• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Tanzania Mhe. Pinda Akizungumza na Wanafunzi na Watumishi wa Chuo Hicho Mkoani Kagera.

Imewekwa : February 26th, 2018

Waziri Mkuu Mstaafu Aagiza Chuo Kikuu Huria Tanzania Kuanzisha Kozi Fupi Kwa Watumishi Ili Kuendana na Sera ya Viwanda

Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Kayanza Pinda Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Tanzania aagiza chuo hicho kuandaa kozi fupi kwa kada mbalimbali ili kuwawezesha watumishi wa umma kuendana na utekelezaji wa Sera ya Serikali ya Awamu ya Tano ya Serikali ya Viwanda.

Waziri Mkuu Mstaafu Pinda aliyasema Hayo alipofanya ziara Mkaoni Kagera Februari 23, 2018 ili kukagua miundombinu na maendeleo ya Chuo Kikuu Huria Tanzania Tawi la Kagera ambapo alipongeza juhudi za zinazoendelea kuchukuliwa  kukiendeleza chuo hicho Tawi la Kagera.

Akiongea na wanafunzi, watumishi , uongozi wa chuo hicho na uongozi wa Mkoa wa Kagera katika viwanja vya Chuo Kikuu Huria Tawi la kagera  Migera Manispaa ya Bukoba  Waziri mkuu Mstaafu Pinda alisema chuo hicho ni Chuo cha wananchi na kinawafuata wananchi badala ya wananchi kukifuata chuo.

“Chuo hiki ni chuo cha wananchi kwani hakimlazimishi mwananchi kuacha familia yake au mtumishi kuacha majukumu yake ya kazi kwenda kusoma mbali bali mwananchi yeyote atasoma mahali popote alipo kwan i Chuo chetu kina matawi kila Mkoa na kwa sasa kila Wilaya.” Alifafanua Mhe, Pinda.

Mhe. Pinda alisema pia kuwa tayari amemwagiza Makamu Mkuu wa Chuo  Profesa Elphazi Bisanda na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho Profesa Rwekaza Mkandara kuhakikisha wanaangalia uwezekano wa kuandaa kozi fupi kwa watumishi wa umma kama Watendaji wa kata juu ya kusimamia sera ya viwanda pia kozi hizo zitawafanya watumishi waendane na wakati wa Sayansi na Teknolojia.

Mhe. Pinda alitoa mfano wa Nchi ya Korea Kusini kuwa Vyuo Vikuu Huria nchini humo vilisaidia sana katika kuwanoa watumishi ambao  baadae walikuja kutoa mchango mkubwa katika mapinduzi ya kiuchumi na nchi hiyo kupiga hatua kubwa ya kimaendeleo katika Sayansi na Teknolojia .

Katika Kuhitimisha Mhe. Pinda alimwomba Mkuu wa Mkoa Kagera kuhakikisha watumishi wa umma wanaruhusiwa kutumia fursa ya chuo hicho kujiendeleza kielimu, pili aliwaomba wanafunzi wa chuo hichio kusoma kwa bidii ili kupambana na ushindani wa vyuo vingine na ikiwezekana wasome kwa muda muafaka kama vyuo vingine pia mfano badala ya kusoma shahada ya kwaza kwa zaidi ya miaka mitatu iwe mitatu tu.

Naye Makamu Mkuu wa Chuo Huria Tanzania Prof. Elphazi Bisanda alisema kuwa Mkoa wa Kagera una mwitikio mzuri wa wanafunzi wanaojiandikisha kusoma katika chuo hicho. Ambapo alihaidi kuwa matawi zaidi yatazidi kufunguliwa ili chuo kiwafutae wananchi. Tawi jipya linalotarajiwa kufunguliwa ni Katika Wilaya ya Biharamulo.

Prof. Bisanda alihaidi kuwa uongozi unaendelea na juhudi za kuboresha miundombinu ya Chuo Kikuu Huria Tawi la Kagera ili miundombinu hiyo iwe na hadhi ya chuo Kikuu. “ Tunaendelea kuboresha miundombinu ya hapa kadri tunavyopata fedha na nina uhakika kuwa tutaweza kufika tunapopataka. Alifafanua Prof, Bisanda

Naye mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu akimshukuru Mhe. Pinda kwa kuja Kagera kutembelea Chuo Kiku Huria Tawi la Kagera alisema Mkoa wa Kagera ni wa tatu kutoka mwisho kwa umasikini lakini kwa sasa kuna juhudi kubwa zinafanyika ikiwa ni pamoja na kuhamasisha wananchi kujiendeleza ili kuutoa Mkoa kwenye nafasi hiyo ya tatu toka mwisho.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa