapo allijibu kuwa anao Maafisa Wanne na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  aliwataka Maafisa hao kusimama ndani ya ukumbi na kumwagiza Mkurugenzi kuondoka kwenye kikao kwenda kuwaandikia barua za kuhamia vijijini kuwasaidia wananchi katika masuala ya kilimo Maafisa wawili na kubakiza wawili Makao makuu ya Halmashauri.

Mkurugenzi wa Halmshauri ya Wilaya ya Biharamulo Bi Wende  alitekeleza agizo la Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa kwa kuwaandikia barua za uhamisho Maafisa wawili waIdara ya Kilimo ambapo Bw. Juma M. Deja Afisa Kilimo II alihamishishwa kuhudumia Kata ya Nyakatahoka na Nyarubungo, aidha Bw. Bruno Ngawagala Afisa Kilimo Msaidizi Mkuu Ialihamishwa kuhudumia Kata za Bisibo na Nyakiziba.

ARDHI, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliwaagiza Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA) kuweka vigingi vinavyoonekana katika mapori ya Biraharamulo, Burigi na Kimisi (BBK) ili kuondoa migogoro ya ardhi kati ya Shirika hilo na wananchi. Aidha, alimwagiza Meneja wa Mapori ya (BBK) Kagoma Bigiramungu kumrejesha Mhasibu Adamu katika majukumu yake ya Kihasibu na kumuondoa mara moja Bi Ruth Mhifadhi Wanyamapori katika majukumu ya kihasibu na kumrejesha katika majukumu ya  taaluma yake aliyoisomea.

Mwisho Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliuagiza  uongozi wa Wilaya ya Biharamulo kuimarisha ulinzi na Usalama kwani Wilaya hiyo inapakana na nchi jirani na kuruhusu wahamiaji haramu kuingia bila kufuata taratibu kanuni na sheria za nchi.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa